Zanzibar 2020 Maalim Seif Sharif Hamad unataka kutugawa Watanzania kwa faida ya nani?

Mathayo Fungo

JF-Expert Member
Nov 13, 2018
319
510
“Mimi sioni tabu kumwambia (Magufuli) tugawane mbao”. Haya ni maneno aliyoyatamka Mgombea wa Urais Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha ACT-Wazalendo, Maalim Seif Sharif Hamad akiwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika eneo la Mkele, Mjini Magharibi visiwani Zanzibar.

Kauli hiyo ameitoa sambamba na kauli zingine nyingi ambazo zinaonesha dhamira ya dhati ya Maalim Seif Sharif Hamad kuvunja Muungano endapo tu atachaguliwa kuwa Rais katika Visiwa hivyo.

Ameendelea kusema hata kama Rais Magufuli atachaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania basi atamwambia Rais Magufuli abaki na Tanganyika na yeye (Maalim Seif) Zanzibar. Hii ni kauli inayoashiria wazi kuwa Mgombea huyu hana nia njema na Muungano ambao umedumu na kuenziwa na Marais wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ile ya Mapinduzi Zanzibar, kwa takribani miaka 56 tangu uasisisiwe na Waasisi wake, Hayati Mzee Abeid Aman Karume na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mnamo Aprili 26, 1964.

Tunapenda kumkumbsha Maalim Seif na Chama cha ACT Wazalendo kuwa dhambi ya ubaguzi mnayotaka kuitekeleza haitawaacha salama watanzania kwani itaathiri maisha ya watanzania wa pande zote ambao kwa miaka yote wameishi na kufanya shughuli zao za kiuchumi na kijamii mahali popote bila kubaguliwa wala kubughudhiwa.

Uimara na utulivu wa Muungano huu ambao ni mkongwe zaidi barani Afrika, umekuwa wa kutolewa mfano na kuzifanya nchi nyingi kuunda umoja ikiwemo Jumuiya ya Ulaya, Jumuiya ya Afrika Mashari na Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), kuzitajakwa uchache.

Ni rai yetu kwa Wazanzibari na watanzania kwa ujumla, kuwakataa viongozi wa aina ya Maalim Seif ambae hata hajaingia madarakni anaanza kuonesha wazi wazi kuwagawa watanzania. Tuchague kiongozi kutoka Chama kitakachowaunganisha watanzania na kuwapa uhuru wa kufanya shughuli zao mahali popote bila kubaguliwa wala kubughudhiwa kwa ajili ya ustawi wa maisha yao.
 
Hitaji la siku nyingi la Wazanzibari waliokuwa wengi ni kulivua na hatimaye kuondokana na koti la muungano. Huu ndio ukweli wenyewe, ni sisi Watanganyika ndio ambao hasa tunauhitaji kwa udi na uvumba.
 
The conduct of the upcoming elections in Tanzania has important consequences not only for Tanzania, but for the entire East African region. Tanzania’s history of peaceful multi-party elections stretching back 25 years has made it a model on the continent.

The United States government reaffirms unequivocally that it does not support any specific candidate or party in Tanzania’s upcoming elections. The United States supports the democratic process itself. We support a genuinely free, fair, transparent, and peaceful electoral process, before, during, and after election day. This includes ensuring the safety of all contestants, respect for the rule of law, and the absolute impartiality of the authorities in charge of managing the elections.

The United States, along with other democratic nations, will be paying close attention to actions of individuals who interfere in the democratic process or instigate violence against the civilian population before, during, or after the elections. We will not hesitate to consider consequences for those found to be responsible for election-related violence or undermining the democratic process.

We welcome the calls by the leading candidates for a peaceful and transparent electoral process, and we urge them and their supporters to take measures to decrease tensions and avoid inciteful rhetoric.

By U.S. Embassy Dar es Salaam | 1 October, 2020 | Topics: Press Releases
 
And you have similar/same pattern: You have to write your full names to win favour:
tumeishi pamoja miaka 56 bila kuona faida.

ati kuna madhara makubwa ya kutengana ni yapi hayo. Let them go if they can manage themselves moreover they are a country With their own land, flag and people
 
Zanzibar kwa udogo wake,ni rahisi mno kupiga maendeleo zaidi ikiwa nje ya Muungano wakiwa kama taifa, wataweza kufanya maamuzi sahihi ya kukuza uchumi wao kilimo cha karafu na spices, utalii,uvuvi,uchimbaji wa mafuta na gesi baharini.

Lakini hata Bara itafaidika zaidi kwa kuwauzia bidhaa nyingi mno kutoka bara ikiwepo,umeme, vyakula,mifugo,vifaa vya ujenzi,nguvu kazi n.k kwa sasa muungano ni mzigo mkubwa kwa bara kutokea utawala,bunge.n.k.

Lakini zaidi ya nusu ya Wazanzibari wanaishi bara na wanavitega uchumi bara,na hilo linaweza kuwa kikwazo cha kuvunja Muungano,labda utabuniwa ushirikiano wa kindugu bila nchi hizo mbili kuingilia mambo ya nchi nyingine.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom