Maandamano ya CHADEMA Jijini Mwanza

Maandamano ya CHADEMA Jijini Mwanza

Kwa hiyo maandamano ndio yataleta hospitali?
Vyama vinavyojifanya kujali kwa nini visihamasishe foundations zitakazofanya miradi ya maendeleo kwa mfano?
Maandamano feki ni unafiki tu!

Kweli Tanzania bila Wajinga haiwezekani!!!!!!!!!!!!
 
Huyu ze marcopolo katumwa ye haoni hata umeme umeshashushwa kisa serikali kusikia mandamano ya chadema
 
Walisema lazima dowans ilipwe wathubutu waone

Maandamano kama yanafanyika kwa dhamira njema kwa nia ya kuelezea hisia fulani halali na kwa kuzingatia sheria hayana matatizo. Tatizo litakuja kama baadhi ya wanasiasa wasomi watavuta hisia za watu kutumia kauli mbiyu fulani kutekeleza fikra iliyojiificha. Kwa hili wananchi tunatakiwa kuwa makini. Tusiandamane kwa sababu ya kufanikisha matakwa binafsi ya kisiasa ya watu au kundi la watu fulani na wala tusizuiwe kuandamana kwaajili ya kulinda maslahi ya watu au kundi la watu fulani.

Kabla hatujakubari wala kukataa kushiriki maandamano tunatakiwa kutafakari juu ya uhalali wa dhamira ya maandamano hayo na umhimu wake. Vipindi ambavyo kuna matatizo fulani ya kiuchumi huwa ni hatari sana katika usalama wa nchi. Wakati mwingine wacheza siasa hutumia matatizo hayo kujipatia umaarufu wa haraka na hatimaye kutwaa mamlaka ya kisiasa kwa haraka. Hali kama hii ya kutwaa nguvu za kisiasa kutokana na panic ya wananchi ya kimaisha mara nyingine huweza kuzaa dola ya kidikiteta na hatimaye ikawa ngumu kuin'goa. Utakumbuka kwamba madikiteta kama Mussolin na Hitla walapata umaarufu na hatimaye kutwaa madaraka ya ghafula katika vipindi vya matatizo ya kiuchumi ambapo watu walikuwa na panic ya kimaisha. Watu waliona kila anachokisema Hitla ni muarubaini wa matatizo ya kiuchumi. Matokeo yake alijizolea upendo kwa watu na kutwaa nchi kwa vigelegele. Baadaye wananchi walijikuta wakijuta.

Sina wasiwasi sana na wanasiasa mbalimbali tulio nao. Lakini binaadamu hubadilika kutokana na mazingira. Ni bora wananchi tukawa macho kuangalia kila upande na kuchukua tahadhari zote. Kila kinachosemwa tukiangalie katika pande zake mbili. Mtu kwa macho yako unaweza kuona matatizo mawili lakini kutokana na umahili wa kalamu au mdomo wa mwanasiasa unaweza matatizo mawili ukayaona milioni. Mtu unaweza kujisikia unaumwa kichwa kidogo lakini kutokana na umahili wa uzungumzaji wa mwanasiasa ukajihisi huwezi hata kupumua bila msaada wa mashine.
 
Kweli tunataka mabadiliko! watanzania hatuombi bali tunataka katiba mpya kwa lazima! haki haiombwi mahali popote! haki inadaiwa!
 
mnapoeza muda wa watu kufanya kazi. Watu wanataka barabara, hospitali, shule bora n.k. Hawataki maandamano.
Acheni uzushi, kahamasisheni shughuli za maendeleo.

libya wamepata zaidi ya hivyo unavyo sema uchumi nia mrama 11 kutuzidi!! Kachunguzwe akili, naskia kuna orodha ya wana ccm ambao wamechukuliwa mizukule na shekhe yahya, sije kuwa we ni mmoja wapo?
 
Ukitaka kumpima mtu upeo unaweza kuanza na jina analo tumia na kulitafakari, ZEMARCOPOLO huyu jamaa alikuwa mtembezi, au ni jina maalumu lilipewa aina fulani ya mabasi, sasa nina hakika huyu jamaa ali refer mabasi ndo akajiita jina hili,

Sasa kurudi kwenye mada...!!!!!!Nyerere aliwahi kusema katika moja ya hotuba zake HAKUNA KITU KIGUMU KAMA KUONGOZA WAJINGA, na hakuna kitu kibaya kuongozana na mpumbavu akatafsiri mpumbavu ni mtu wa namna gani 9 hapa atatafuta maana mwenenyewe) sasa kwa habari ya ukombozo wa taifa letu, lazima watu wa jinsi hii wawepo, mimi nimemsamehe na wanaharakati wote wa maendeleo pls naomba msamaha kwa niaba yake (Zemarcopolo) mumsamehe..! HANA AKILI NI MJINGA TU JAMANI......!!!! hila ni muhimu kwakuwa analeta challenge
 
nlishuhudia kabla ya mkutano zilitokea ajal mbya sana za pikipiki hapo hapo furahisha!
 
