Maamuzi ya CHADEMA Kuandika Barua UN, US, EU, AU, EAC ni sawa na kupaka rangi upepo.

Maamuzi ya CHADEMA Kuandika Barua UN, US, EU, AU, EAC ni sawa na kupaka rangi upepo.

Getrude Mollel

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2022
Posts
308
Reaction score
424
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza mpango wa kuandika barua kwa mashirika ya kimataifa Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Ulaya (EU), Marekani (US), Umoja wa Afrika (AU) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kikilalamikia mifumo ya uchaguzi.

Kulingana na Makamu Mwenyekiti wake, John Heche, chama hicho kinadai mifumo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeunganishwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa manufaa ya CCM.

Lakini historia yenye inaonesha kwamba barua na lundo la Malalamiko inaonesha wazi kwamba hayabadilisha chochote.

Tanzania ni taifa huru lenye katiba na mamlaka ya kujiamulia mambo yake. Jumuiya za kimataifa, hata zenye ushawishi mkubwa kama UN, haziwezi kufanya kazi ndani ya nchi bila ridhaa ya serikali husika. Hii ni kanuni ya msingi ya kidiplomasia uhuru wa mataifa (sovereignty),na Tanzania imekuwa mstari wa mbele kuilinda.

Historia ya Malalamiko ya CHADEMA nje ya nchi

CHADEMA imekuwa na rekodi ndefu ya kutumia njia ya barua na malalamiko kwa mashirika ya kimataifa. Mifano kadhaa inathibitisha namna juhudi hizo zimekuwa zikikosa matokeo tarajiwa.

Sheria za Uchaguzi: Mwaka 2019, CHADEMA iliandika barua Umoja wa Mataifa kupinga marekebisho ya Sheria ya Uchaguzi, wakidai yalilenga kubana upinzani. Hata hivyo, hakuna hatua iliyochukuliwa, na mabadiliko hayo yalitekelezwa kwa mujibu wa bunge na mamlaka ya kitaifa.

Kuhamishwa kwa wamasai Ngorongoro: KKatika hatua na mkakati wa serikali kulinda hifadhi ya Ngorongor, CHADEMA na mashirika ya kimataifa na washirika wengine walipeleka malalamiko UN wakipinga mpango wa serikali kuhamisha baadhi ya wamasai hao kutoka kwenye hifadhi. Licha ya mijadala mikali, serikali iliendelea na mpango wake, na chadema haikuambia kitu.

Mikopo ya nje: CHADEMA pia iliwahi kuandika barua kwa taasisi za kifedha za kimataifa kama IMF na Benki ya Dunia (WB) kuomba mikopo ya maendeleo isimamishwe. Lakini mwaka 2021 na 2022 pekee, Tanzania ilipokea zaidi ya USD 1.3 bilioni kutoka IMF kwa ajili ya kufufua uchumi baada ya janga la COVID-19. Hii ilionyesha kwamba taasisi za kifedha huangalia uhalali wa miradi na uwezo wa taifa kurejesha fedha, si shinikizo la vyama vya siasa.

FIFA na CAF dhidi ya Yanga: Hivi karibuni, baada ya klabu ya Yanga kuchangia shilingi milioni 100 kwenye harambe ya CCM ya kuchangia za uchaguzi wa mwaka huu, CHADEMA walilalamika FIFA na CAF wakidai ni ukiukwaji wa misingi ya michezo kwa klabu kushiriki siasa. Lakini FIFA haikuchukua hatua yoyote, kwa sababu haina mamlaka kuingilia masuala ya kisiasa ya ndani pasipo ushahidi wa uvunjifu wa kanuni zake.

Kwanini nasema ni sawa kupaka rangi upepo?

Sababu kuu za Chadema kuangukia pua mara kwa mara ukweli kwamba hakuna taasisi ya kimataifa itakayohatarisha uhusiano wake na Tanzania kwa ajili ya malalamiko ya chama kimoja cha siasa.

