Lushoto: Irente view point hotel, Mazinde Juu,Magamba na Nyumba ya Mkapa

Mkuu Mndundu,
Nimekumbuka kitu kingine muhimu sana nilichokiona miaka hiyo ya 70 huko Lushoto.
Ilikuwa ikifika jioni, ilikuwa ni raha kuona magari ya mashindano yakipita kwa speed kali sana na yakiwa machafu si kawaida. Nilikuwa nashangaa hasa nikiyaona mchana, kwa nini yana taa nyingi namna hiyo. Baadaye nilipokuja yaona jioni yakipita ndipo nikajua. Unakuta taa zote zimewashwa na anakokwenda dereva inakuwa kuna mwanga mkubwa na wa kutosha.
Kama sikosei ilikuwa ni East African Safari Rally. Ni bahati mbaya sana haya mashindano yalikufa maana ilikuwa ni tangazo la nchi muhimu sana. Baadaye Wakenya walibaki peke yao na kama sikosei na wao sasa wameondolewa. Too sad.
 
Thanks for the pics, the Mkapa house is rather modest from what I expected.

Kuna mijengo ova Bavaria vile.Huku ndiko mijerumani ilikaa nini?
 
Mkuu Mndundu,
Nimekumbuka kitu kingine muhimu sana nilichokiona miaka hiyo ya 70 huko Lushoto.
Ilikuwa ikifika jioni, ilikuwa ni raha kuona magari ya mashindano yakipita kwa speed kali sana na yakiwa machafu si kawaida. Nilikuwa nashangaa hasa nikiyaona mchana, kwa nini yana taa nyingi namna hiyo. Baadaye nilipokuja yaona jioni yakipita ndipo nikajua. Unakuta taa zote zimewashwa na anakokwenda dereva inakuwa kuna mwanga mkubwa na wa kutosha.
Kama sikosei ilikuwa ni East African Safari Rally. Ni bahati mbaya sana haya mashindano yalikufa maana ilikuwa ni tangazo la nchi muhimu sana. Baadaye Wakenya walibaki peke yao na kama sikosei na wao sasa wameondolewa. Too sad.

...si mambo ya siasa za ujamaa hayo,...kuvunjika kwa jumuia ya africa mashariki na fuel crunch ilipelekea Tanzania kuyafungia mashindano hayo katika ardhi yake, ikatukosesha sie wengine bahati ya kuwaona kina Bert Shankland na Zully Rhemtulla pale Kilimanjaro hotel enzi hizo...
 
Thanks for the pics, the Mkapa house is rather modest from what I expected.

Kuna mijengo ova Bavaria vile.Huku ndiko mijerumani ilikaa nini?

...Mjerumani alipapenda, kaacha kumbukumbu nyingi tu ya majengo yake, likiwemo kanisa na post office. Kuzuri sana huko mkuu. Nilitembelea mitaa hiyo hivi karibuni... kunafaa kujenga nyumba ya kustaafu huko, ...hewa saaaafi kabisa...

3rd-5th October 2008 (69).JPG
3rd-5th October 2008 (83).JPG
 
Mkuu Mndundu tunashukuru kwa picha......Lushoto kuzuri sana

Hamna noma mkuu nilikuwa huko kwa likizo ya kama siku tatu hivi kwa kweli ni kuzuri sana na kuna matunda mengi.
 
Hamna noma mkuu nilikuwa huko kwa likizo ya kama siku tatu hivi kwa kweli ni kuzuri sana na kuna matunda mengi.

Mkuu hukufanya kuulizia huko plot zinakuwa bei gani.....walau Low density plot......?
 
Kwa mnaopajua vizuri Irente, hivi kile kituo cha watoto yatima bado kipo?

Nilipita Irente mwezi Machi, 2008. Dereva niliyekuwa naye akanionyesha kituo cha watoto yatima pale Irente. Kituo kipo na kinafanya kazi.
 
Mkuu hukufanya kuulizia huko plot zinakuwa bei gani.....walau Low density plot......?

Niliulizia mzee, nilikutana na kijana mmoja anayesoma chuo cha mahakama pale lushoto ambaye wakati wa likizo huwa anafanya kazi kama tour guide. Kwa maeneo niliyoulizia (nje ya mji kidogo) alisema kuanzia laki 6 hadi mil 1 unapata kiwanja kizuri. Lakini nadhani hivyo vitakuwa havijapimwa....

Hii ndio nyumba yake aliyojenga.
 

