youngkato
JF-Expert Member
- Sep 3, 2014
- 3,638
- 3,641
Hi ni biashara pekee ambayo mtu au mchimbaji anaweza kukukopesa hata milioni 50 bila kuandikishana au kuwepo na shahidi yoyote.
Ni biashara ambayo mtu anaweza kukuuzia udongo ambao hauna uhakika wa kilichomo ndani.
Ni biashara ambayo pamoja na mtu anaweka pesa kubwa, ila wanaamini uchawi kwa asilimia 90
Biashara ya dhahabu ni biashara ambayo inaweza ikakufanya milionea kwa mwezi mmoja na ikachukua pesa zako zote ukawa maskini ndani ya miezi mitatu.
Ardhi ina siri nyingi sana na pesa ina siri nyingi sana.
Unaweza ukachimba shimo au duara ukaambulia udongo tu, ila mwenzako akachimba pembeni tu akapata utajiri.
Pamoja na pesa walizonazo wachimbaji wa dhahabu, hakuna mtu mwenye pesa za kuwekeza kwa kiwango kikubwa cha kutumia sayansi kama wazungu.
Dhahabu ambayo tayari imechimbwa ni kama asilimia 3 tu ya dhahabu ambayo haijaguswa Tanzania.
Nimefanya kazi kwenye uchimbaji miiaka nane hakuna kitu utanidanganya kwenye dhahabu.
Ni biashara ambayo mtu anaweza kukuuzia udongo ambao hauna uhakika wa kilichomo ndani.
Ni biashara ambayo pamoja na mtu anaweka pesa kubwa, ila wanaamini uchawi kwa asilimia 90
Biashara ya dhahabu ni biashara ambayo inaweza ikakufanya milionea kwa mwezi mmoja na ikachukua pesa zako zote ukawa maskini ndani ya miezi mitatu.
Ardhi ina siri nyingi sana na pesa ina siri nyingi sana.
Unaweza ukachimba shimo au duara ukaambulia udongo tu, ila mwenzako akachimba pembeni tu akapata utajiri.
Pamoja na pesa walizonazo wachimbaji wa dhahabu, hakuna mtu mwenye pesa za kuwekeza kwa kiwango kikubwa cha kutumia sayansi kama wazungu.
Dhahabu ambayo tayari imechimbwa ni kama asilimia 3 tu ya dhahabu ambayo haijaguswa Tanzania.
Nimefanya kazi kwenye uchimbaji miiaka nane hakuna kitu utanidanganya kwenye dhahabu.