Kama kuna chama ambacho msajili anapaswa kukifuta haraka basi ni CUF. Haiwezekani mtendaji mkuu wa chama anahubiri waziwazi tena bila kificho utengano wa kitaifa halafu anatazamwa tu!
Tanzania ni moja na mipaka yake lazima ilindwe kwa gharama zote. Hoja zake alipaswa azitolee kama mwananchi wa kawaida kwenye Tume ya Katiba na sio majukwaani. Tendwa upo?
Kwa staili hii hata maadui watakuheshimu Maalim Seif .Maalim Seif Sharif Hamad ahutubia mkutano mkubwa wa hadhara kisiwani Pemba hii leo na anasema:
"Mimi sitafuni maneno kwamba ni muumini wa Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mashirikiano kati yake na Tanganyika kupitia Muungano wa Mkataba.
Namshangaa leo anakuja kiongozi wa Zanzibar anasema tuna bendera na muhuri na wimbo wa taifa, hayo yanatosha. Hivi huyu anajua anachokisema au anatumikia maslahi ya waliomtuma? Una bendera gani hii ambayo mwisho wake Chumbe? Mimi nataka niione bendera ya Dola ya Zanzibar inapepea Umoja wa Mataifa, New York pale. Nataka tuwe na Paspoti ya Zanzibar, nikisafiri nitoe Paspoti ya nchi yangu. Nataka tuwe na Ofisi za Kibalozi za Zanzibar katika nchi za nje. Leo hata mamlaka ya kiuchumi hatuna.
Tumeamua rasilimali yetu ya mafuta na gesi asilia yasiwe mambo ya Muungano, mpaka leo Tanganyika wamekwamisha, wanatuzuia tusinufaike na rasilimali zetu tukajenga uchumi wetu. Wanasema tuna viwango na mfumo mmoja wa kodi lakini bidhaa zikitoka Zanzibar wanazitoza ushuru tena. Lengo ni kuua uchumi wetu ili hatimaye tudhoofike na tusalimu amri kwao. Yaguju! Wasahau
hilo.
Leo hata katika mikutano ya kimataifa, viongozi wetu wa Zanzibar hawapewi heshima ya uwakilishi wa nchi yetu. Inafika mahala hata Naibu Waziri tu wa Bara anaongoza ujumbe wa Tanzania wakati kuna Waziri kamili kutoka Zanzibar lakini haheshimiwi. Tutarejesha mamlaka yetu kamili.
Tuwe na Benki Kuu, tuwe na sarafu yetu ya Zanzibar, tupange uchumi wetu kwa Kw
maslahi ya watu wetu. Tunataka tuwe na uanachama katika jumuiya na mashirika yote ya kimataifa. Tuwe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zanzibar. Tuwe na uwezo wa kuingia mikataba na nchi za kigeni.
Hayo ndiyo tunayoyataka. Tukisema hivi hatuna maana tunataka ugomvi na Tanganyika. Hapana! Tunataka tuwe majirani wema na Tanganyika kama tutakavyokuwa na ujirani mwema na Kenya. Hayo yatafikiwa kupitia Muungano wa Mkataba wa Madola mawili huru kamili."
Kama utasoma kwa Umakini Speech hii utaona Dhulma wanayofanyiwa wazanzibar na CCM
Lakini mkuu yeye ndo aliuchelewesha muungano wa kweli kwa kumsaliti mzee jumbe.Mkuu ubarikiwe sana kwa kuiweka vidio hii nimeisikiliza kwa makini maalim seif anatisha mi nilijua yupo ktk serikali haongei kumbe anamwaga vitu balaa kweli maalim anatafuta ukombozi wa wazanzibar uwe unatuwekea vidio zake mana ktk tv hawatoi
huvi kuna nini kilichojificha katika muungano huu ambacho hakitakiwi kijuilikane mpaka inafikia mtu akiamua kuuzungumzia anatiwa hatiani na kuonekana kama anatenda dhambi?! Inawezekana ile dhana ya sheikh ilunga hassan ya kwamba zanzibar inatawaliwa na watanganyika kwa 'mfumo kristo' kupitia mgongo wa muungano hapa ndio inajidhihirisha! Na ndio maana wazanzibari hatuipendi chadema, na itakua ni ndoto chama hichi kua cha kitaifa mpaka tutakapojitenga na watanganyika.
