1: Bandari inakosa Meli TPA wanakiri mizigo imepunga alafu serikali inasema hakuna mizigo Iliyopungua!!
2: V.A.T inapanda Gavana wa Benki kuu anasema hii itakuwa kwa Mteja Waziri wa fedha unakuja na kusema watoa huduma ndio watalipa!!
3: Rais anasimama na Kumuita mwananchi wake ****** alafu Mwananchi akimuita ****** anafunguliwa kesi ya jinai na faini ya milioni 7
4: Police anamkamata mtu kwa kosa la kuvuta bangi ambayo ni starehe binafisi anashindwa kukamata watu waliosababisha twiga wetu wakapanda ndege na kupelekwa nje ya nchi!!
5: TBC anashindwa kuonyesha bunge Live Wakati huohuo wanaonyesha Harusi live!!
6: Mikataba ya Nchi inapitishwa kwa hoja ya Dharura kama walivyofanya kwenye Gesi alafu Rais wa nchi anaenda kuwapa wananchi wake Magwangala!!
7: Mbunge wa Bunge anapewa Dakika 10 za kuongea bungeni 3 anaishukuru familia yake 3 anamsifia Rais Mtukufu 4 anawashambulia wabunge wenzake ambao mawazo yanakinzana na Baada ya hapo anasaini posho anaenda baa na kulala hoterini!!
Tutafika nchi ya viwanda kweli?