Tanzania ni nchi yenye uchumi unaokua kwa wastani wa zaidi ya 5% kwa mwaka, na ni kitovu cha biashara katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Diplomasia ya Tanzania inajengwa juu ya misingi ya kutoshirikiana na mashirika yanayoweza kuhatarisha uthabiti wake wa ndani. Ndiyo maana, mara zote, barua za CHADEMA zimeishia kuwa maandiko yasiyo na impact yeyote. Kwa wa kihistoria na takwimu, barua ya CHADEMA kwa UN, US, EU, AU na EAC hazitazaa matunda yoyote, wanafanya kazi ya bure isiyo na matokeo kama vile kupaka rangi upepo.
 
Screenshot_20250725-185609~2.png
 
ikiwa hakuna sheria wamevunja wapo huru kufanya wafanyalo Mbona kuna waliopo madarakani miaka zaidi ya 60 na nchi haifanani na Singapore ama Malaysia
ndo tuseme nao ni rundo la miaka ya utawala isiyo na matokeo chanya?
 
ikiwa hakuna sheria wamevunja wapo huru kufanya wafanyalo Mbona kuna waliopo madarakani miaka zaidi ya 60 na nchi haifanani na Singapore ama Malaysia
ndo tuseme nao ni rundo la miaka ya utawala isiyo na matokeo chanya?
Hili jibu ulilompa ni kama gunia la misumari kwenye kichwa cmake🤣🤣🤣🤣
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza mpango wa kuandika barua kwa mashirika ya kimataifa Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Ulaya (EU), Marekani (US), Umoja wa Afrika (AU) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kikilalamikia mifumo ya uchaguzi.

Kulingana na Makamu Mwenyekiti wake, John Heche, chama hicho kinadai mifumo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeunganishwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa manufaa ya CCM.

Lakini historia yenye inaonesha kwamba barua na lundo la Malalamiko inaonesha wazi kwamba hayabadilisha chochote.

Tanzania ni taifa huru lenye katiba na mamlaka ya kujiamulia mambo yake. Jumuiya za kimataifa, hata zenye ushawishi mkubwa kama UN, haziwezi kufanya kazi ndani ya nchi bila ridhaa ya serikali husika. Hii ni kanuni ya msingi ya kidiplomasia uhuru wa mataifa (sovereignty),na Tanzania imekuwa mstari wa mbele kuilinda.

Historia ya Malalamiko ya CHADEMA nje ya nchi

CHADEMA imekuwa na rekodi ndefu ya kutumia njia ya barua na malalamiko kwa mashirika ya kimataifa. Mifano kadhaa inathibitisha namna juhudi hizo zimekuwa zikikosa matokeo tarajiwa.

Sheria za Uchaguzi: Mwaka 2019, CHADEMA iliandika barua Umoja wa Mataifa kupinga marekebisho ya Sheria ya Uchaguzi, wakidai yalilenga kubana upinzani. Hata hivyo, hakuna hatua iliyochukuliwa, na mabadiliko hayo yalitekelezwa kwa mujibu wa bunge na mamlaka ya kitaifa.

Kuhamishwa kwa wamasai Ngorongoro: KKatika hatua na mkakati wa serikali kulinda hifadhi ya Ngorongor, CHADEMA na mashirika ya kimataifa na washirika wengine walipeleka malalamiko UN wakipinga mpango wa serikali kuhamisha baadhi ya wamasai hao kutoka kwenye hifadhi. Licha ya mijadala mikali, serikali iliendelea na mpango wake, na chadema haikuambia kitu.

Mikopo ya nje: CHADEMA pia iliwahi kuandika barua kwa taasisi za kifedha za kimataifa kama IMF na Benki ya Dunia (WB) kuomba mikopo ya maendeleo isimamishwe. Lakini mwaka 2021 na 2022 pekee, Tanzania ilipokea zaidi ya USD 1.3 bilioni kutoka IMF kwa ajili ya kufufua uchumi baada ya janga la COVID-19. Hii ilionyesha kwamba taasisi za kifedha huangalia uhalali wa miradi na uwezo wa taifa kurejesha fedha, si shinikizo la vyama vya siasa.

