Maafisa Habari, Waandishi wa Habari kila mmoja atimize majukumu yake. Waandishi acheni kulazimisha kupewa hela kama haupo kwenye bajeti

Mchaga Tajiri

Member
Mar 14, 2023
10
16
Kuna tabia ambayo imeshika kasi kwa baadhi ya maafisa habari binafsi na hata wa Serikali.

Wanapoandaa matukio yao mara nyingi huwa wanavyombo vya habari ambavyo wamevialika, anapofika Mwandishi wa Habari ambaye hayuko kwenye orodha yao wengine huzuiwa kuchukua matukio Kwa kigezo kwamba hawako kwenye bajeti ambayo wameiandaa.

Au wakati mwingine anapofika mwandishi wa habari anaulizwa wewe ni wa chombo gani? Anapotaja chombo chake anaambiwa kwamba wewe sijakualika ni nani aliyekupa taarifa?

Hali hii sasa imesababisha hata Waandishi wa Habari wenyewe kwa wenyewe kushindwa kupeana taarifa zinazotokea kwenye maeneo yao kwa kuhofia kuulizwa na wadau wao waliowaalika kwa nini wameongeza watu wengine ambao hawako kwenye orodha.

Pamoja na yote wakati mwingine wapo baadhi ya waandishi ambao hata wakipewa nafasi ya kuchukua matukio na wanajua fika hawako kwenye orodha ya malipo wamekuwa ving'ang'anizi kuwasumbua wadau kuwapatia pesa kilazima akijua fika hayuko kwenye orodha.
 
Sasa mwaandishi akipewa bahasha ataandika habari kinyume na mtowa bahasha?

Ndio maana nimeacha kusoma magazeti siku nyingi tu, tena vile vigazeti vya michezo ndio takataka kabisa.
Kwani hiyo bahasha ina uhusiano gani na habari? habari za matukio wala hazina shida. kuna zile story ambazo unaibua mwenyewe kama mwandishi, au za kiuchunguzi ndio ukichukua bahasha unaweza kuandika wanayoyataka.

Habari nyingi za matukio wanaandika tu kilichozungumzwa hapo basi
 
Hii tabia ipo sana Kwenye mkoa wa Kilimanjaro na Arusha kule waanahabri wao kwa wao wanajuana na wale maafisa habri wana watu wao wakienda wageni wanateseka sana lazima wakuzuie. wenye raha ni wale wa magazeti na radio wao wakifika wanakaa tu na diary na voice recorder wanatulia kama wageni kumbe wapo kazini.

Changamoto inakuwa kwa wale wenye macamera tu.

Mimi ningekuwa mwandishi ningeenda popote kwenye matukio ya wazi na usingenifanya kitu, labdavikao tu ndio ningeomba ruhusa
 
Binafsi naona suala la waandishi wa habari inabidi liangaliwe upya, ikiwezekana mfumo ubadilishwe (sijui kama itawezekana).
Wengiwao wanaongoza kwa kulia njaa na ujanja ujanja, hiyo ni fedhea na aibu kwa tasnia.
 
Binafsi naona suala la waandishi wa habari inabidi liangaliwe upya, ikiwezekana mfumo ubadilishwe (sijui kama itawezekana).
Wengiwao wanaongoza kwa kulia njaa na ujanja ujanja, hiyo ni fedhea na aibu kwa tasnia.
Wengi hufanya kazi pasipo kulipwa Mishahara ya mwezi (Hawana mikataba) ya Ajira.

Kwahiyo huponea hizo Posho (bahasha) tu
 
Binafsi naona suala la waandishi wa habari inabidi liangaliwe upya, ikiwezekana mfumo ubadilishwe (sijui kama itawezekana).
Wengiwao wanaongoza kwa kulia njaa na ujanja ujanja, hiyo ni fedhea na aibu kwa tasnia.
sio kulia njaa mkuu mm nawaonaga wanaenda kwenye event kisha wanaitwa wachche wanalipwa nauli zao wengine wanapewa tu maji tena ya moto waondoke. japo mm sifagilii ikiwa hata mm nisingependa kabisa jambo hilo. Ni afadhali hizo posho zifutwe. kuna siku nilienda na boss wangu kwenye event fulan hivi alikuwa mgeni Rasmi baada ya kuhutubia wakamuita pembeni wafanye nae mahojiano.

