Maajabu ya Jiji la Dar es Salaam

Kintiku

JF-Expert Member
Feb 3, 2011
617
319
  1. Ni jiji pekee ambalo mtu hujenga kwanza na kuomba kibali baadaye = Ujenzi holela
  2. Ni jiji Pekee ambalo halina building codes katika ya jiji (city center)
  3. NI jiji Pekee ambalo mtu hujenga jengo la hata orofa 18 bila kujenga maegesho ya magari
  4. Ni jiji pekee ambalo mtu akiwa na matofali ya kutosha na viezekeo basi hujenga ghorofa popote -cheki pale Kariakoo
  5. Ni jiji pekee ambalo 80% ya makazi yake ni holela (unplanned)
  6. Ni jiji pekee ambalo ukiwa unatoka katika ya mji umbali hata wa km 10 bado kuna foleni ya kutisha kutoka nje ya jiji kimara, mbezi, tegeta, mbagala)
  7. Ni jiji pekee ambalo 70% ya maeneo yake yananuka kinyesi
  8. Ni jiji ambalo huwa na mito mingi sana kwa muda mfupi wakati wa mvua (kutiririsha choo)
  9. Ni jiji pekee ambalo weekend huwa na foleni kubwa katika ya mji- miji mingi huwa hakuna foleni watu wanaenda mashambani/ picnic etc
  10. Ni jiji pekee ambalo lina nyumba nyingi za wageni kuliko idadi ya wageni wanaoingia jijini- Guest houses nyingi kuliko makanisa na misikiti
  11. Ni jiji pekee ambalo watu wake wengi hawajitambui na hawajui haki zao
  12. Ni jiji pekee Duniani ambalo 95% ya magari ya kuzoa taka yenyewe tu ni takataka
  13. NI jiji pekee ambalo mtu anaweza kuanzisha baa, ukumbi hata katikati ya makazi ya watu bila shida
  14. NI jiji Pekee ambalo mtu anaweza akaamua kufunga barabara na maisha yakaendelea tu
  15. Ni jiji pekee ambalo wakazi wake wengi hawajawahi kumiliki chombo cha moto zaidi ya pasi
  16. .....
  17. ......


 
hongera sana mtoa mada Nakubaliana kabisa na yote
3. Ni kweli kabisa maegesho hakuna, tumebaki kusikia sera "Mtambuka" zisizotekelezeka zikipaacha katikati ya mji na kutambukia kwa wanyonge.
13. hasa inapofika usiku, bila kujali moshi kwenye majengo katikati ya jiji , usiku mitaa ugeuzwa majiko ya kuchomea kuku wenye kutoa moshi mzito sana na hakuna hatua yo yote inayochukuliwa.(mh! sijui ingefanywa na chinga ingekuwaje?)
14. hii naikubali hasa kwa visingizio vya ujenzi, pia kumechangia sana mchanga wa ujenzi kuziba undergroung drainages.
+ Ni jiji ambalo kontrakta wake ni mmoja tu Linza. sijui CRB, National Construcion Council hawajashitukia diri hili la floor moja kwa Tsh. 1,500,000/=?!
 
Duu umenishtua kuhusu Linza. hivi huyu ndo mtaalamu wa zege hapa Dar? Maana kila kibao cha ujenzi lazima nione hilo jina.
 
Si kweli kuwa ni mtaalamu, bali akili inayotumika hapa ni kuwa, wajenzi wasomi hawapewi kujenga maghorofa yetu ila wale mafundi wetu wa kimara, G/Mboto,ndio wajenzi wa majengo haya, wao ununua kipande cha ujenzi wa jengo kwa kulipwa na wenye majengo bei ndogo. Ila, ili jengo lisimame lazima awepo kontrakta mkuu na bango lake. Sasa basi Linza ndiye rahisi kununuliwa na wenye majengo kwa kusimamisha hilo bango unaloliona. Floor moja analipwa Tsh. 1,500,000/=. Lakini wajenzi wakuu ni hao mafundi wetu wa mitaani. KARABAGAO
 
kile kipindi cha jiji letu cha itv ilifaa waonyeshe uozo wa jiji hili. Kila kitu kwenye huu mji ni ovyo sana, alaf ndio lango kuu la wageni. Hivi wakienda huko makwao si sifa mbaya kwa watanzania wote!
 