Nifahamisheni nyie muliyouona tu mkataba wa dowans, kifungu gani cha mkataba ni kibaya na inapashwa kiweje
 
Dada Regia, mimi mwanachama wa chadema. Lakini naanza kupata mashaka na agenda mliyonayo viongozi wetu hii ya kuandamana. Siogopi maandamano ila sidhani kama ni muda muafaka. Tumieni njia mbadala kuimarisha chama na sio hii inaleta mtazamo hasi na kukitenga chama na kundi flani kubwa la watu ambao kwa kiasi kikubwa kwa kutokuamini upinzani unaweza kufanya kile unachoahidi, waliipa kura ccm mwaka jana na kuirudisha madarakani japo wameshaichoka sana. Lazima tukubali ukweli, ccm bado inakubalika sana. Unaweza kuona Bungeni walivyofunika, ok hata ukisema walituibia viti 20 vya ubunge bado upinzani hauna nguvu. Maandamano na migomo haiwezi kuwang'oa kwa sababu ni wachache ndio wataunga mkono. Tena leo CCM wakiamka wakafunga mjadala wa Dowans, wakawafikisha mafisadi kadhaa kizimbani(kama ilivyofanya kwa kina Mramba), upinzani wote utanyong'onye. Hebu tutafute sera za kudumu tuachane na vivuli vya matukio ya mpito. Kwa hiyo staili yenu, mnapunguza kasi ya ukombozi wa Taifa hili. Muda wa maandamano sio sasa, msirubuniwe na wachache wanaowazunguka ambao ni waelewa, wasomi na walio karibu na vyombo vya habari. Watanzania wengi hawako pamoja na nyie hata kidogo. Na siku CCM ikiamua kutusambaratisha litakua ni pigo takatifu na hatutasimama tena. Mwambie Dk Slaa, ths will never work out!!
 
Mnapoeza muda wa watu kufanya kazi. Watu wanataka barabara, hospitali, shule bora n.k. Hawataki maandamano.
Acheni uzushi, kahamasisheni shughuli za maendeleo.

Kwa hali ilivyo ni lazima watu waingie mtaani ili kupata barabara, hospitali, shule bora n.k kama ulivyo tambua.
Haki yako hupewi - unaichukua kwa nguvu.
 
Cha msingi sio kujua theme bali ni kujiuliza jamii itanufaika vipi na maandamano hayo na je, jitihada zinazotumika kuandaa maandamano zisingeweza kutumika kuleta manufaa zaidi? Hawa wote wanafiki tu!

A real man knows when to keep his biggest hole shut. You do not seem to be that kind of a man.
 
Maandamano kama yanafanyika kwa dhamira njema kwa nia ya kuelezea hisia fulani halali na kwa kuzingatia sheria hayana matatizo. Tatizo litakuja kama baadhi ya wanasiasa wasomi watavuta hisia za watu kutumia kauli mbiyu fulani kutekeleza fikra iliyojiificha. Kwa hili wananchi tunatakiwa kuwa makini. Tusiandamane kwa sababu ya kufanikisha matakwa binafsi ya kisiasa ya watu au kundi la watu fulani na wala tusizuiwe kuandamana kwaajili ya kulinda maslahi ya watu au kundi la watu fulani.

Kabla hatujakubari wala kukataa kushiriki maandamano tunatakiwa kutafakari juu ya uhalali wa dhamira ya maandamano hayo na umhimu wake. Vipindi ambavyo kuna matatizo fulani ya kiuchumi huwa ni hatari sana katika usalama wa nchi. Wakati mwingine wacheza siasa hutumia matatizo hayo kujipatia umaarufu wa haraka na hatimaye kutwaa mamlaka ya kisiasa kwa haraka. Hali kama hii ya kutwaa nguvu za kisiasa kutokana na panic ya wananchi ya kimaisha mara nyingine huweza kuzaa dola ya kidikiteta na hatimaye ikawa ngumu kuin'goa. Utakumbuka kwamba madikiteta kama Mussolin na Hitla walapata umaarufu na hatimaye kutwaa madaraka ya ghafula katika vipindi vya matatizo ya kiuchumi ambapo watu walikuwa na panic ya kimaisha. Watu waliona kila anachokisema Hitla ni muarubaini wa matatizo ya kiuchumi. Matokeo yake alijizolea upendo kwa watu na kutwaa nchi kwa vigelegele. Baadaye wananchi walijikuta wakijuta.