Mimi kwa sababu nilikuwa na boss nilifuatana nae wakamuita nyuma ya ukumbi wakaja washikaji wanne na demu mmoja wakapiga naye interview nzuri kweli walipata story nzuri, kimbembe baada ya interview wakawa bado wanaongea ongea nae wanamchekea chekea

Nikamwambia boss kwa lugha wape nauli bila hivyo hawaondoki jamaa akatoa laki akawapa wagawane asee ile story waliitoa vizuri sana, kwa kweli. na kuanzia hapo wakawa wadau wetu wakubwa tukiwa na matangazo tunawaita,events semina n.k

Kama unaweza kuwapa chocote sio mbaya wengi wao wanapewa tu vitambulisho basi wakajitafutie hela mjini hawalipwi hasa radio za huku mikoani

kwa sababu wahitimu ni wengi na ajira hakuna kajiajiri kwa namna ya kipekee maana kama ni taasisi yako na wewe unapata expos sasa kumpa laki moja wewe utapungukiwa nini?
 
Kuna tabia ambayo imeshika kasi kwa baadhi ya maafisa habari binafsi na hata wa Serikali.

Wanapoandaa matukio yao mara nyingi huwa wanavyombo vya habari ambavyo wamevialika, anapofika Mwandishi wa Habari ambaye hayuko kwenye orodha yao wengine huzuiwa kuchukua matukio Kwa kigezo kwamba hawako kwenye bajeti ambayo wameiandaa.
Kwanza ni kweli.
Jambo la kwanza ni habari ni bure, dunia nzima!. Mwandishi wa habari/chombo cha habari ni jukumu lake kutafuta habari na kutangaza habari bure.

Kwenye uandishi wa habari kuna matukio ya aina 3
1. Public, Public events - haya ni matukio ya kawaida ya public kama sherehe za kitaifa, polisi, hospital, mahakamani, mwandishi yoyote wa habari au chombo chochote kiko free ku cover bila kualikwa na yeyote na hutaulizwa lolote na hutazuiwa na yeyote.
2. Public News- haya ni matukio ya kihabari yanayotokea bila kupanga, ajali, ujambazi, wizi, ugojwa wa milipuko, media iko free kuripoti hakuna mwaliko wala hakuna wa kukuzuia.
3. Private Public Events - ni public events ambazo ni private, media ni lazima ualikwe kama press conference, uzinduzi, mikutano, semina, warsha na makongamano. Mhusika wa event ndie anajua anataka vyombo gani na kuvialika na anaweza kuwaandalia bahasha za lunch au transport, hivyo ukija mtu usioalikwa, usije kuharibu budget unaweza kuzuiwa. Na pia kwa vile media ni nyingi, media zikizidi zinageuka kero, na ukiwalipa wengine na wengine huwalipi inakuwa zogo!.
4. Making your own beat- hizi ni habari ambazo mwandishi anatafuta mwenyewe bila kualikwa na yeyote lakini lazima aombe access kuzipata.
5. IJ. Hizi ni habari za uchunguzi, mwandishi/chombo cha habari lazima kitumie mbinu kuzipata, usually scandals na wahusika pia hutumia mbinu kuzifukia au kuzizuia na ndio hapa maisha ya waandishi huwa mashakani!. Hakuna kualikwa na ikibidi hakuna kujulikana.
Au wakati mwingine anapofika mwandishi wa habari anaulizwa wewe ni wa chombo gani? Anapotaja chombo chake anaambiwa kwamba wewe sijakualika ni nani aliyekupa taarifa?
Yes kwenye kutafuta habari ziko habari za kujiandikia tuu na nyingine ni lazima ualikwe na sio kuvamia matukio ya watu.
Hali hii sasa imesababisha hata Waandishi wa Habari wenyewe kwa wenyewe kushindwa kupeana taarifa zinazotokea kwenye maeneo yao kwa kuhofia kuulizwa na wadau wao waliowaalika kwa nini wameongeza watu wengine ambao hawako kwenye orodha.
Waandishi wote tunaushirikiano kwenye kupashana habari, lakini kwa matukio ya mialiko hupaswi kumjulisha asiyealikwa, ila akikosa habari, we usually share free of charge.
Pamoja na yote wakati mwingine wapo baadhi ya waandishi ambao hata wakipewa nafasi ya kuchukua matukio na wanajua fika hawako kwenye orodha ya malipo wamekuwa ving'ang'anizi kuwasumbua wadau kuwapatia pesa kilazima akijua fika hayuko kwenye orodha.
This is wrong, ukijijua hujaalikwa usilazimishe kujialika na kama ni public events, hata kama hujaalikwa lakini habari hiyo ni muhimu kwako then just cover na usidai nauli!.
Haya tumeisha fundisha sana humu
P
 
