Maalim Seif: Tunataka Zanzibar yetu!

Maalim Seif: Tunataka Zanzibar yetu!

Namkumbuka seif sharif vizur sana na ninakaa nae jirani kabisa pale wete,nimewahii kumskililiza tangu Anaansha bismillah, walikua as a group wengine sasa ni marehemu,seif Huyu Huyu anachokikimbilia zaidi ni madaraka. Na sio manufaa ya waznz.
 
Kwenda kule muongo seif hajawahi kukaa wete kwao mtambwe kasoma huko kenda boarding form one kaRudi kusomesha fidel castro school hajawahi kukaa wete
Wete pale yupo kaka yake
Jambo alilo nalo Seif ni kutaka kukata minyororo ya kanisa kwa waislam Wa znz
Na wale wote wanaOpinga ni mawakala kanisa

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Kwenda kule muongo seif hajawahi kukaa wete kwao mtambwe kasoma huko kenda boarding form one kaRudi kusomesha fidel castro school hajawahi kukaa wete
Wete pale yupo kaka yake
Jambo alilo nalo Seif ni kutaka kukata minyororo ya kanisa kwa waislam Wa znz
Na wale wote wanaOpinga ni mawakala kanisa

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums

Kwa iyo ndo maana mnachoma makanisa??
Hapo ndo mnapokosea kwa kutomjua adui yenu,
mimi ni mkristo na nina unga mkono harakati zenu za kuvunja muungano huu. Ila nasikitika sana kuona kumbe hamumjui adui yenu.
Mtapata shida sana kupambana na adui msiyemjua tena mmemkumbatia wenyewe.
A wise man knows his enemy.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Kati ya Same ORG na Daudi mchambuzi muongo nani? Maana Mchambuzi anavyomuelezea na kumtetea Seif utadhani ni pacha wake!
 
Mtu wa Pwani,

..sasa huu undugu utabaki vipi wakati kuna washabiki wa UAMSHO wanatamka waziwazi kwamba Watanganyika wanapeleka UKIMWI, madawa ya kulevya, ujambazi, popobawa, umalaya, ushoga, na mambo mengi mabaya??

..tena wanasema hivyo mchana kweupe, na wale Mashekhe viongozi hawafanyi juhudi zozote zile kuwaweka sawa.

..tatizo siyo Zanzibar kudai kutoka ktk muungano, tatizo ni CHUKI inayopandikizwa dhidi ya Watanganyika. Hivi ni lazima kujenga CHUKI ili kuweza kuvunja muungano kati ya Tanganyika na Zanzibar??

NB:

..hata huku Tanganyika, kabla ya muungano, na wakati tunakua, kulikuwa hakuna ukimwi,udokozi,ujambazi, madawa ya kulevya, etc etc.

..je, unadhani ni sahihi kwa wa-Tanganyika kudai kwamba mambo yote hayo mabaya yamesababishwa na muungano, na tumeletewa na wa-Zanzibari??

joka kuu, hayo maneno tu hata kwenye kanga yamo.

wako wa tanga wanawachukia wazenji sana kupita kiasi. hata humu soma utaona machukizo yao. lkn udugu wetu haufutwi na wachache wenye chuki walio huku au kule.

ss ni ndugu kabla ya muungano na baada ya muungano, wandugu wa damu. hata kaka, mama au baba hutukanana wakikoseana ila haifuti udugu wao joka kuu la kibisa
 
Namkumbuka seif sharif vizur sana na ninakaa nae jirani kabisa pale wete,nimewahii kumskililiza tangu Anaansha bismillah, walikua as a group wengine sasa ni marehemu,seif Huyu Huyu anachokikimbilia zaidi ni madaraka. Na sio manufaa ya waznz.

Same ORG.

Ukiwa Znz kuna Seif Sharif wengi sana na pasi na shaka ndio uliokuwa unakaa nao huko wete. Lakin kama unamzungumzia Maalim Seif Shariif Hamad umepotea sana njia kwa lugha ya sasa naweza sema umepelekwa choo cha kike.

Kama utapitia historia yake vizuri hajawahi kabisa kukaa Wete iwe kimasomo au hata kikazi labda kupita njia tu. Pitia CV yake utaligundua hilo.


Pole sana

 
Bendera gani? Hii ambayo mwisho wake ni Chumbe? Haaaaaaaaaaaaaaaaaaaa...... lol nimeipenda hii.
Hivi huko chumbe ni wapi?
 
namkumbuka seif sharif vizur sana na ninakaa nae jirani kabisa pale wete,nimewahii kumskililiza tangu anaansha bismillah, walikua as a group wengine sasa ni marehemu,seif huyu huyu anachokikimbilia zaidi ni madaraka. Na sio manufaa ya waznz.

wacha kudanganya hapo wete ukikaa wapi ??? Mtambwe???
 
Kwa iyo ndo maana mnachoma makanisa??
Hapo ndo mnapokosea kwa kutomjua adui yenu,
mimi ni mkristo na nina unga mkono harakati zenu za kuvunja muungano huu.
Kwa uzoefu tu. TISS na polisi inapokosa "habari za kiintelijensia" na wanapokosa mtu wa kum-bambikia kesi, ujue ni kati yao na CCM ndio wanaofanya zengwe hilo ili kuzima madai ya kikundi husika, au chama husika.