FIFA na CAF dhidi ya Yanga: Hivi karibuni, baada ya klabu ya Yanga kuchangia shilingi milioni 100 kwenye harambe ya CCM ya kuchangia za uchaguzi wa mwaka huu, CHADEMA walilalamika FIFA na CAF wakidai ni ukiukwaji wa misingi ya michezo kwa klabu kushiriki siasa. Lakini FIFA haikuchukua hatua yoyote, kwa sababu haina mamlaka kuingilia masuala ya kisiasa ya ndani pasipo ushahidi wa uvunjifu wa kanuni zake.

Kwanini nasema ni sawa kupaka rangi upepo?

Sababu kuu za Chadema kuangukia pua mara kwa mara ukweli kwamba hakuna taasisi ya kimataifa itakayohatarisha uhusiano wake na Tanzania kwa ajili ya malalamiko ya chama kimoja cha siasa.

Tanzania ni nchi yenye uchumi unaokua kwa wastani wa zaidi ya 5% kwa mwaka, na ni kitovu cha biashara katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Diplomasia ya Tanzania inajengwa juu ya misingi ya kutoshirikiana na mashirika yanayoweza kuhatarisha uthabiti wake wa ndani. Ndiyo maana, mara zote, barua za CHADEMA zimeishia kuwa maandiko yasiyo na impact yeyote. Kwa wa kihistoria na takwimu, barua ya CHADEMA kwa UN, US, EU, AU na EAC hazitazaa matunda yoyote, wanafanya kazi ya bure isiyo na matokeo kama vile kupaka rangi upepo.
Wameandika barua nyingi za namna hiyo na hakuna la maana wanachopata.Adui wa chadema ni viongozi wao
 
Mwandiko wa vijana wa Masaki, kwenye OFisi za Dulla! Nasubiri Polepole atupatie GPS location yenu tuwasalimie kama majirani wema!
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza mpango wa kuandika barua kwa mashirika ya kimataifa Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Ulaya (EU), Marekani (US), Umoja wa Afrika (AU) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kikilalamikia mifumo ya uchaguzi.

Kulingana na Makamu Mwenyekiti wake, John Heche, chama hicho kinadai mifumo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeunganishwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa manufaa ya CCM.

Lakini historia yenye inaonesha kwamba barua na lundo la Malalamiko inaonesha wazi kwamba hayabadilisha chochote.

Tanzania ni taifa huru lenye katiba na mamlaka ya kujiamulia mambo yake. Jumuiya za kimataifa, hata zenye ushawishi mkubwa kama UN, haziwezi kufanya kazi ndani ya nchi bila ridhaa ya serikali husika. Hii ni kanuni ya msingi ya kidiplomasia uhuru wa mataifa (sovereignty),na Tanzania imekuwa mstari wa mbele kuilinda.

Historia ya Malalamiko ya CHADEMA nje ya nchi

CHADEMA imekuwa na rekodi ndefu ya kutumia njia ya barua na malalamiko kwa mashirika ya kimataifa. Mifano kadhaa inathibitisha namna juhudi hizo zimekuwa zikikosa matokeo tarajiwa.

Sheria za Uchaguzi: Mwaka 2019, CHADEMA iliandika barua Umoja wa Mataifa kupinga marekebisho ya Sheria ya Uchaguzi, wakidai yalilenga kubana upinzani. Hata hivyo, hakuna hatua iliyochukuliwa, na mabadiliko hayo yalitekelezwa kwa mujibu wa bunge na mamlaka ya kitaifa.

Kuhamishwa kwa wamasai Ngorongoro: KKatika hatua na mkakati wa serikali kulinda hifadhi ya Ngorongor, CHADEMA na mashirika ya kimataifa na washirika wengine walipeleka malalamiko UN wakipinga mpango wa serikali kuhamisha baadhi ya wamasai hao kutoka kwenye hifadhi. Licha ya mijadala mikali, serikali iliendelea na mpango wake, na chadema haikuambia kitu.

