KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,590
- 4,603
Hii ni kwa vyama vyote vinavyoshiriki uchaguzi ,uwe uchaguzi mdogo, uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu. Kila chama ni muhimu kufanya maandalizi ili kuepuka kutupa lawama kusikostahili.
Kwanza, Kila chama kinatakiwa kihakikishe kina wanachama wafia chama ambao watakuwa pamoja na Chama nyakati zote. Mtaji wa wanachama wafia chama ni hakikisho sahihi la chama kushinda kirahisi.
Pili, Kila chama kihakikishe kinakuwa na mpangokazi wa muda mrefu wa mipango, mikakati na mbinu za ushindi. Chama kushiriki uchaguzi bila kuwa na mpangokazi wa ushindi ni kufanya jaribio la kushindwa.
Tatu, wakati wa kampeni Kila chama kijielekeze kwenye sera na sio lawama Kwa sababu unapotumia muda mwingi kulaumu utakosa muda wa kutangaza sera.
Nne, ahadi zinazotekelezeka. Wapigakura wanatamani kusikia na kuahidiwa vinavyotekelezeka hata kama Ahadi zisizotekelezeka zinaweza kuwa tamu zaidi. Kwa mfano, mmoja kuahidi watu kusema Bure mpaka chuo kikuu na mwingine kuahidi watu kusoma Bure Hadi kidato Cha nne, atachaguliwa aliyeahidi kusomesha Bure Hadi kidato Cha nne hata kama kusomeshwa Bure Hadi chuo kikuu ni vizuri zaidi lakini utekelezaji wake sio rahisi.
Tano, Kila chama kihakikishe wanachama wake wenye umri wa kupigakura wameandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapigakura. Kuwa na wananchi wengi lakini hawaandikishwa ni kazi bure maana hawatakuwa na uwezo wa kupiga kura.
Sita, Chama kisimamishe wagombea wanaouzika kirahisi ili iwe ni rahisi kuwanadi wakati wa kampeni. Wagombea wenye kashfa za rushwa, ufisadi n.k itahitaji kusafishwa kwanza ili wanadiwe. Kipindi cha kampeni ni kifupi kufanya yote hayo.
Saba, Kila chama kihakikishe kinaweka mawakala wa kusimamia upigaji na kuhesabu kura.
Nane, vyama vinavyoshindwa vikubali kushindwa na kusonga mbele, warekebishe kasoro zilizopelekea kushindwa na wajipange vema Kwa uchaguzi ujao. Kukaa miaka mitano unalalamika umeibiwa kura, inakufanya uoneshe udhaifu mkubwa ulionao wa kutokukubali matokeo na Hilo litapelekea kushindwa kesho na kesho kama usipoweza kurekebisha.
Kwanza, Kila chama kinatakiwa kihakikishe kina wanachama wafia chama ambao watakuwa pamoja na Chama nyakati zote. Mtaji wa wanachama wafia chama ni hakikisho sahihi la chama kushinda kirahisi.
Pili, Kila chama kihakikishe kinakuwa na mpangokazi wa muda mrefu wa mipango, mikakati na mbinu za ushindi. Chama kushiriki uchaguzi bila kuwa na mpangokazi wa ushindi ni kufanya jaribio la kushindwa.
Tatu, wakati wa kampeni Kila chama kijielekeze kwenye sera na sio lawama Kwa sababu unapotumia muda mwingi kulaumu utakosa muda wa kutangaza sera.
Nne, ahadi zinazotekelezeka. Wapigakura wanatamani kusikia na kuahidiwa vinavyotekelezeka hata kama Ahadi zisizotekelezeka zinaweza kuwa tamu zaidi. Kwa mfano, mmoja kuahidi watu kusema Bure mpaka chuo kikuu na mwingine kuahidi watu kusoma Bure Hadi kidato Cha nne, atachaguliwa aliyeahidi kusomesha Bure Hadi kidato Cha nne hata kama kusomeshwa Bure Hadi chuo kikuu ni vizuri zaidi lakini utekelezaji wake sio rahisi.
Tano, Kila chama kihakikishe wanachama wake wenye umri wa kupigakura wameandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapigakura. Kuwa na wananchi wengi lakini hawaandikishwa ni kazi bure maana hawatakuwa na uwezo wa kupiga kura.
Sita, Chama kisimamishe wagombea wanaouzika kirahisi ili iwe ni rahisi kuwanadi wakati wa kampeni. Wagombea wenye kashfa za rushwa, ufisadi n.k itahitaji kusafishwa kwanza ili wanadiwe. Kipindi cha kampeni ni kifupi kufanya yote hayo.
Saba, Kila chama kihakikishe kinaweka mawakala wa kusimamia upigaji na kuhesabu kura.
Nane, vyama vinavyoshindwa vikubali kushindwa na kusonga mbele, warekebishe kasoro zilizopelekea kushindwa na wajipange vema Kwa uchaguzi ujao. Kukaa miaka mitano unalalamika umeibiwa kura, inakufanya uoneshe udhaifu mkubwa ulionao wa kutokukubali matokeo na Hilo litapelekea kushindwa kesho na kesho kama usipoweza kurekebisha.