Maalim Seif: Tunataka Zanzibar yetu!

Maalim Seif: Tunataka Zanzibar yetu!

Wakuu, as Days goes on mie nimekuwa nawashangaa sana wenzetu, Waliberali wa CUF.
Leo Maalim Seif alikuwa Zanzibar kwenye Harakati za Kudai Zanzibar Huru.
Zanzibar yenye Mamlaka Yote, hii ikifanikiwa inamaana kuwa Hakuna Mungano.
Cha ajabu Huyu huyu Mzee, Maalim Seif pamoja na wa Liberali wenzake wa CUF, wanasema Lipumba ndo Rais 2015????????
Haya wameyasemea Morogoro, Tanganyika.
Natatizika hapa, Hawa Jamaa CUF wanataka kutawala Tanganyika na Zanzibara???????
Kuna Sabababu gani ya the Same Maaliim Seif Kudai Mamlaka kamili ya Zanzibar and at the same time Kuja Tanganyika.
Kudai Uuungwaji Mkono na Wa Tanganyika.
Maalim Seif anadai Mamlaka Kamili ya Zanzibar kwa Kofia ya CUF.
Maalim Seif huyu huyu anakuja Tanganyika tena kuomba Wa Tanganyika waunge Mkono CUF????
Jamani Mbona Wa Liberali CUF wamechanganyikiwa hivyo, Mbona Mwana Ndoa mwenzao CCM hafanyi hayo??????
Hivi Wakuu, Liberal Lipumba kwani ni Mzanzibar????


Hebu tujadilini jamani, hawa Wa Liberali wa CUF ni nini hasa wanataka
[h=2]Ukweli Kuhusu Mabadiliko ya Sera Ndani ya CUF na Ushoga!!!!!!!!!!![/h]
Nakumbuka Mwaka 2009 April Chama Cha CUF Kiliitisha mkutano mkuu wa mabadiliko ya Katiba na Sera. Mkutano huo ambao ulikuwa na agenda za uchaguzi Mkuu ambapo Prof Lipumba kupitia idara ya Blue Gad alimufanyia Umafia Prof Safari ili asipate nafasi ya Mwenyekiti Taifa kwa Kumuundia zengwe na kumuwinda kama mhalifu.

Kufuatia kampeni hizo Chafu Prof Safari alimuhoji Lipumba kuhusu mkewe kuwa mbano hatumuoni kwenye chama??
Lipumba akasema mke wake anafanya kazi UN ambapo hawatakiwi kujihusisha na Mambo ya Siasa.
Pili Sfari alihoji ni kwa nini CUF viongozi wake wengi katika nafasi za Juu ni waislamu hata katika majimbo yenye Wakristo wengi??. Pia alihoji ni kwa nini CUF haina hata moja???. Pia alihoji kwa nini CUF ibakie ZNZ pekee wakati wapo waasisi bara???

Kura zilipigwa Safari akaambulia kura sita (6).

Kwenye Uchaguzi huo Julias Mtatiro aliletwa na Seif kama Mwangalizi wa Uchaguzi na kusimamia uchaguzi huo wakati si Mwanachama . Na baadaye ikaja kuonekana walikuwa na Lengo la kumuanda Mkristo kuchukua nafasi ya Naibu katibu mkuu bara baada ya kutengeneza njama za kumutimua Wilfred Lwakatare.

Kabla ya mabadiliko ya sera CUF ilikuwa ina amini katika Utajirisho na Mwaasisi wa sera hii ni marehemu Shabani Khamis Mloo .
Muasisi wa sera ya uliberali ni Maalim Seif na alimtumia Imail Jussa mtu wa karibu na Julius Mtatiro kuleta mabadiliko ya katiba .
Watu ambao walikuwa wanapinga sera hiyo ni pamoja na prof Safari , Marehemu Shabani Mloo,Mhe Masoud na idara ya Blue Gad .
Kwenye mjadala wa kupitisha katiba hiyo Seif na Lipumba walikuwa kitu kimoja huku Hamadi Rashid akiwazunguka.
Marehemu Mloo alipinga hadi akatoa machozi na baada ya tukio hilo Masoud ambaye alikuwa mkurungenzi wa blue gad Taifa naye aliumia sana kwa hakutaka Ulibelali na kufanya mkakati wa kupinga kwa nguvu zote.