Mikopo ya nje: CHADEMA pia iliwahi kuandika barua kwa taasisi za kifedha za kimataifa kama IMF na Benki ya Dunia (WB) kuomba mikopo ya maendeleo isimamishwe. Lakini mwaka 2021 na 2022 pekee, Tanzania ilipokea zaidi ya USD 1.3 bilioni kutoka IMF kwa ajili ya kufufua uchumi baada ya janga la COVID-19. Hii ilionyesha kwamba taasisi za kifedha huangalia uhalali wa miradi na uwezo wa taifa kurejesha fedha, si shinikizo la vyama vya siasa.

FIFA na CAF dhidi ya Yanga: Hivi karibuni, baada ya klabu ya Yanga kuchangia shilingi milioni 100 kwenye harambe ya CCM ya kuchangia za uchaguzi wa mwaka huu, CHADEMA walilalamika FIFA na CAF wakidai ni ukiukwaji wa misingi ya michezo kwa klabu kushiriki siasa. Lakini FIFA haikuchukua hatua yoyote, kwa sababu haina mamlaka kuingilia masuala ya kisiasa ya ndani pasipo ushahidi wa uvunjifu wa kanuni zake.

Kwanini nasema ni sawa kupaka rangi upepo?

Sababu kuu za Chadema kuangukia pua mara kwa mara ukweli kwamba hakuna taasisi ya kimataifa itakayohatarisha uhusiano wake na Tanzania kwa ajili ya malalamiko ya chama kimoja cha siasa.

Tanzania ni nchi yenye uchumi unaokua kwa wastani wa zaidi ya 5% kwa mwaka, na ni kitovu cha biashara katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Diplomasia ya Tanzania inajengwa juu ya misingi ya kutoshirikiana na mashirika yanayoweza kuhatarisha uthabiti wake wa ndani. Ndiyo maana, mara zote, barua za CHADEMA zimeishia kuwa maandiko yasiyo na impact yeyote. Kwa wa kihistoria na takwimu, barua ya CHADEMA kwa UN, US, EU, AU na EAC hazitazaa matunda yoyote, wanafanya kazi ya bure isiyo na matokeo kama vile kupaka rangi upepo.
Policies do change....wa leo sio wa jana! You try whatever is at your disposal
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza mpango wa kuandika barua kwa mashirika ya kimataifa Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Ulaya (EU), Marekani (US), Umoja wa Afrika (AU) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kikilalamikia mifumo ya uchaguzi.

Kulingana na Makamu Mwenyekiti wake, John Heche, chama hicho kinadai mifumo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeunganishwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa manufaa ya CCM.

Lakini historia yenye inaonesha kwamba barua na lundo la Malalamiko inaonesha wazi kwamba hayabadilisha chochote.

Tanzania ni taifa huru lenye katiba na mamlaka ya kujiamulia mambo yake. Jumuiya za kimataifa, hata zenye ushawishi mkubwa kama UN, haziwezi kufanya kazi ndani ya nchi bila ridhaa ya serikali husika. Hii ni kanuni ya msingi ya kidiplomasia uhuru wa mataifa (sovereignty),na Tanzania imekuwa mstari wa mbele kuilinda.

Historia ya Malalamiko ya CHADEMA nje ya nchi

CHADEMA imekuwa na rekodi ndefu ya kutumia njia ya barua na malalamiko kwa mashirika ya kimataifa. Mifano kadhaa inathibitisha namna juhudi hizo zimekuwa zikikosa matokeo tarajiwa.

Sheria za Uchaguzi: Mwaka 2019, CHADEMA iliandika barua Umoja wa Mataifa kupinga marekebisho ya Sheria ya Uchaguzi, wakidai yalilenga kubana upinzani. Hata hivyo, hakuna hatua iliyochukuliwa, na mabadiliko hayo yalitekelezwa kwa mujibu wa bunge na mamlaka ya kitaifa.