Vyombo vyetu vya usalama unavielewa vyema? Kazi yake ni kulinda mali na raia na CCM, au vipi?

Umejiuliza kwa nini hakamatwi mhusika yeyeto katika matukio hayo?

Siku baada ya tukio CCM na polisi wanakimbilia kwenye vyombo vya habari kutupia lawama vikundi, vyama vinavyowachachafya na kuwakosesha usingizi.na kutaka jumuiya, vyama na "vikundi vya wahuni" wanavyovibebesha lawana vifutiwe usajili.
 
Maalim Seif Sharif Hamad ahutubia mkutano mkubwa wa hadhara kisiwani Pemba hii leo na anasema:

"Mimi sitafuni maneno kwamba ni muumini wa Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mashirikiano kati yake na Tanganyika kupitia Muungano wa Mkataba.

Namshangaa leo anakuja kiongozi wa Zanzibar anasema tuna bendera na muhuri na wimbo wa taifa, hayo yanatosha. Hivi huyu anajua anachokisema au anatumikia maslahi ya waliomtuma? Una bendera gani hii ambayo mwisho wake Chumbe? Mimi nataka niione bendera ya Dola ya Zanzibar inapepea Umoja wa Mataifa, New York pale. Nataka tuwe na Paspoti ya Zanzibar, nikisafiri nitoe Paspoti ya nchi yangu. Nataka tuwe na Ofisi za Kibalozi za Zanzibar katika nchi za nje. Leo hata mamlaka ya kiuchumi hatuna.

Tumeamua rasilimali yetu ya mafuta na gesi asilia yasiwe mambo ya Muungano, mpaka leo Tanganyika wamekwamisha, wanatuzuia tusinufaike na rasilimali zetu tukajenga uchumi wetu. Wanasema tuna viwango na mfumo mmoja wa kodi lakini bidhaa zikitoka Zanzibar wanazitoza ushuru tena. Lengo ni kuua uchumi wetu ili hatimaye tudhoofike na tusalimu amri kwao. Yaguju! Wasahau hilo.

Leo hata katika mikutano ya kimataifa, viongozi wetu wa Zanzibar hawapewi heshima ya uwakilishi wa nchi yetu. Inafika mahala hata Naibu Waziri tu wa Bara anaongoza ujumbe wa Tanzania wakati kuna Waziri kamili kutoka Zanzibar lakini haheshimiwi. Tutarejesha mamlaka yetu kamili.

Tuwe na Benki Kuu, tuwe na sarafu yetu ya Zanzibar, tupange uchumi wetu kwa maslahi ya watu wetu. Tunataka tuwe na uanachama katika jumuiya na mashirika yote ya kimataifa. Tuwe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zanzibar. Tuwe na uwezo wa kuingia mikataba na nchi za kigeni.

Hayo ndiyo tunayoyataka. Tukisema hivi hatuna maana tunataka ugomvi na Tanganyika. Hapana! Tunataka tuwe majirani wema na Tanganyika kama tutakavyokuwa na ujirani mwema na Kenya. Hayo yatafikiwa kupitia Muungano wa Mkataba wa Madola mawili huru kamili."


Kama utasoma kwa Umakini Speech hii utaona Dhulma wanayofanyiwa wazanzibar na CCM
NA CUF KIWE CHAMA DOLA ZNZ ndiyo ndiyo mnanfahamu!! huyo ni maalim bana!! Wape ZNZ yao jamani!!
 
joka kuu, hayo maneno tu hata kwenye kanga yamo.

wako wa tanga wanawachukia wazenji sana kupita kiasi. hata humu soma utaona machukizo yao. lkn udugu wetu haufutwi na wachache wenye chuki walio huku au kule.

ss ni ndugu kabla ya muungano na baada ya muungano, wandugu wa damu. hata kaka, mama au baba hutukanana wakikoseana ila haifuti udugu wao joka kuu la kibisa
Mtu wa Pwani,

..I hope what u r saying is true.


..Lakini ukishatamka kwamba wa-Tanganyika wanawaambukiza wa-Zanzibar ukimwi, ushoga, uzinzi, wizi, ujambazi, nadhani suala la udugu linapotea hapo.

..Kinachotia uoga ni kwamba maneno makali yenye CHUKI yanatamkwa waziwazi mbele ya viongozi wa kidini ambao hawachukui tahadhari kuwarekebisha mashabiki wao.

..Zaidi wana UAMSHO wanataka mkataba gani na Watanganyika ikiwa tayari wanaeneza chuki dhidi yetu??
 
Last edited by a moderator:
......kwa kweli wazanzibari kwa sasa wanadai nchi yao ....
....Kule ni kimoja tu watu wanataka nchi yao tena yenye mamlaka kamili...

i

Mkuu, Kwanza nakugongea "LIKE". Naungana na wewe katika harakati za Kuikomboa Tanganyika, na wakati huohuo, kuendeleza udugu wetu, nje ya Muungano.