Aliwapanga vijana wa blue gadi wakiongozwa na desk officer Mzee Wandwi. Kazi hiyo ilipo anza , Maalimu seif alipata taarifa na kumutuma Jussa kumushughurikia Wandwi.
Jussa alikwenda kumutukana Mzee Wandwi kwa kumwita Mbwaa!!!

Baada ya Mzee Wandi kutukana Mbwaa alikasirika sana ndipo Mzee Saidi Miraji ambaye akaingilia kati na kuweka msimamo kuwa ulibelali haufahamiki vizuri hivyo sio vema kuiga mambo ya kigeni kwa kuwa yanaweza kupotosha taswira ya chama.

Prof Lipumba alimpinga Mzee Saidi Miraji na mpasukoa ukawa mkubwa. Mpasuko huu ni sehemu ya chanzo cha baadhi ya watu kuunda chama kingine cha ADC.


NB:
Mimi nimeshangaa sana Mhe Masoudi kumushambulia Wenje wakati hata yeye alipinga sera hiyo ndani ya CUF . Mimi nawashauli CUF waitishe Mkutano mkuu Taifa na kujadili suala hilo tena
CUF inaburuzwa na Maalimu Seif na ni chama cha Wapemba na sakata la Ushoga lina mkono wa Seif. Nawaomba CUF kama wana ujasiri wapinge maneno haya. pia namtaka mtatiro aje humu atoe mchango wake hapa!!!
Nawaomba waandishi nenda kawahoji niliowataja ili ukweli ujulikana ndani ya CUF sera ya Ushaga ipo lakini hawakujua!!




SEHEMU YA TAARIFA YA WENJE


3.0. VYAMA VYA SIASA NA MISAADA KUTOKA NJE YA NCHI.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na Umoja wa Mataifa ‘United Nations University'(UNU-WIDER) ya mwezi Aprili 2012 iliyoandaliwa na Aili Mari Tripp ilionyesha kuwa misaada ya wahisani kutoka nje katika mabadiliko ya kisiasa Tanzania ‘Donor Assistance and Political Reform in Tanzania', inaonyesha kuwa Tanzania imepokea misaada kutoka nje yenye thamani ya dola za kimarekani bilioni 26.85 toka mwaka 1990-2010.

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa ripoti hiyo ni kuwa Tanzania ni nchi inayoongoza kusini mwa jangwa la Sahara kwa kupokea misaada mingi kutoka nje ya nchi na hasa kutoka mataifa ya Ulaya na taasisi za nchi za Uingereza, Marekani, Ujerumani, Uholanzi, Norway, Canada, Sweden, na taasisi kama Benki ya Dunia, IMF ,UNDP ,UNICEF na mengineyo.

Pamoja na misaada yote hiyo, bado tumeendelea kuwa nchi maskini sana duniani pamoja na kuwa na rasilimali lukuki ambazo tumepewa na Mungu ila tunashindwa kuzitumia kwa manufaa ya watanzania na badala yake tumeendelea kudanganywa na vimisaada vidogo vidogo na kubadilishana na rasilimali zetu kama madini, misitu ,wanyama nk kwa ajili ya misaada hiyo.

Mheshimiwa Spika, pamoja na misaada hiyo kwa serikali hii ya CCM bado vyama vya siasa vimekuwa na mahusiano na baadhi ya vyama vingine vya siasa katika mataifa ya magharibi na vimekuwa vikipokea misaada ya aina mbalimbali kama fedha , nyenzo na mengineyo kadiri ya makubaliano na mirengo ya kiitikadi ya vyama husika.Pamoja na ukweli huo bado vipo vyama vya siasa vinavyopotosha umma kuhusiana na misaada vinayopokea kutoka nje ya nchi na vyama hivi vimekuwa mstari wa mbele kueneza propaganda za uongo kuwa vyenyewe havipokei misaada kutoka nchi za magharibi.