Kwanza ni kweli.
Jambo la kwanza ni habari ni bure, dunia nzima!. Mwandishi wa habari/chombo cha habari ni jukumu lake kutafuta habari na kutangaza habari bure.

Kwenye uandishi wa habari kuna matukio ya aina 3
1. Public, Public events - haya ni matukio ya kawaida ya public kama sherehe za kitaifa, polisi, hospital, mahakamani, mwandishi yoyote wa habari au chombo chochote kiko free ku cover bila kualikwa na yeyote na hutaulizwa lolote na hutazuiwa na yeyote.
2. Public News- haya ni matukio ya kihabari yanayotokea bila kupanga, ajali, ujambazi, wizi, ugojwa wa milipuko, media iko free kuripoti hakuna mwaliko wala hakuna wa kukuzuia.
3. Private Public Events - ni public events ambazo ni private, media ni lazima ualikwe kama press conference, uzinduzi, mikutano, semina, warsha na makongamano. Mhusika wa event ndie anajua anataka vyombo gani na kuvialika na anaweza kuwaandalia bahasha za lunch au transport, hivyo ukija mtu usioalikwa, usije kuharibu budget unaweza kuzuiwa. Na pia kwa vile media ni nyingi, media zikizidi zinageuka kero, na ukiwalipa wengine na wengine huwalipi inakuwa zogo!.
4. Making your own beat- hizi ni habari ambazo mwandishi anatafuta mwenyewe bila kualikwa na yeyote lakini lazima aombe access kuzipata.
5. IJ. Hizi ni habari za uchunguzi, mwandishi/chombo cha habari lazima kitumie mbinu kuzipata, usually scandals na wahusika pia hutumia mbinu kuzifukia au kuzizuia na ndio hapa maisha ya waandishi huwa mashakani!. Hakuna kualikwa na ikibidi hakuna kujulikana.

Yes kwenye kutafuta habari ziko habari za kujiandikia tuu na nyingine ni lazima ualikwe na sio kuvamia matukio ya watu.

Waandishi wote tunaushirikiano kwenye kupashana habari, lakini kwa matukio ya mialiko hupaswi kumjulisha asiyealikwa, ila akikosa habari, we usually share free of charge.

This is wrong, ukijijua hujaalikwa usilazimishe kujialika na kama ni public events, hata kama hujaalikwa lakini habari hiyo ni muhimu kwako then just cover na usidai nauli!.
Haya tumeisha fundisha sana humu
P
safi sana Mkuu, mimi nipo hapo Juu ni kweli kuna baadhi ya vyombo vya habari vinajulikana mrengo wao mfano uhuru akienda kwenye event ya chadema hasa labda semina ma warsha nafikiri siio rahisi wamruhusu.

ILi kujenga Heshima yako kama hujaalikwa usiende kuvamia matukio yasiyokuhusu.