Mimi ni mwanachama mwanzilishi, na nitaendelea kuwa Mwanachama damu wa chama changu, hadi hapo Mungu atakapo ichukua roho yangu. Isipokuwa, Tofauti niliyonayo na wenzangu ndani ya chama changu, ni jinsi tunavyoikalia nchi nyingine kimabavu, bila ridhaa yao.

Naunga mkono wazo la kimapinduzi mlilonalo la kudai nchi yenu, ila naomba mpunguze mbinu za kudai nchi kwa kuchoma makanisa, pamoja na mbinu chafu kama hizo. Njoni kwenye meza ya mazungumzo, Mdai nchi kupitia maoni ya Katiba mpya, pamoja na mbinu halali.
Mungu awabariki.
 
Mtu wa Pwani,

..I hope what u r saying is true.


..Lakini ukishatamka kwamba wa-Tanganyika wanawaambukiza wa-Zanzibar ukimwi, ushoga, uzinzi, wizi, ujambazi, nadhani suala la udugu linapotea hapo.

..Kinachotia uoga ni kwamba maneno makali yenye CHUKI yanatamkwa waziwazi mbele ya viongozi wa kidini ambao hawachukui tahadhari kuwarekebisha mashabiki wao.

..Zaidi wana UAMSHO wanataka mkataba gani na Watanganyika ikiwa tayari wanaeneza chuki dhidi yetu??

ww msomi usishtuke hata siku moja, nnarejea hayo ni mambo ya familia, ss ni familia moja kwa vile mmoja anaona anaonewa kwa kutaka kujinasua atasema lolote lile ili yule mwengine audhike ili atoe kile anachodaiwa ni la kawaida hilo. wala si la kuumiza kichwa sana kwa mtu msomi.

jengine wazenji pia huku kuna wanaowaita ma alqaida, alshabaab na wao wanatumia dini kuwadharau na kuwatukana wazenji. ila kwa wenye kuelewa wanajua hayo yote ni mapambio tu. mziki muungano hauko poa. hili dubwana tulin'goe utaona tunakaa tunaresolve haya madogo madogo.

ukitaka kujua kua haya si mambo ya kushtua angalia jinsi ambapo wazanzibari wanavyoendelea na mambo yao tanganyika na wakitaniana na ndugu zao bukheri wa hamsa hamsini. na kule wako watanganyika wengi tu wanaendelea na shughuli zao bukheri wa shuwari. hata ww kama unataka kwenda vacation mkuu karibu sana, na unajua kua wabongo wengi huenda kupunga upepo kule na unatembea bila shida wakikujua hukutania tu twataka nchi yetu.
 
“Mimi sitafuni maneno kwamba ni muumini wa Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mashirikiano kati yake na Tanganyika kupitia Muungano wa Mkataba. Namshangaa leo anakuja kiongozi wa Zanzibar anasema tuna bendera na muhuri na wimbo wa taifa, hayo yanatosha. Hivi huyu anajua anachokisema au anatumikia maslahi ya waliomtuma? Una bendera gani hii ambayo mwisho wake Chumbe? Mimi nataka niione bendera ya Dola ya Zanzibar inapepea Umoja wa Mataifa, New York pale. Nataka tuwe na Paspoti ya Zanzibar, nikisafiri nitoe Paspoti ya nchi yangu. Nataka tuwe na Ofisi za Kibalozi za Zanzibar katika nchi za nje.


Leo hata mamlaka ya kiuchumi hatuna. Tumeamua rasilimali yetu ya mafuta na gesi asilia yasiwe mambo ya Muungano, mpaka leo Tanganyika wamekwamisha, wanatuzuia tusinufaike na rasilimali zetu tukajenga uchumi wetu. Wanasema tuna viwango na mfumo mmoja wa kodi lakini bidhaa zikitoka Zanzibar wanazitoza ushuru tena. Lengo ni kuua uchumi wetu ili hatimaye tudhoofike na tusalimu amri kwao. Yaguju! Wasahau hilo. Leo hata katika mikutano ya kimataifa, viongozi wetu wa Zanzibar hawapewi heshima ya uwakilishi wa nchi yetu.


Inafika mahala hata Naibu Waziri tu wa Bara anaongoza ujumbe wa Tanzania wakati kuna Waziri kamili kutoka Zanzibar lakini haheshimiwi. Tutarejesha mamlaka yetu kamili. Tuwe na Benki Kuu, tuwe na sarafu yetu ya Zanzibar, tupange uchumi wetu kwa maslahi ya watu wetu. Tunataka tuwe na uanachama katika jumuiya na mashirika yote ya kimataifa. Tuwe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zanzibar. Tuwe na uwezo wa kuingia mikataba na nchi za kigeni. Hayo ndiyo tunayoyataka. Tukisema hivi hatuna maana tunataka ugomvi na Tanganyika. Hapana! Tunataka tuwe majirani wema na Tanganyika kama tutakavyokuwa na ujirani mwema na Kenya. Hayo yatafikiwa kupitia Muungano wa Mkataba wa Madola mawili huru kamili.”

Seif asema Tunataka Zanzibar yetu | Mzalendo.net
 
Back
Top Bottom