Maajabu ya daraja la Kigamboni!

Hivi hili tangazo lilitolewa kwenye Daily news tu?

Wenye pesa zao nje ya TZ wametangaziwa vipi kwa sababu sidhani kama kuna kampuni yoyote ya kitanzania ambayo ina uzoefu na utaalamu wa PPP hasa ya barabara na madaraja? Au haya makampuni ya nje yataletwa kupitia connection zao na wanasiasa tu kama Richmond n.k?

Suala la kuwa makampuni ya Tanzania yataweza au la nadhani hilo litaamuliwa na wataalam

lakini mimi nimeliona tangazo mpaka kwenye site ya UNDP na kama kuna kampuni ambayo iko serious kufanya hii shughuli then sidhani kama kutakuwa na tatizo hata kidogo kujua kama kuna tenda imetangazwa sasa sidhani kama kuna tatizo la kupata hizo kampuni kwenye pre qualification

Na hapa inabidi NSSF wapewe apate credits kwani kila kitu kiko wazi na Open sasa hatujui kama huko mbele wanasiasa kama akina Magufuli na akina Mgonja na wapambe wao wakianza kutia mikono yao kama wizara ya ujenzi walivyofanya


Kilichonisikitisha ni kuwa GREY MGONJA deliberately aliamua kutotoa hiyo LETTER OF PRIORITY AND GUARANTEE kwa ajili ya ujenzi wa daraja. Sasa kama si UFISADI sijui ni nini lakini kesho tutakwenda kwenye uchaguzi huku ilani ya uchaguzi haijakamilika

halafu mlikuwa mnatafuta nani wanaomsabotage JK

Sasa hivi hatujui kwa nini directives za Rais zinapuuzwa left and right na cha kujiuliza directives ngapia za Rais hawa jamaa washazipuuza.

Sijui KAPUYA naye kasimama wapi kwenye hili lakini simsikii babisaa lakini usije shangaa kuwa naje kafunikwa na akina Kijazi kwenye hili


In short hii issue ya daraja la kigamboni inaonyesha jinsi gani serikali yetu inavyoyumba. Leo hii nadhani ilitakiwa hii kitu ishakamilika kisha sisi tuanze kulalamikia mambo mengine
 
Tunaishi kwenye nchi ambayo kifo cha watu 10 au 20 kwa mwaka hapo kivukoni, au kuchelewa kazini kwa walala hoi wachache wanaoishi kigamboni sio tatizo kubwa kwa viongozi wetu. Watu wanalala usingizi bila shida. Viongozi wetu wanakuwa na busara zaidi na kuona umuhimu au kuyatambu matatizo ya wananchi kipindi cha uchaguzi tu. uchaguzi ukipita akili za viongozi wetu zinajaa funza na wanafanya mambo ambayo hata ukija uchaguzi mwingine akili zikiwarudia wanayaona kuwa ni dhambi (wakati huo) na ni wepesi kuyakanusha.

Kule Singida kuna simba wawili wameendelea kuua watu na mifugo yao kwa zaidi ya miezi sita. Simba mmoja ndio kauwawa wiki iliyopita baada ya kuua Wasingida 14 na mifugo kadhaa! Mkuu wa Mkoa akaenda pale, akapiga picha na simba aliyekufa na akatoa pongezi nyingi kwa waliofanikisha kumuua simba yule. Tuna muundo mzuri sana wa serikali nchi hii; ipo ya KIJIJI, KATA, TARAFA, WILAYA, MKOA hadi TAIFA. Utendaji tu ndio unaoleta shida hasa kwenye MAAMUZI na USIMAMIZI.
 
Kama ilivyozoeleka ..hao Wadachi wakitoa Grant basi hapo hakuna ulaji wa maana kwa makampuni Watz na wale wa 10% Miundombinu! Mtu yuko tayari kuliko asipate hapo kitu basi na daraja lisijengwe!

Kwa kifupi ni kukosa tu uzalendo na kuweka kwanza maslahi binafsi mbele!

Maana sasa miaka zaidi ya 15 kweli Tz tunashindwa kufikia maamuzi jambo dogo hivi.. je makubwa tutaweza?

siyo mara ya kwanza kutokea,hata pesa ya Barabdara y aAli hassan Mwinyi ilikuwa hivi hivi
 
siyo mara ya kwanza kutokea,hata pesa ya Barabdara y aAli hassan Mwinyi ilikuwa hivi hivi

the most interesting part ni kua hautosikia magazeti ya akina KUBENEA yakimlalamikia GREY MGONJA ambaye zaidi ya kuwa one of the top civil servants amekuwa instrumental katika kublock mipango ya maendeleo kama hili la daraja na kusaini mikataba mbali mbali ya kifisadi..sihitaji kusema mengi hebu soma hapa:
 