  1. Ni jiji pekee ambalo mtu hujenga kwanza na kuomba kibali baadaye = Ujenzi holela
  2. Ni jiji Pekee ambalo halina building codes katika ya jiji (city center)
  3. NI jiji Pekee ambalo mtu hujenga jengo la hata orofa 18 bila kujenga maegesho ya magari
  4. Ni jiji pekee ambalo mtu akiwa na matofali ya kutosha na viezekeo basi hujenga ghorofa popote -cheki pale Kariakoo
  5. Ni jiji pekee ambalo 80% ya makazi yake ni holela (unplanned)
  6. Ni jiji pekee ambalo ukiwa unatoka katika ya mji umbali hata wa km 10 bado kuna foleni ya kutisha kutoka nje ya jiji kimara, mbezi, tegeta, mbagala)
  7. Ni jiji pekee ambalo 70% ya maeneo yake yananuka kinyesi
  8. Ni jiji ambalo huwa na mito mingi sana kwa muda mfupi wakati wa mvua (kutiririsha choo)
  9. Ni jiji pekee ambalo weekend huwa na foleni kubwa katika ya mji- miji mingi huwa hakuna foleni watu wanaenda mashambani/ picnic etc
  10. Ni jiji pekee ambalo lina nyumba nyingi za wageni kuliko idadi ya wageni wanaoingia jijini- Guest houses nyingi kuliko makanisa na misikiti
  11. Ni jiji pekee ambalo watu wake wengi hawajitambui na hawajui haki zao
  12. Ni jiji pekee Duniani ambalo 95% ya magari ya kuzoa taka yenyewe tu ni takataka
  13. NI jiji pekee ambalo mtu anaweza kuanzisha baa, ukumbi hata katikati ya makazi ya watu bila shida
  14. NI jiji Pekee ambalo mtu anaweza akaamua kufunga barabara na maisha yakaendelea tu
  15. Ni jiji pekee ambalo wakazi wake wengi hawajawahi kumiliki chombo cha moto zaidi ya pasi
  16. .....
  17. ......



16- watu wengi wakija Dar kusoma hawarudi walikotoka (majumbani kwao/mkoa au kijiji).
 
Si kweli kuwa ni mtaalamu, bali akili inayotumika hapa ni kuwa, wajenzi wasomi hawapewi kujenga maghorofa yetu ila wale mafundi wetu wa kimara, G/Mboto,ndio wajenzi wa majengo haya, wao ununua kipande cha ujenzi wa jengo kwa kulipwa na wenye majengo bei ndogo. Ila, ili jengo lisimame lazima awepo kontrakta mkuu na bango lake. Sasa basi Linza ndiye rahisi kununuliwa na wenye majengo kwa kusimamisha hilo bango unaloliona. Floor moja analipwa Tsh. 1,500,000/=. Lakini wajenzi wakuu ni hao mafundi wetu wa mitaani. KARABAGAO



Mguse uone. Kuna wakati alikuwa na kesi ya jengo lilioanguka ERB wakamfungia. Waliona cha moto.... Sijui hata ile kesi iliishia wapi. Nafikiri kuna gamba mmoja anamlinda.
 
Hivi kumbe mkusanyiko wa magorofa yaliyo changanyika na vijumba, vibanda, takataka, msongamano, vibaka, joto n.k ndio unaitwaga "jiji"?
 
Ndyo jiji linalokuwa kwa kasi ingawa chafu,hata mtoa mada amekimbia kwao yupo Dar anashangaa,watu wake hawapendi siasa uchwara wapo busy kusaka hela,
 
Ni jiji linaloongoza kuonesha status ya maisha yao kwa wengine via majumba, magari, vyeo, biashara, magamba(vyeti), pesa na mengineyo!
 
JIJI PEKEE DUNIANI HUGEUKA BAHARI PINDI MVUA ZIKINYESHA!!:eyebrows:

Haswaa. Watu wake wengi ni wajuaji sana, anaweza hata kubishana na Profesa wa Kiswahili kuhusu neno la KIswahili (mfano. Hakunaga Suma Lee). Wao wanasema kila mtu hapa jijini ni msomi, maana kuweza kuishi Dar tu hiyo ni sawa na kumaliza kidato cha nne, kwa hiyo aliyemaliza kidato cha nne ni sawa na kidato cha sita, kidato cha sita= shahada, shahada= s/uzamili, s/uzamili= s/uzamivu...........
 
Ni jiji pekee ambalo watu wanawanua na kuchoma moto bila kuelewa alichoiba, hasa baada ya kusikia kelele ya mwizi tu....:A S embarassed:
 
Back
Top Bottom