Ndio amekuwa mtoaji wa maamuzi ndani ya Cuf kwa kuingilia madaraka ya mwenyekiti hili ndilo lililomuondoa Prof Lipumba katika uenyekiti, ameua cuf bara kwa maslahi Zanzibar, ruzuku ya chama yote kwa 80% imepelekwa zanzibar.
Prof Lipumba alikuwa anataka kujua maslahi ya cuf ndani ya ukawa kuhusu ruzuku itokanayo na kura za urais. Lipumba ana Mengi moyoni hajayasema tuvute muda.
Hakuna asiefaham kwamba wewe binafsi na roho yako ulitaka siku1 Prof. Lipumba aseme hivyo ulivyo mtazamo wako ili onekane kwa maalim seif awe ni mtu wa hivyo ulivyomfikiria. hii ni interest yako tu na chuki zako tu dhidi ya maalim seif.
Lakini kuna mambo ya kuyazingatia kama ifuatavyo:-
1. Prof. Lipumba kwanini hakujiuzulu siku zote hizo lakini alikuja kujiuzulu siku1 tu baada ya UKAWA kumtangaza Lowassa kugombania Urais kwa ticket ya Ukawa?
2. Je pia unataka kuniambia Dr. Slaa naye pia ana elements kama ulizozifikiria wewe kwa Lipumba dhidi ya CUF na Maalim Seif? mana baada ya CHADEMA tu kumpokea Lowassa na kumtaka achukue form ya urasi kwa Ukawa ni siku ile ile tu wala haikuzidi Dr Slaa aliingia mitini, kabla ya hapo Dr Slaa akihudhuria vikao vya Ukawa usiku na mchana.
3. Lakini kama haitoshi lipumba alipojiuzulu kwanini aligusia kuhusu Lowassa kupiga kura ya NDIO kwenye katiba pendekezwa wakati Ukawa ilipiga hapana? pia kwa hoja unataka kutuaminisha kuna sababu nyengine ambazo wewe na Prof. Lipumba munazifikiria ili kuja hadharani siku1 mkitamani kumsema maalim Seif na kuivuruga CUF?
5. Maalim Seif Sharif Hamad ni kiongozi wa umma na kwa silimia 100% anaiwakilisha Zanzibar kupitia Upinzani, Wazanzibari wenyewe ndio waliomkubali Maalim Seif lakini tunashindwa kufahamu watu nje ya Zanzibar wanakuja na hoja kutoka katika mawazo yao kujaribu kuipotosha CUF lakini ni jambo ambalo miaka nenda miaka rudi CUF bado inapaa na kukua kila siku.
Hamad Rashid alikuja na mtazamo na fikra kama za kwako lakini hakuna aliyemsikiliza Wazanzibari wameendelea kuunganika kumsupport Maalim Seif. Na kwa taarifa yako tu October Inshaalah utapata majibu muruwa.