Maajabu ya Rangi 3 za msingi

Maajabu ya Rangi 3 za msingi

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
40,617
Reaction score
46,713
Hapa duniani inakadiriwa kwamba kuna rangi takribani milioni 6 mpaka 7 ambazo zinaweza kuonekana kwa kutumia macho bila msaada wa kifaa chochote kile!

Pia inafahamika kwamba rangi hizo zote zinatokana na mchanganyiko wa rangi tatu za msingi ambazo ni Nyekundu, Kijani, na Kibluu. Mfano rangi ya Chungwa, Udhurungwi, Zambarau n.k hupatikana kwa kuchanganya rangi hizo tatu kwa uwiano flani ili kupata matokeo tarajiwa.

Lakini vile vile mchanganyiko wa mwanga wa rangi tatu za msingi huleta mwanga wa rangi nyeupe, hivyo tunasema mwanga wa rangi nyeupe ni mchanganyiko wa rangi zote duniani, na consequently ukiutawanya mwanga mweupe utaziona rangi hizo zote.

Utaalam/ujuzi huu umekuwa muhimu sana katika ugunduzi wa taa za LED zenye mwanga mweupe na ambao huokoa umeme kwa asilimia 90%! Hapo awali iliwezekana kutengeneza 'light emitting diode' (LED) zenye kutoa mianga yenye rangi nyekundu na kijani, baada ya miaka mingi ya uhangaikaji iliwezekana kutengeneza 'LED' zenye kutoa mwanga wa bluu na hivyo muunganiko wa hizo tatu uliwezesha utengenezaji wa taa za LED nyeupe na kuleta mapinduzi katika teknolojia zenye kuokoa nguvu ya umeme!
 
rangi nyeusi

BujiBuji, weusi si rangi bali ni 'hali'. Infact hakuna kitu kama rangi nyeusi hapa duniani, kwanini nasema haya?!

Ili rangi iwe rangi inabidi iwe na uwezo wa kutoa mwanga wa rangi husika, mfano utakuta kuna taa zinazotoa mwanga wa bluu, 'orange', kijani n.k, lakini hatakuta taa inayota mwanga mweusi!

Weusi ni hali ya kushindwa ku-reflect/kuakisi rangi yoyote ile kati ya zile rangi milioni takrian 7 zilizopo kwenye mwanga mweupe, na badala yake huzinyonya rangi hizo zote na kuacha hali ya giza kwenye eneo husika, ambapo wewe umeamua kuita ni 'rangi nyeusi', lakini neno sahihi ni 'hali ya weusi'...!

Kitu cha bluu hunyonya rangi zote zilizo kwenye mwanga mweupe na kuakisi/ku-reflect rangi moja tu ambayo ni rangi ya bluu.., hali kadhalika kwa rangi zingine zote.., lakini vitu vyenye hali ya weusi havina uwezo huo!
 
BujiBuji, weusi si rangi bali ni 'hali'. Infact hakuna kitu kama rangi nyeusi hapa duniani, kwanini nasema haya?!

Ili rangi iwe rangi inabidi iwe na uwezo wa kutoa mwanga wa rangi husika, mfano utakuta kuna taa zinazotoa mwanga wa bluu, 'orange', kijani n.k, lakini hatakuta taa inayota mwanga mweusi!

Weusi ni hali ya kushindwa ku-reflect/kuakisi rangi yoyote ile kati ya zile rangi milioni takrian 7 zilizopo kwenye mwanga mweupe, na badala yake huzinyonya rangi hizo zote na kuacha hali ya giza kwenye eneo husika, ambapo wewe umeamua kuita ni 'rangi nyeusi', lakini neno sahihi ni 'hali ya weusi'...!