Mwisho mimi naona hawa waandishi hata kama wanapewa bahasha, basi ule mwaliko kialikwe chombo cha habari kisha mhariri ndio achague mwandishi wa kwenda. kumwalika mwandishi mmoja kweny kila tukio lako saa nyingine kunaondoa ule uhuru wa kuandika na kureport
 
safi sana Mkuu, mimi nipo hapo Juu ni kweli kuna baadhi ya vyombo vya habari vinajulikana mrengo wao mfano uhuru akienda kwenye event ya chadema hasa labda semina ma warsha nafikiri siio rahisi wamruhusu.
Naunga mkono hoja
ILi kujenga Heshima yako kama hujaalikwa usiende kuvamia matukio yasiyokuhusu.
Naunga mkono hoja
Mwisho mimi naona hawa waandishi hata kama wanapewa bahasha, basi ule mwaliko kialikwe chombo cha habari kisha mhariri ndio achague mwandishi wa kwenda. kumwalika mwandishi mmoja kweny kila tukio lako saa nyingine kunaondoa ule uhuru wa kuandika na kureport
This is how it should be, mwaliko ni kwa mhariri yeye ndiye atakupangia mwandishi wa kuja.

Kwavile waandishi hawalingani uwezo, kama unamtaka mwandishi fulani specific kwasababu ana ku cover vizuri, then mset mhariri wake ampangie na sio wewe kumpangia
P
 
Binafsi naona suala la waandishi wa habari inabidi liangaliwe upya, ikiwezekana mfumo ubadilishwe (sijui kama itawezekana).
Wengiwao wanaongoza kwa kulia njaa na ujanja ujanja, hiyo ni fedhea na aibu kwa tasnia.
It's true fani imevamiwa na makanjanja!.
P
 
Kwanza ni kweli.
Jambo la kwanza ni habari ni bure, dunia nzima!. Mwandishi wa habari/chombo cha habari ni jukumu lake kutafuta habari na kutangaza habari bure.

Kwenye uandishi wa habari kuna matukio ya aina 3
1. Public, Public events - haya ni matukio ya kawaida ya public kama sherehe za kitaifa, polisi, hospital, mahakamani, mwandishi yoyote wa habari au chombo chochote kiko free ku cover bila kualikwa na yeyote na hutaulizwa lolote na hutazuiwa na yeyote.
2. Public News- haya ni matukio ya kihabari yanayotokea bila kupanga, ajali, ujambazi, wizi, ugojwa wa milipuko, media iko free kuripoti hakuna mwaliko wala hakuna wa kukuzuia.
3. Private Public Events - ni public events ambazo ni private, media ni lazima ualikwe kama press conference, uzinduzi, mikutano, semina, warsha na makongamano. Mhusika wa event ndie anajua anataka vyombo gani na kuvialika na anaweza kuwaandalia bahasha za lunch au transport, hivyo ukija mtu usioalikwa, usije kuharibu budget unaweza kuzuiwa. Na pia kwa vile media ni nyingi, media zikizidi zinageuka kero, na ukiwalipa wengine na wengine huwalipi inakuwa zogo!.
4. Making your own beat- hizi ni habari ambazo mwandishi anatafuta mwenyewe bila kualikwa na yeyote lakini lazima aombe access kuzipata.
5. IJ. Hizi ni habari za uchunguzi, mwandishi/chombo cha habari lazima kitumie mbinu kuzipata, usually scandals na wahusika pia hutumia mbinu kuzifukia au kuzizuia na ndio hapa maisha ya waandishi huwa mashakani!. Hakuna kualikwa na ikibidi hakuna kujulikana.

Yes kwenye kutafuta habari ziko habari za kujiandikia tuu na nyingine ni lazima ualikwe na sio kuvamia matukio ya watu.

Waandishi wote tunaushirikiano kwenye kupashana habari, lakini kwa matukio ya mialiko hupaswi kumjulisha asiyealikwa, ila akikosa habari, we usually share free of charge.