Kuhamishwa kwa wamasai Ngorongoro: KKatika hatua na mkakati wa serikali kulinda hifadhi ya Ngorongor, CHADEMA na mashirika ya kimataifa na washirika wengine walipeleka malalamiko UN wakipinga mpango wa serikali kuhamisha baadhi ya wamasai hao kutoka kwenye hifadhi. Licha ya mijadala mikali, serikali iliendelea na mpango wake, na chadema haikuambia kitu.

Mikopo ya nje: CHADEMA pia iliwahi kuandika barua kwa taasisi za kifedha za kimataifa kama IMF na Benki ya Dunia (WB) kuomba mikopo ya maendeleo isimamishwe. Lakini mwaka 2021 na 2022 pekee, Tanzania ilipokea zaidi ya USD 1.3 bilioni kutoka IMF kwa ajili ya kufufua uchumi baada ya janga la COVID-19. Hii ilionyesha kwamba taasisi za kifedha huangalia uhalali wa miradi na uwezo wa taifa kurejesha fedha, si shinikizo la vyama vya siasa.

FIFA na CAF dhidi ya Yanga: Hivi karibuni, baada ya klabu ya Yanga kuchangia shilingi milioni 100 kwenye harambe ya CCM ya kuchangia za uchaguzi wa mwaka huu, CHADEMA walilalamika FIFA na CAF wakidai ni ukiukwaji wa misingi ya michezo kwa klabu kushiriki siasa. Lakini FIFA haikuchukua hatua yoyote, kwa sababu haina mamlaka kuingilia masuala ya kisiasa ya ndani pasipo ushahidi wa uvunjifu wa kanuni zake.

Kwanini nasema ni sawa kupaka rangi upepo?

Sababu kuu za Chadema kuangukia pua mara kwa mara ukweli kwamba hakuna taasisi ya kimataifa itakayohatarisha uhusiano wake na Tanzania kwa ajili ya malalamiko ya chama kimoja cha siasa.

Tanzania ni nchi yenye uchumi unaokua kwa wastani wa zaidi ya 5% kwa mwaka, na ni kitovu cha biashara katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Diplomasia ya Tanzania inajengwa juu ya misingi ya kutoshirikiana na mashirika yanayoweza kuhatarisha uthabiti wake wa ndani. Ndiyo maana, mara zote, barua za CHADEMA zimeishia kuwa maandiko yasiyo na impact yeyote. Kwa wa kihistoria na takwimu, barua ya CHADEMA kwa UN, US, EU, AU na EAC hazitazaa matunda yoyote, wanafanya kazi ya bure isiyo na matokeo kama vile kupaka rangi upepo.
Ni wazi hapakuwa na mkakati wa kuzuia uchaguzi. Kinachofanyika ni kuweka kumbukumbu kwamba walijitokeza kupigania haki hata kama mbinu waliyochagua haikuwa inatekelezeka.
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza mpango wa kuandika barua kwa mashirika ya kimataifa Umoja wa Mataifa (UN), Umoja wa Ulaya (EU), Marekani (US), Umoja wa Afrika (AU) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kikilalamikia mifumo ya uchaguzi.

Kulingana na Makamu Mwenyekiti wake, John Heche, chama hicho kinadai mifumo ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imeunganishwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa manufaa ya CCM.

Lakini historia yenye inaonesha kwamba barua na lundo la Malalamiko inaonesha wazi kwamba hayabadilisha chochote.

Tanzania ni taifa huru lenye katiba na mamlaka ya kujiamulia mambo yake. Jumuiya za kimataifa, hata zenye ushawishi mkubwa kama UN, haziwezi kufanya kazi ndani ya nchi bila ridhaa ya serikali husika. Hii ni kanuni ya msingi ya kidiplomasia uhuru wa mataifa (sovereignty),na Tanzania imekuwa mstari wa mbele kuilinda.

Historia ya Malalamiko ya CHADEMA nje ya nchi

CHADEMA imekuwa na rekodi ndefu ya kutumia njia ya barua na malalamiko kwa mashirika ya kimataifa. Mifano kadhaa inathibitisha namna juhudi hizo zimekuwa zikikosa matokeo tarajiwa.

