BujiBuji, weusi si rangi bali ni 'hali'. Infact hakuna kitu kama rangi nyeusi hapa duniani, kwanini nasema haya?!
Ili rangi iwe rangi inabidi iwe na uwezo wa kutoa mwanga wa rangi husika, mfano utakuta kuna taa zinazotoa mwanga wa bluu, 'orange', kijani n.k, lakini hatakuta taa inayota mwanga mweusi!
Weusi ni hali ya kushindwa ku-reflect/kuakisi rangi yoyote ile kati ya zile rangi milioni takrian 7 zilizopo kwenye mwanga mweupe, na badala yake huzinyonya rangi hizo zote na kuacha hali ya giza kwenye eneo husika, ambapo wewe umeamua kuita ni 'rangi nyeusi', lakini neno sahihi ni 'hali ya weusi'...!
Kitu cha bluu hunyonya rangi zote zilizo kwenye mwanga mweupe na kuakisi/ku-reflect rangi moja tu ambayo ni rangi ya bluu.., hali kadhalika kwa rangi zingine zote.., lakini vitu vyenye hali ya weusi havina uwezo huo!