Mheshimiwa Spika, CCM wao ‘wanajiita' kuwa wapo mrengo wa kijamaa/kikomunisti na wamekuwa wakipokea misaada mingi sana ya fedha na nyenzo kutoka Umoja wa Vyama vya Kikomunisti Ulimwenguni ‘Socialist International' kutoka katika nchi kama za Ujerumani kupitia SDP ,Uingereza kupitia chama cha Labour,China kupitia chama cha Kikomunist ,Marekani kupitia chama cha Democrats. Pamoja na misaada ya kifedha na kiufundi ambayo CCM imekuwa ikipata kutoka nje wamekuwa hawatangazi hadharani hata mara moja kuhusiana na kiasi ambacho wamekuwa wakipokea na hivyo kila kitu kwao imekuwa ni siri kuu ya viongozi wao.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa chama cha CUF, kutokana na itikadi zake za mrengo wa Kiliberali ambazo miongoni mwa misingi yake mikuu ni pamoja na "kupigania haki za ndoa ya jinsia moja, usagaji na ushoga". Hii ni kwa mujibu wa tangazo lao kwenye mtandao wao wa umoja wa maliberali ulimwenguni, likiungwa mkono na Waziri wa Haki na Usawa wa Uingereza, Lynn Featherstone kutoka chama cha Liberal Democrats wakati chama hicho(www.liberal-international.org) kilipokuwa kinapitisha azimio la kuruhusu ndoa za jinsia moja kama haki ya mtu mmoja mmoja, wanashirikiana na vyama kama vile LPC ya Canada, Det Radikale Venstre cha Norway, FDP cha Ujerumani, Israel Liberal Group cha Israel,PDS cha Senegal na Liberal Democrats cha Uingereza.

Kutokana na umoja huo, CUF wamekuwa wakipata msaada wa kifedha na nyenzo nyingine mbalimbali kutoka kwa vyama hivyo vya mrengo wa Kiliberali na msaada wa mwisho ni hivi majuzi mwezi Machi 2013 waliposaini makubaliano na chama cha Kiliberali kutoka Norway.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa CHADEMA, wapo kwenye Umoja wa Vyama vya Kidemokrasia Ulimwenguni (International Democratic Union - IDU). Huu ni umoja wa vyama ambavyo vipo kwenye mrengo wa kati na ambavyo msingi wake mkuu ni pamoja na kuwa na familia, kama taasisi muhimu katika jamii, ikimaanisha kwamba: "tunapinga vitendo vyote vya ushoga na usagaji". Tunatetea demokrasia, haki za binadamu na kupambana na ufisadi katika serikali. Vyama wanachama wa umoja huu ni pamoja na Conservative Party cha UK, CPP cha Norway, Republican cha Marekani na vingine vinavyofuata mrengo huo.

Mheshimiwa Spika, Kambi rasmi ya upinzani Bungeni, inavitaka vyama vyote ambavyo vimekuwa na mahusiano na vyama vya nje viweke wazi mikataba yao na malengo ya mahusiano hayo ikiwa ni pamoja na misaada ambayo vimekuwa vikipokea kutoka kwenye nchi hizo .​
 
Jana Kamati ya maridhiano huko Zanzibar imefanya mkutano mkubwa ulioelezea juu ya mambo yanayoashiria kuifanya Zanzibar iwe na mamlaka kamili na kuashiria kutaka kuiondoa ndani ya muungano. Je huu si uhaini? Je kuna haja ya CCM kuendelea na ndoa yao na CUF?
 
Jana Kamati ya maridhiano huko Zanzibar imefanya mkutano mkubwa ulioelezea juu ya mambo yanayoashiria kuifanya Zanzibar iwe na mamlaka kamili na kuashiria kutaka kuiondoa ndani ya muungano. Je huu si uhaini? Je kuna haja ya CCM kuendelea na ndoa yao na CUF?