Sheria za Uchaguzi: Mwaka 2019, CHADEMA iliandika barua Umoja wa Mataifa kupinga marekebisho ya Sheria ya Uchaguzi, wakidai yalilenga kubana upinzani. Hata hivyo, hakuna hatua iliyochukuliwa, na mabadiliko hayo yalitekelezwa kwa mujibu wa bunge na mamlaka ya kitaifa.

Kuhamishwa kwa wamasai Ngorongoro: KKatika hatua na mkakati wa serikali kulinda hifadhi ya Ngorongor, CHADEMA na mashirika ya kimataifa na washirika wengine walipeleka malalamiko UN wakipinga mpango wa serikali kuhamisha baadhi ya wamasai hao kutoka kwenye hifadhi. Licha ya mijadala mikali, serikali iliendelea na mpango wake, na chadema haikuambia kitu.

Mikopo ya nje: CHADEMA pia iliwahi kuandika barua kwa taasisi za kifedha za kimataifa kama IMF na Benki ya Dunia (WB) kuomba mikopo ya maendeleo isimamishwe. Lakini mwaka 2021 na 2022 pekee, Tanzania ilipokea zaidi ya USD 1.3 bilioni kutoka IMF kwa ajili ya kufufua uchumi baada ya janga la COVID-19. Hii ilionyesha kwamba taasisi za kifedha huangalia uhalali wa miradi na uwezo wa taifa kurejesha fedha, si shinikizo la vyama vya siasa.

FIFA na CAF dhidi ya Yanga: Hivi karibuni, baada ya klabu ya Yanga kuchangia shilingi milioni 100 kwenye harambe ya CCM ya kuchangia za uchaguzi wa mwaka huu, CHADEMA walilalamika FIFA na CAF wakidai ni ukiukwaji wa misingi ya michezo kwa klabu kushiriki siasa. Lakini FIFA haikuchukua hatua yoyote, kwa sababu haina mamlaka kuingilia masuala ya kisiasa ya ndani pasipo ushahidi wa uvunjifu wa kanuni zake.

Kwanini nasema ni sawa kupaka rangi upepo?

Sababu kuu za Chadema kuangukia pua mara kwa mara ukweli kwamba hakuna taasisi ya kimataifa itakayohatarisha uhusiano wake na Tanzania kwa ajili ya malalamiko ya chama kimoja cha siasa.

Tanzania ni nchi yenye uchumi unaokua kwa wastani wa zaidi ya 5% kwa mwaka, na ni kitovu cha biashara katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Diplomasia ya Tanzania inajengwa juu ya misingi ya kutoshirikiana na mashirika yanayoweza kuhatarisha uthabiti wake wa ndani. Ndiyo maana, mara zote, barua za CHADEMA zimeishia kuwa maandiko yasiyo na impact yeyote. Kwa wa kihistoria na takwimu, barua ya CHADEMA kwa UN, US, EU, AU na EAC hazitazaa matunda yoyote, wanafanya kazi ya bure isiyo na matokeo kama vile kupaka rangi upepo.
CHADEMA wanatakiwa kukisambaza chama chao mpaka ngazi za kata na shina huko chini kabisa. Wajenge mtandao mzuri na wawe sehemu ya maisha ya kila siku ya mwanakijiji wa kawaida.

Kila siku watakuwa wanakuja na mbinu za miezi ya kuelekea uchaguzi mkuu bila ya kujua tatizo lao la msingi linalowakwamisha ni lipi. Wataishia kufanya siasa za majukwaani wakifurahishwa na makundi ya watu wanaowasikiliza huku wakikosa kuaminiwa.

Lissu, Heche na wengine wa humu jukwaani waanze kutumia mbinu ya kisasa ya kumfikia mwananchi wa kawaida.

Hizi huruma wanazotafuta kwa taasisi za kimataifa haziwezi kuwasaidia lolote, kwanza wabadilishe mwelekeo wa siasa zao.
 
Back
Top Bottom