Kitu cha bluu hunyonya rangi zote zilizo kwenye mwanga mweupe na kuakisi/ku-reflect rangi moja tu ambayo ni rangi ya bluu.., hali kadhalika kwa rangi zingine zote.., lakini vitu vyenye hali ya weusi havina uwezo huo!
nadhani muulizaji anataka kujua rangi nyeusi ni inapatikana kwa kuchanganya rangi zipi...coz rangi nyeusi ipo na inatumika
 
nadhani muulizaji anataka kujua rangi nyeusi ni inapatikana kwa kuchanganya rangi zipi...coz rangi nyeusi ipo na inatumika
Rangi ile hupatikana kwa kutumia powder zenye hali ya weusi.., na kama nilivyosema, ile si rangi. Haipatikani kwa kuchanganya zile rangi tatu za msingi.
 
Rangi ile hupatikana kwa kutumia powder zenye hali ya weusi.., na kama nilivyosema, ile si rangi. Haipatikani kwa kuchanganya zile rangi tatu za msingi.
sawa mkuu..ila ninachokumbuka

ni kuwa ukichukua zile rangi tatu(kijani.nyekundu na blue) na kuzichanganya unapata njano,dhambarau na bluu mpauko
nyekundu + blue = dhambarau
nyekundu + kijani = njano
kijani + blue = blue mpauko

zen ukichanganya hizo rangi zilizopatikana(njano,dhambarau,bluu mpauko) unapata rangi nyeusi
njano + dhambarau + bluu mpauko = nyeusi

hapo unasemaje?
 
Umenikumbusha formula yangu ya sekondari, GREYE means green+red=yellow. Black means absence of colour. Hapa namkumbuka Mzee wa mbwembwe "Time is a limiting factor, let us end here....." Hapo yupo mlangoni akikusanya vimia mia vyake
 
Umenikumbusha formula yangu ya sekondari, GREYE means green+red=yellow. Black means absence of colour. Hapa namkumbuka Mzee wa mbwembwe "Time is a limiting factor, let us end here....." Hapo yupo mlangoni akikusanya vimia mia vyake

Bila Shaka unamzungumzia moudy physics... Mchikichin hiyo aise pale tumepitia wengi
 
sawa mkuu..ila ninachokumbuka

ni kuwa ukichukua zile rangi tatu(kijani.nyekundu na blue) na kuzichanganya unapata njano,dhambarau na bluu mpauko
nyekundu + blue = dhambarau
nyekundu + kijani = njano
kijani + blue = blue mpauko

zen ukichanganya hizo rangi zilizopatikana(njano,dhambarau,bluu mpauko) unapata rangi nyeusi
njano + dhambarau + bluu mpauko = nyeusi

hapo unasemaje?
Ray lee black is the absence of color. huo mchanganyiko huleta hali ya kushindwa kuakisi rangi ya aina yoyote ile kutoka kwenye mwanga mweupe. hivyo kinachotokea hapo ni giza a.k.a weusi.
 
sawa mkuu..ila ninachokumbuka

ni kuwa ukichukua zile rangi tatu(kijani.nyekundu na blue) na kuzichanganya unapata njano,dhambarau na bluu mpauko
nyekundu + blue = dhambarau
nyekundu + kijani = njano
kijani + blue = blue mpauko

zen ukichanganya hizo rangi zilizopatikana(njano,dhambarau,bluu mpauko) unapata rangi nyeusi
njano + dhambarau + bluu mpauko = nyeusi

hapo unasemaje?
Umechemka wewe. Njano ni rangi ya msingi. Haipatikani kwa kuchanganya rangi zingine. Rangi za msingi ni Njano, Bluu na Nyekundu
 
Umenikumbusha formula yangu ya sekondari, GREYE means green+red=yellow. Black means absence of colour. Hapa namkumbuka Mzee wa mbwembwe "Time is a limiting factor, let us end here....." Hapo yupo mlangoni akikusanya vimia mia vyake

Yellow ni rangi ya msingi,haipatikani kwa kumix na rangi yyte
 
Umechemka wewe. Njano ni rangi ya msingi. Haipatikani kwa kuchanganya rangi zingine. Rangi za msingi ni Njano, Bluu na Nyekundu
sikubishii coz wapo wanaosema hivyo pia..so unaweza kuchukua unachoamini ww
RGB_color-Model.png
 
Back
Top Bottom