Namshangaa analalamika wakati yeye ni sehemu ya serikali ya zanzibar na ndio wenye maamuzi na zanzibar yao.
Hapana HANA MAMLAKA YOYOTE, mwenye mamlaka ni Makamu wa pili wa Rais! Yeye ni kama picha tu au danganya toto ya UMOJA WA KITAIFA.
Sijui nitapigwa "ban" kwa comment hii...
Those days has long gone!Yuko wapi Mkapa akarejeshe yale alilofanya miaka ya 2000/1
Those days has long gone!
Muislamu wa mwaka 2000/1 si wa mwaka 2014.
Tunamsubiri rais kama Mkapa (Lowasa?) aje awashe utambi...
Aache ujinga yeye si ndio aliwasaliti wenzake walipotaka kuvunja muungano kwa kuandika barua UN badala yake akamwambia Nyerere deal likafaMaalim Seif Sharif Hamad ahutubia mkutano mkubwa wa hadhara kisiwani Pemba hii leo na anasema:
"Mimi sitafuni maneno kwamba ni muumini wa Zanzibar yenye mamlaka kamili kitaifa na kimataifa itakayofuatiwa na mashirikiano kati yake na Tanganyika kupitia Muungano wa Mkataba.
Namshangaa leo anakuja kiongozi wa Zanzibar anasema tuna bendera na muhuri na wimbo wa taifa, hayo yanatosha. Hivi huyu anajua anachokisema au anatumikia maslahi ya waliomtuma? Una bendera gani hii ambayo mwisho wake Chumbe? Mimi nataka niione bendera ya Dola ya Zanzibar inapepea Umoja wa Mataifa, New York pale. Nataka tuwe na Paspoti ya Zanzibar, nikisafiri nitoe Paspoti ya nchi yangu. Nataka tuwe na Ofisi za Kibalozi za Zanzibar katika nchi za nje. Leo hata mamlaka ya kiuchumi hatuna.
Tumeamua rasilimali yetu ya mafuta na gesi asilia yasiwe mambo ya Muungano, mpaka leo Tanganyika wamekwamisha, wanatuzuia tusinufaike na rasilimali zetu tukajenga uchumi wetu. Wanasema tuna viwango na mfumo mmoja wa kodi lakini bidhaa zikitoka Zanzibar wanazitoza ushuru tena. Lengo ni kuua uchumi wetu ili hatimaye tudhoofike na tusalimu amri kwao. Yaguju! Wasahau hilo.
Leo hata katika mikutano ya kimataifa, viongozi wetu wa Zanzibar hawapewi heshima ya uwakilishi wa nchi yetu. Inafika mahala hata Naibu Waziri tu wa Bara anaongoza ujumbe wa Tanzania wakati kuna Waziri kamili kutoka Zanzibar lakini haheshimiwi. Tutarejesha mamlaka yetu kamili.
Tuwe na Benki Kuu, tuwe na sarafu yetu ya Zanzibar, tupange uchumi wetu kwa maslahi ya watu wetu. Tunataka tuwe na uanachama katika jumuiya na mashirika yote ya kimataifa. Tuwe na Waziri wa Mambo ya Nje wa Zanzibar. Tuwe na uwezo wa kuingia mikataba na nchi za kigeni.
Hayo ndiyo tunayoyataka. Tukisema hivi hatuna maana tunataka ugomvi na Tanganyika. Hapana! Tunataka tuwe majirani wema na Tanganyika kama tutakavyokuwa na ujirani mwema na Kenya. Hayo yatafikiwa kupitia Muungano wa Mkataba wa Madola mawili huru kamili."
Kama utasoma kwa Umakini Speech hii utaona Dhulma wanayofanyiwa wazanzibar na CCM
kaka hayo ni mawazo binafsi ya maalim seifu,sasa chama cha cuf kifutwe kwasababu kinaukataa mungano,kwanini kisifutwe chama cha ccm kwa kung'ang'ania mungano usio na mwelekeo kwa pande zote mbili,je na chadema nacho kifutwe kwa kuwa na sera ya serikali tatu
waswahili wanasema wenye nguvu wape hapa utaona kisiasa ccm wako peke yao kwa huu msimamo wao wa mungano,kwa mantiki hiyo ccm cdio chama kinachotakiwa kifutwe