Kuna taarifa kuwa kuna watawala ofisi kuu tatu za serikali ambao wana conspiracy daraja la kigamboni lisijengwe. Hii sitoileta kwa style muziki kama MKJJ lakini I wont hesitate to drop names.Hivyo nawaomba radhi wale ambao wataona majina ya hao watawala ambao wako karibu nao

Nipeni muda namalizia ku compile file zima

Game Theory, can you please be kindly enough to mention those dirty names heres since JF we dare to speak openly?
 
ujenzi Wa Daraja La Kigamboni Ambao Unatarajiwa Kuanza Hivi Karibuni . Ujenzi Huo Ambao Utatekelezwa Na Serikali Kwa Pamoja Na Nssf Kama Main Financer Au Kama Mwekezaji Wa Mradi Huo Mkubwa.mradi Huo Mkubwa Kuchukuliwa Na Kuekelezwa Na Nssf Ni Mkubwa Na Wa Aina Yake Kutekelezwa Na Mfuko Huo Wa Penseni Utagharimu Zaidi Ya Shillingi Billioni 35. ( 35,0000,000,0000.00)na Mradi Huo Utaendeshwa Kwa Mtindo Wa Build, Run And Transfer Yaani Wawekezaji Nssf Watawekeza Hizo Billion 35 Za Walalahoi Yaani Michango Yetu Sisi Kwenye Hili Daraja Na Kuliendesha Kama Road Toll . Kwa Muda Wa Miaka 25 Na Baada Ya Hapo Watalikabidhi Kwa Serikali Waliendeshe Wenyewe.
Mutakumbuka Ya Kwamba Nssf Imeanzishwa Kama Ni Mfuko Wa Pensheni Kwa Wafanyakazi Wa Makampuni Ya Binafsi Yaani Private Sector . Inatarajiwa Hawa Nssf Wawekeze Katika Miradi Ambayo Itakua Na Tija Ili Wastaafu Waweze Kupata Faida Kubwa Wakati Wa Kustaafu . Hili Ndio Lengo La Mfuko Huu Wa Nssf.
Huu Mradi Wa Daraja La Kigamboni Hauna Tija Ni Wa Kisiasa Zaidi Na Pia Hata Hio Upembuzi Yakinifu Yaani Feasibilty Study Iliofanywa Anaonekana Ni Fake Na Haikuzingatia Ukweli Yakinifu Kwamba Ni Hasara Kubwa Kwetu Sisi Tunaochanga Ndani Ya Mfuko Huo Kwa Kutegemea "viji9senti" Tutapokua Tumestaafu.
Laiti Hizi 35 Billion Za Michango Yetu Zingewekezwa Katika Miradi Mingine Kama Real Estates Basi Uwezekano Wa Wanachama Kupata Bonus Kwa Wanachama Ni Mkubwa Sana.
Inawezekana Hapa Kuna Ufisadi Wanalazimishwa Nssf Kuingia Ili Watu Wapate Ulaji.
35,000,000,000/= Ni Nyingi Mno Kuzirejesha Na Kupata Faida Kwenye Daraja. Fedha Hizi Ili Zirudi Kwa Faida Ya Wanachama Basi Daraja Hili Liwe Na Uwezo Wa Kuipatia Nssf Tzs 615,881,988.56 Kila Mwezi (ukichukulia Interest Ya 21% Inayotolewa Na Mabenki Kama Mikopo ). Sasa Jee Nssf Wataweza Kupata Tzs 615,881,988.56
Kwa Mwezi? Ukweli Hapana Hata Kama Kila Gari Itatozwa Tshs:1000 Kwa Kila Trip Moja Inayopita Kwenye Daraja Hilo.hata Kama Kutakua Na Investment Aina Gani Huko Kigamboni Haitarajiwi Kuwa Na Movements Ya Magari Zaidi Ya 1000 Kwa Siku Kutumia Daraja Hilo . Hivyo Nssf Watarajie Kupata Tshs:30,000,000/= Kwa Mwezi . Si Dhani Kama Itaku Haki Kuwatoza Ushuru Wataopita Kwa Miguu Kwenye Daraja Hilo.
Kwa Hio Nssf Wacheni Kuingia Kwenye Mradi Huu Kwa Kutumia Mapesa Yetu Wanachama Hauna Faida Kwetu Na Kwa Mfuko Ni Hasara Kubwa.ila Labda Kuna Maslahi Ya Kifisadi Tu.
Daraja Lijengwe Lakini Si Na Nyinyi Nssf Bali Serikali Itafute Fedha Zake Wenyewe Kwa Wafadhili Wafanikishe Huu Mradi Na Sio Nssf . Mukiendeleza Na Mradi Huu Basi Hamtakua Mumetenda Haki Kwa Wanachama Wa Mfuko Huu.
Natoa Mwito Kwa Nssf Wastop Kuendeleza Mradi Huu. Nssf Ni Kwa Wanachama Wa Mfuko Huo Sio Kazi Yake Kuingia Katika Miradi Ya Miundo Mbinu Hii Ni Kazi Ya Serikali Kuu Inayokusanya Kodi. Nssf Wanatukata Sisi Kwa Ajili Yetu Kupata Mafao Bora Na Mengi Zaidi Kuliko Sasa Ambapo Tunapata Sio Zaidi Ya Kile Tulichochanga Kwani Mfuko Huu Unatumiwa Vibaya.
Ndio
 
Game Theory, can you please be kindly enough to mention those dirty names heres since JF we dare to speak openly?


