Mabibi na mabwana kumekuwa na shamra shamra nyingi hasa kutokea kwa wale makada nguli wa chama mboga mboga kuwa bwana Nyalandu katoka Chadema.
Ajabu ni kuwa furaha zimeelekezwa kwenye kuwa bwana huyu asiyekuwa na jina ndani ya Chadema, ametoka Chadema wala si kuwa kajiunga na CCM!
Maajabu zaidi ya Mussa ni kuwa, kwa Chadema: "kuondoka kwake ni mithili ya kuvuja kwa pakacha ambayo ni nafuu mno, kwa mchukuzi."
Wajameni, kwanini CCM wanashangilia hivi kuwa huyu bwana katoka Chadema? Kwanini CCM hawashangilii kuwa kwa kajiunga nao? Kwamba labda sasa wamepata jembe mahiri la kulimia kweri kweri?
Kwamba, kuwa promo zote anazopewa huyu bwana, ni kuwa katoka Chadema na si kuwa kajiunga na CCM?!
Hiiiiii bagosha, pana nini hapa?
Au huyu bwana ana siri gani nzito ambazo CCM walikuwa zimewakosesha kabisa usingizi kila walipokumbuka kuwa huyu bwana yuko huko? Kwamba sasa ni heri mno katoka huko, na kuwa angalau sasa watapumua kwa nafasi waliniambia na kujimwaya mwaya?
Aliwabana nini CCM Nyalandu kuwa Chadema? Mbona hatuoni shamra shamra za kuwa huyu bwana sasa atawafaa na nini huko CCM?
Au labda tuseme ni yale mambo ya kumpongeza tu, kwa kuwa alishindwa kabisa kuziimba zile nyimbo zake za Sayuni alizozizowea alipokuwa huko?
Wajameni, furaha na shamra shamra hizi, sababu zake tafadhali.
Ninawasilisha
Ajabu ni kuwa furaha zimeelekezwa kwenye kuwa bwana huyu asiyekuwa na jina ndani ya Chadema, ametoka Chadema wala si kuwa kajiunga na CCM!
Maajabu zaidi ya Mussa ni kuwa, kwa Chadema: "kuondoka kwake ni mithili ya kuvuja kwa pakacha ambayo ni nafuu mno, kwa mchukuzi."
Wajameni, kwanini CCM wanashangilia hivi kuwa huyu bwana katoka Chadema? Kwanini CCM hawashangilii kuwa kwa kajiunga nao? Kwamba labda sasa wamepata jembe mahiri la kulimia kweri kweri?
Kwamba, kuwa promo zote anazopewa huyu bwana, ni kuwa katoka Chadema na si kuwa kajiunga na CCM?!
Hiiiiii bagosha, pana nini hapa?
Au huyu bwana ana siri gani nzito ambazo CCM walikuwa zimewakosesha kabisa usingizi kila walipokumbuka kuwa huyu bwana yuko huko? Kwamba sasa ni heri mno katoka huko, na kuwa angalau sasa watapumua kwa nafasi waliniambia na kujimwaya mwaya?
Aliwabana nini CCM Nyalandu kuwa Chadema? Mbona hatuoni shamra shamra za kuwa huyu bwana sasa atawafaa na nini huko CCM?
Au labda tuseme ni yale mambo ya kumpongeza tu, kwa kuwa alishindwa kabisa kuziimba zile nyimbo zake za Sayuni alizozizowea alipokuwa huko?
Wajameni, furaha na shamra shamra hizi, sababu zake tafadhali.
Ninawasilisha