Sina wasiwasi sana na wanasiasa mbalimbali tulio nao. Lakini binaadamu hubadilika kutokana na mazingira. Ni bora wananchi tukawa macho kuangalia kila upande na kuchukua tahadhari zote. Kila kinachosemwa tukiangalie katika pande zake mbili. Mtu kwa macho yako unaweza kuona matatizo mawili lakini kutokana na umahili wa kalamu au mdomo wa mwanasiasa unaweza matatizo mawili ukayaona milioni. Mtu unaweza kujisikia unaumwa kichwa kidogo lakini kutokana na umahili wa uzungumzaji wa mwanasiasa ukajihisi huwezi hata kupumua bila msaada wa mashine.
You have raised important points but the truth remains and that is change require force - in science or sociology.
 
Dada Regia, mimi mwanachama wa chadema. Lakini naanza kupata mashaka na agenda mliyonayo viongozi wetu hii ya kuandamana. Siogopi maandamano ila sidhani kama ni muda muafaka. Tumieni njia mbadala kuimarisha chama na sio hii inaleta mtazamo hasi na kukitenga chama na kundi flani kubwa la watu ambao kwa kiasi kikubwa kwa kutokuamini upinzani unaweza kufanya kile unachoahidi, waliipa kura ccm mwaka jana na kuirudisha madarakani japo wameshaichoka sana. Lazima tukubali ukweli, ccm bado inakubalika sana. Unaweza kuona Bungeni walivyofunika, ok hata ukisema walituibia viti 20 vya ubunge bado upinzani hauna nguvu. Maandamano na migomo haiwezi kuwang'oa kwa sababu ni wachache ndio wataunga mkono. Tena leo CCM wakiamka wakafunga mjadala wa Dowans, wakawafikisha mafisadi kadhaa kizimbani(kama ilivyofanya kwa kina Mramba), upinzani wote utanyong'onye. Hebu tutafute sera za kudumu tuachane na vivuli vya matukio ya mpito. Kwa hiyo staili yenu, mnapunguza kasi ya ukombozi wa Taifa hili. Muda wa maandamano sio sasa, msirubuniwe na wachache wanaowazunguka ambao ni waelewa, wasomi na walio karibu na vyombo vya habari. Watanzania wengi hawako pamoja na nyie hata kidogo. Na siku CCM ikiamua kutusambaratisha litakua ni pigo takatifu na hatutasimama tena. Mwambie Dk Slaa, ths will never work out!!

Kuwa mwanachama haina maana unaamini ktk kile ambacho chama hicho kinapigania/simamia. Watz wengi wanajiunga na chama si kwa sababu ya itikadi, bali kwa ajili ya vyeo, umaarufu na mkumbo. Je ni wanachama wangap wanajua sera na katiba za vyama vyao?

Nadhani muono hasi dhidi ya maandamano ni uoga tu. Ni nidhamu ya uoga ambayo imetamalaki miongoni mwa watz toka zamani. Mbona hutuambii njia mbadala? Mbona hujiulizi kipi kimefanya chadema kuinuka ghafla? Unaikumbuka operesheni sangara?

Maandamano ni njia pekee ambayo inaeleweka kwa CCM na ndio maana wanaruhusu kwa shingo upande. Kwa jinsi maisha yalivyo magumu, hatuwezi kuendelea kutumia mbinu zilezile za miaka yote,maandamano ndio strategy mpya inayoweza kututoa. Mtaji mkubwa wa chadema ni vjana ambao msimamo wao sio wa kutiliwa shaka wala kudanganywa na propaganda, hao wengine watakuja taratibu baada ya maisha kuwaonyesha ukatili.

Mwisho mimi sio mwanachama wa chama chochote na sitarajii kujiunga na chochote, ila chama cha ukweli chenye nia na uwezo wa kuwatoa wananchi nakijua na nakiunga mkono hata nikiwa ndotoni. Na pia nawaelimisha na kuhamasisha wengine waliokaribu yangu wakiunge mkono na kuchangia maendeleo yk.
 
Back
Top Bottom