WALIOKUWA WAKIKWAMISHA UJENZI WA WA DARAJA LA KIGAMBOPNI NI HAWA:

Mheshimiwa JOHN POMBE MAGUFULI -alipokuwa wizara ya UJENZI


GREY MGONJA-Aalipokuwa katibu mkuu kule Hazina


Eng JOHN KIJAZI-alipokuwa katibu kule wizara ya UJENZI


JOSEPH RUGYAMHETO-alipokuwa PS kule utumishi
 
WALIOKUWA WAKIKWAMISHA UJENZI WA WA DARAJA LA KIGAMBOPNI NI HAWA:

Mheshimiwa JOHN POMBE MAGUFULI -alipokuwa wizara ya KAZI


GREY MGONJA-Aalipokuwa katibu mkuu kule Hazina


Eng JOHN KIJAZI-alipokuwa katibu kule wizara ya Kazi


JOSEPH RUGYAMHETO-alipokuwa PS kule utumishi

John Pombe Magufuli na Eng. John Kijazi hawajawahi kufanya kazi wizara ya Kazi. Ila Magufuli amewahi kuwa waziri katika wizara ya ujenzi na John Kijazi katibu mkuu wa wizara ya ujenzi enzi za utawala wa uwazi na ukweli.
 
Last edited:
John Pombe Magufuli na Eng. John Kijazi hawajawahi kufanya kazi wizara ya Kazi. Ila Magufuli amewahi kuwa waziri katika wizara ya ujenzi na John Kijazi katibu mkuu wa wizara ya ujenzi enzi za utawala wa uwazi na ukweli.



KWELI

MAGUFULI alikuwa wizara ya UJENZI wakati ule KAPUYA ndio alikuwa wizara ya KAZI


NAni kweli vile vile ENGINEER JOHN KIJAZI alikuwa PS MoW

asante kwa kunirekebisha hapo
 
Bridge of the Horn ....


Wakati sie wabongo tunapingana na kushindana nani atajenga Daraja au wengine kuona hakuna umuhim wa Daraja kama Hilo,Wenzetu wa NCHi zingine wanafanya Makubwa ya Kujenga Daraja la Nguvu la Kilometre 14 kutoka Djibuout to Yemen...linaitwa BRIDGE OF THE HORN unaweza search ktk google utakuta useful information.

http://www.eriplanet.com/news/horn-of-africa/4088.html


angalia hio.... 070502-redsea.jpg

Ubwege au UFISADI wa Viongozi wetu wa Kuhitaji 10% ktk Kila Miradi utakwisha LINI?
 
maswali yameisha?

Mkuu GT na wanaJamvi, leo nimeisoma hii kwenye Nipashe naona hawa jamaa sasa wanaanza mazingaombwe manake kama mtoa chochote ndiyo hivyo tena itakuwaje na kadaraja ketu haka pale Kigamboni? Ina maana ule ucheleweshaji ulikuwa ni kushindwa kwa NSSF?? Just thinking out loud!!!

NSSF yajitoa ujenzi wa daraja la Kigamboni

2008-10-30 13:11:13
Na Richard Makore


Ujenzi wa Daraja la Kigamboni liliIokuwa linasubiriwa kwa hamu na wakazi wa Kigamboni, jijini Dar es Salaam sasa umekwama baada ya Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kujitoa ramsi katika kazi hiyo.

Awali NSSF ilisema, itajenga daraja hilo ambalo lingeunganisha Kigamboni na maeneo mengine ya Jiji la Dar es Salaam.

Daraja hilo lenye urefu wa mita 100 eneo la Kurasini kwa sasa litajewanga kwa ubia wa kampuni binafsi itakayojitokeza pamoja na serikali.

Mkurugenzi wa Habari wa Wizara ya Miundombinu, Martin Ntemo alisema baada ya NSSF kushindwa kujenga daraja hilo ilipewa kazi ya kumtafuta mtu ambaye anaweza kufanya kazi hiyo.

Aliongeza kuwa mchakato wa kumtafuta mtu au kampuni itakayofanya kazi hiyo umekamilika.

Hata hivyo, hakusema ni lini kazi hiyo itaanza ili kuwaondolea wakazi wa Kigamboni usumbufu wa kutegemea kivuko kwa ajili ya usafiri.
Eneo la Kigamboni ni moja ya maeneo ambayo yanaonekana yametengwa kutokana na tatizo la kutokuwepo daraja.

SOURCE: Nipashe
 
Back
Top Bottom