Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 8,943
- 6,863
However, huyu Tutu hana credibility kabisaa zaidi ya hiyo Nobel thing ambayo hata Carter alipewa, huyu nasikia ndiye chanzo cha Mandela kuachana na mkewe Winnie, nasikia amegeuka kuwa agent wa makaburu ambao ndio hasa wasiomtak Zuma, hivi exactly ni nani aliyemtuma huko Kenya, au ni kihere here tu!
Haujui unachoongelea. The only credible person sasa hivi ni Tutu. Tutu ndiye pekee aliyeweza kumkemea Mandela ilpopendekezwa alipwe mshahara wa ajabu mara baada ya kushinda uchaguzi, Mandiba akamsikiliza na wakampunguza mshahara. Ni Tutu aliyemkemea tena Mandiba kwa kufanya kimada Gracia, naye akamsikiliza akafunga naye ndoa. Ni Tutu alikemea mashambulizi ya marekani Iraq. Ni Tutu aliyemwita Mugabe kikaragosi cha madikteta wa kiafrika ( au maneno kama hayo) kutokana na vitendo anavyovifanya. Ni Tutu aliyesema WOTE wawili, yaani Mbeki na Zuma hawafai kutokana na matendo yao. Ni Tutu ambaye amewaambia wazi viongozi wa kanisa lake la kianglikana kuwa wanapoteza wakati muhimu kushupalia masuala ya ushoga wakati hapa duniani kuna matatizo mengi makubwa zaidi. Tutu haogopi mtu. Tutu anasema ukweli anavyouona bila kujali ataeleweka vipi. Kumuita kibaraka wa makaburu ni kumtukana na kumwonea huyu shujaa wa Afrika. Unaiponda Nobel kwa sababu walipewa Tutu na Carter! Ulitaka apewe George W Bush ndiyo uiheshimu? Samahani kwa kutoka nje ya mada lakini hili sikuweza kuliachia lipite.