Attachments

  • nyumba.JPG
    nyumba.JPG
    816.2 KB · Views: 227
ni kweli ndo maana pale mwanzoni mwa hekaheka za uchaguzi mkuu wa 2005 watu waliokuwa wakisemekana kuwa ni machaguo ya mkapa kugombea urais na ngwilizi alikuwemo kutokana na uswahiba wao. Mtu mmoja alituambia tulipokuwa lushoto kuwa hicho kiwanja alichojenga mkapa aliporwa mwananchi mmoja na akaambiwa asithubutu kupiga kelele. Sasa sijui kama ilikuwa hivyo kweli au watu waliongeza chumvi.

sio kweli ni vema kama jambo hulijui ukanyamaza na sio kuongea kwa kuhisi, ni kweli mkapa na ngwilizi ni maswahiba saana na yeye ndio alichangia mpaka mkapa akajenga huko,,historia ya hicho kiwanja kuna mkandarasi nadhani alikuwa mzungu alipewa dili la kujenga barabara hiyo ilikuwa ni site yake jamaa alijenga hapo nyumba nzuri tu za wahandisi wake na yeye mwenyewe alikuwa anaishi hapo, alipomaliza ujenzi zile nyumba zilikuwa zikabidhiwe wilaya, gwiliza kama unakumbuka ndo alikuwa boss wa tamisemi ndo akampa mzee,

kiwanja hakunyanganywa mtu kama unavyojaribu kueleza hapa
 
Majizi tu hayo yanazani yataishi milele kwenye hayo ma palace,angekua wa maana angejenga huko kwao umakondeni,kawadharau wamakonde akaona mjengo kama huo haustahili kua kule.
 
Mmmenikumbusha sana the where I belong, Lushoto ni Nyumbani kwa kuishi, tulihamia Lushoto, ingawa nina muda mrefu sana sijaenda home where my Dady's tomb is! Well, nilishatafutiwa plot japo sikuipenda sana, Ipo jirani na Montesory - Usambara Sisters, kama kuna mtu ataihitaji, naweza muunganisha na ndugu zangu, just PM me!
 
Magamba Secondary School ya enzi hizo na Mazinde Juu Secondary

Nimesoma Magamba baada ya kuhamia nikitokea Shambalai Sec, nawakumbuka walimu wangu akina Madiga naskia amekua afisa elimu japo sijui ni wapi!
 
sio kweli ni vema kama jambo hulijui ukanyamaza na sio kuongea kwa kuhisi, ni kweli mkapa na ngwilizi ni maswahiba saana na yeye ndio alichangia mpaka mkapa akajenga huko,,historia ya hicho kiwanja kuna mkandarasi nadhani alikuwa mzungu alipewa dili la kujenga barabara hiyo ilikuwa ni site yake jamaa alijenga hapo nyumba nzuri tu za wahandisi wake na yeye mwenyewe alikuwa anaishi hapo, alipomaliza ujenzi zile nyumba zilikuwa zikabidhiwe wilaya, gwiliza kama unakumbuka ndo alikuwa boss wa tamisemi ndo akampa mzee,

kiwanja hakunyanganywa mtu kama unavyojaribu kueleza hapa
thanks prodigal son... je kabla ya engineer hakulizwa mtu hapo??
 
Kwa mnaopajua vizuri Irente, hivi kile kituo cha watoto yatima bado kipo?

Bado kipo na kinaendelea vizuri na sasa kumeanzishwa shule ya watoto wenye mtindio, unaweza ku-google: Irente Outreach Program
 
kile kituo bado kipo ila siku hizi kiko hoi taabani. si unajua siku hizi huduma za jamii siyo dili tena? kinaendelea kusuasua. Kuna wakati nilikwenda Lushoto nikakaa hapo Irente, mwenyeji wangu mmoja ( nadhani katika kunisimanga kwa nini nini nilikataa kukaa Kialiro) akaamua kunipitisha hapo. Nilichokikuta hapo kilinifanya nibadili mawazo na kuwaachia hao watoto hapo sehemu kubwa ya rent kesho yake nikarudi kukaa Kialiro.
 
Wow! nimekumbuka mbali sana, nilizaliwa lushoto, nimekulia huko, nimesoma mazinde juu, though familia yetu ilihama miaka ya 1998, nakumbuka jegestal, Majirani zetu wakina Kusaga, Frank Humplick, Mbelwa, Said Matagi, na wengine wengi. Nakumbuka matunda mazuri ambayo hayapatikani kwingineko kama sambia, kadamia, mavilu, apples, mafyoksi, mapeasi. Kweli mmenikumbusha mbali sana.
 
Back
Top Bottom