This is wrong, ukijijua hujaalikwa usilazimishe kujialika na kama ni public events, hata kama hujaalikwa lakini habari hiyo ni muhimu kwako then just cover na usidai nauli!.
Haya tumeisha fundisha sana humu
P
Asantee mkuu
 
Hii tabia ipo sana Kwenye mkoa wa Kilimanjaro na Arusha kule waanahabri wao kwa wao wanajuana na wale maafisa habri wana watu wao wakienda wageni wanateseka sana lazima wakuzuie. wenye raha ni wale wa magazeti na radio wao wakifika wanakaa tu na diary na voice recorder wanatulia kama wageni kumbe wapo kazini.

Changamoto inakuwa kwa wale wenye macamera tu.

Mimi ningekuwa mwandishi ningeenda popote kwenye matukio ya wazi na usingenifanya kitu, labdavikao tu ndio ningeomba ruhusa
Mwandishi wa habari ana haki ya kukuchukua tukio lolote ni vile tu ukata wa maisha un
 
Kwanza ni kweli.
Jambo la kwanza ni habari ni bure, dunia nzima!. Mwandishi wa habari/chombo cha habari ni jukumu lake kutafuta habari na kutangaza habari bure.

Kwenye uandishi wa habari kuna matukio ya aina 3
1. Public, Public events - haya ni matukio ya kawaida ya public kama sherehe za kitaifa, polisi, hospital, mahakamani, mwandishi yoyote wa habari au chombo chochote kiko free ku cover bila kualikwa na yeyote na hutaulizwa lolote na hutazuiwa na yeyote.
2. Public News- haya ni matukio ya kihabari yanayotokea bila kupanga, ajali, ujambazi, wizi, ugojwa wa milipuko, media iko free kuripoti hakuna mwaliko wala hakuna wa kukuzuia.
3. Private Public Events - ni public events ambazo ni private, media ni lazima ualikwe kama press conference, uzinduzi, mikutano, semina, warsha na makongamano. Mhusika wa event ndie anajua anataka vyombo gani na kuvialika na anaweza kuwaandalia bahasha za lunch au transport, hivyo ukija mtu usioalikwa, usije kuharibu budget unaweza kuzuiwa. Na pia kwa vile media ni nyingi, media zikizidi zinageuka kero, na ukiwalipa wengine na wengine huwalipi inakuwa zogo!.
4. Making your own beat- hizi ni habari ambazo mwandishi anatafuta mwenyewe bila kualikwa na yeyote lakini lazima aombe access kuzipata.
5. IJ. Hizi ni habari za uchunguzi, mwandishi/chombo cha habari lazima kitumie mbinu kuzipata, usually scandals na wahusika pia hutumia mbinu kuzifukia au kuzizuia na ndio hapa maisha ya waandishi huwa mashakani!. Hakuna kualikwa na ikibidi hakuna kujulikana.

Yes kwenye kutafuta habari ziko habari za kujiandikia tuu na nyingine ni lazima ualikwe na sio kuvamia matukio ya watu.

Waandishi wote tunaushirikiano kwenye kupashana habari, lakini kwa matukio ya mialiko hupaswi kumjulisha asiyealikwa, ila akikosa habari, we usually share free of charge.

This is wrong, ukijijua hujaalikwa usilazimishe kujialika na kama ni public events, hata kama hujaalikwa lakini habari hiyo ni muhimu kwako then just cover na usidai nauli!.
Haya tumeisha fundisha sana humu
P
MEI 3 ya kila mwaka ni Siku ya Kimataifa ya Uhuru wa vyombo vya habari, Mimi Pascal Mayalla, kwa niaba yangu kama mwanahabari ambaye ni mwandishi wa habari huru na wa kujitegemea kwa kujitolea na kwa niaba ya kampuni yangu ya PPR as chombo huru cha habari, niwatakie wanahabari wenzangu wote, maadhimisho mema ya siku hii, huku nikidurusu, niliwahi kusema nini kuhusu uhuru wa habari kwa media zetu za Tanzania yetu.

Nawatakia maadhimisho mema ya siku yetu hii ya leo na uhuru wa habari mwema.
Paskali.
 
Back
Top Bottom