Maajabu ya Jiji la Dar es Salaam

Maajabu ya Jiji la Dar es Salaam

Leo nimeyaona maajabu ya Dar, kila mahali ni mto...........
 
NI jiji pekee ambalo watu wakipata majanga (mafuriko +mabomu) wanapozwa na ubwabwa na kutulia
 
Ni jiji pekee ambalo linafikiriwa kujengewa barabara za juu wakati wengine hawana hata hizo za chini.
 
Ni jiji pekee ambalo limeharibiwa na wakuja
ni jiji pekee ambalo wenyeji wake hawajaendelea na wanawasingizia wageni kwa ufukara wao kuwa ndiyo chanzo cha ufukara wao wakati wao (wenyeji) wamekalia kusogoa vijiweni na kujipaka rangi mwilini kwa w/wake
 
Ni jiji pekee linaloongoza kipindi cha mfungo wa Ramadhani biashara ya Kitimoto inadorora lakini baada ya mfungo
kumalizika biashara inashamiri Jiulize kwanini????
 
ni jiji pekee ambalo wenyeji wake hawajaendelea na wanawasingizia wageni kwa ufukara wao kuwa ndiyo chanzo cha ufukara wao wakati wao (wenyeji) wamekalia kusogoa vijiweni na kujipaka rangi mwilini kwa w/wake

Ilala ni Wilaya Tajiri katika Tanzania.
 
-Ni jiji pekee duniani ambalo mabomu ya serikali yamelipuka ovyo mara kadhaa na kuwauwa watu na kuharibu mali zao bila kufidiwa kihalali na wakati halali.
-Ni jiji pekee duniani wakazi wake wanafanya gwaride bila kupenda,asubuhi wanaelekea katikati ya mji na jioni wanarudi walikotoka.
-Ni jiji pekee ambapo nyumba zote za serikali zimeuzwa na watumishi wake wanaishi mahoteli ya kifahari.
-Ni jiji pekee ambapo wahindi wanang'ang'ania vijumba vya wanafunzi njini ingali wana uwezo wa kujenga za kwao.
-Ni jiji ambalo askari ni wengi lakini usalama ni mdogo sana
-Ni jiji pekee barabara zake zina matuta kila mahali eti watu wanagongwa sana
-Ni jiji pekee utakuta chupa zilizoisha maji zimetupwa barabarani zimejaa mikojo.
-Ni jiji pekee ukimgonga mtembea kwa miguu basi raia huchukua sheria mkononi kwa kukuua na kuchoma gari lako.
-Ni jiji pekee mwanamke akipata bwana anakuwa amepata muwekezaji, utakoma kwa kutoa pesa, voucher na kodi ya chumba.
-Ni jiji pekee watoto wengi hushuhudia wazazi wao wakifanya mapenzi kisingizio hapa mjini chumba ni kimoja.
-Ni jiji ambalo ukiwa baa mtu uliyekaa naye meza moja atakwambia yeye ni usalama wa taifa.
-Ni jiji pekee wauza mafuta ya magari wanaweza kugoma kuuza mafuta bila kuogopa serikali.
-Ni jiji pekee kuingia mahabusu bure lakini kutoka lazima uwe na hela.
endeleeni!!!!
Bila shaka haya yote yamekukuta!.
Mbavu zangu jaman huko Dar(Bongo) hameni. Nipo huku Canada.
 
Ni jiji pekee linaloongoza kipindi cha mfungo wa Ramadhani biashara ya Kitimoto inadorora lakini baada ya mfungo
kumalizika biashara inashamiri Jiulize kwanini????
Walaji wa take away(chips) wauzaji wake na mazingira yao machafu...lakin walaji wanapanga foleni.
Jiulize kwa nini?
 
NI jiji ambalo mchana wa2 wanaingia kwenye daladala MILANGONI ila asubuhi na jioni wanaingilia MADIRISHANI.
 
NI jiji ambalo hakuna Mapinduzi ya kweli yatakayo anzia hapo..coz kama walivyoongea wengine asilimia kubwa ya vijana wa Dar wanapenda fedha pasipo kufanya kazi......na haishangazi kuona karibu majimbo yote isipokuwa mawili tu yalichukuliwa na Chama tawala...
 
Ni jiji pekee ambalo lina joto na kero zote zinazomkabili binadamu kuliko majiji yote duniani.Lakini cha ajabu hata rais anaishi humo
 
kile kipindi cha jiji letu cha itv ilifaa waonyeshe uozo wa jiji hili. Kila kitu kwenye huu mji ni ovyo sana, alaf ndio lango kuu la wageni. Hivi wakienda huko makwao si sifa mbaya kwa watanzania wote!

Kama tu wanaowapokea yaani viongozi wetu walivyo na sifa mbaya ya ufisadi inatosha kwa wageni kwenda kututangaza vibaya
 
Back
Top Bottom