Jamaa mjanja sana kaona Shein kaenda China yy kabai na nchi anafanya yake, namshauri faster tu asaini kujitoa kwenye Muungano ili Shein akirudi akute Zanzibar ni nchi wasituchoshe.
 
Chama cha mapinduzi Zanzibar wamedai maamuzi na ushawishi wa makamu wa pili Zanzibar kuwa ni muasi na mnafiki kwa mambo waliyokubaliana juu ya muungano na sasa anaibuka na kudai Zanzibar huru.
 
Zimetolewa kauli mbalimbali na hao viongozi wa kisiasa na washirika wakubwa wa CCM. Kauli ya Maalim kuhusu wazenji kuwa huru kwa kupata serikali na mamlaka kamili si nyepesi kihivyo. Lakini pia kauli ya mkuu wa CUF kuhusu wana Ntwara nayo ina uzito wake juu ya mustakabali mzima wa nchi yetu na pengine uhusiano wao na CCM. Pengine urafiki wa vyama hivi ndo unaelekea ukingoni. Yetu macho!
 
Maalim Seif wa CUF anapohubiri Zbz kujitenga anafanya uhaini! Dr Shein apunguze upole. Seif anapaswa kufukuzwa GNU na kukamatwa! Historia inaonesha huyu jamaa ni mkorofi daima.
 
Maalim Seif wa CUF anapohubiri Zbz kujitenga anafanya uhaini! Dr Shein apunguze upole. Seif anapaswa kufukuzwa GNU na kukamatwa! Historia inaonesha huyu jamaa ni mkorofi daima.

Hukumbuki kwamba aliwahi kuwekwa korkoroni na Komandoo kwa madai hayo hayo?

Hukumbuki kilichomnyofoa Uwaziri Kiongozi kule Dodoma?

Mkuu Waambi nakuambia maji hata uyachemshe vipi siku zote huwa hayasahau ubaridi.
 
Last edited by a moderator:
Draft tu hivi, je kura ya maoni? Si itakuwa balaa pale mchambawima!?
 
Ni wazi kwamba kumbe Muungano wa Serikali mbili uliwanufaisha zaidi CCM na Wazanzibari. Hii inadhihirika kutokana na msimamo wa CCM na Wazanzibari wengi kutaka kuendelea na Muungano wa kinyonyaji wa serikali mbili. Mimi napendekeza ili kuwa fair, ama kuwepo na Muunganowa serikali moja au MUUNGANO UVUNJWE, ili kila upande uangalie maisha yake, kuliko kuendelea kutawaliwa na kina mwigulu mtoa kucha. TUMEWACHOKA...!
 
Ni wazi kwamba kumbe Muungano wa Serikali mbili uliwanufaisha zaidi CCM na Wazanzibari. Hii inadhihirika kutokana na msimamo wa CCM na Wazanzibari wengi kutaka kuendelea na Muungano wa kinyonyaji wa serikali mbili. Mimi napendekeza ili kuwa fair, ama kuwepo na Muunganowa serikali moja au MUUNGANO UVUNJWE, ili kila upande uangalie maisha yake, kuliko kuendelea kutawaliwa na kina mwigulu mtoa kucha. TUMEWACHOKA...!

Mkuu Muungano huu hautavunjika kirahisi kama unavyodhani!
 
Ndoa ikiwa na kokoro nyingi ni bora ivunjike ili kuepusha balaa.

Mtu unaweza mwagiwa tindikali ukiwa umelala....
 
Serikali tatu ni porojo. muungano uvunjwe, kwani Zanzibar ni nchi huru. Kama kuna umuhimu wa kuwa karibu basi iwe shirikisho kama ilivyo Jumuiya ya Afrika mashariki. Mbona Uganda na Kenya hamkuzifanya serikali mbili. hii ni kwasababu ni Nchi kubwa na msingeweza kuziburuza. Acha Zanzibar iwe huru wajipangie mambo yao Kama Tanganyika inavyo takiwa kuwa huru. Na hii imeleta matatizo sana wakati wa sharehe ya uhuru Kujua NI uhuru wa Tanganyika au Tanzania
 
Back
Top Bottom