Je, Aga Khan Sea View, ni kwa wahindi, wabunge, mawaziri na viongozi wa juu wa Serikali tu?

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Jan 26, 2013
18,673
22,264
Katikati ya mwaka huu yaani 2023 mwezi wa sita nilikwenda hospitali ya Aga Khan iliyopo Sea View Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu, kama taratibu zilivyo niliwasilisha kadi yangu ya bima ya afya ilipokelewa na nikapewa jibu kuwa siwezi kutibiwa kwenye hospitali hiyo!

Haikuwa shida kwangu, nikaenda hospitali ya Shree Hindu Mandal iliyopo Upanga na nikapata tiba kwa kutumia kadi hiyohiyo.

Mwezi huu wa kumi nilienda kwenye tawi la hospitali ya Aga Khan lililopo uswahilini na nikisema uswahilini ni uswahilini kweli kwani madakitari, manesi na wafanyakazi wengine ni waswahili wenyewe wanakiri wahindi wa uzao wa Aga Khan hawakanyagi huku uswazi!

Baada ya kupata tiba kwenye hilo tawi letu la hospitali ya Aga Khan nikamuuliza dakitari kuhusu hospitali mama ya Sea View, naye hakusita kuniambia kuwa kule ni kwa wahindi, wabunge, mawaziri na viongozi wa juu wa serikali, nikajua kuwa ukiwapendelea hawa basi jambo lako litakwenda vizuri bila kuhojiwa.

Miaka iliyopita tulikuwa tukitibiwa bila tatizo kwenye hospitali hiyo ya Aga Khan Sea View licha ya tatizo la hawa wazalendo watanzania wenzetu kutokujua kiswahili vizuri, lakini walipoona tunawabana wakatufungulia matawi uswazi na madakitari wetu wakiswazi tumaliziane huku huku.
 
Katikati ya mwaka huu yaani 2023 mwezi wa sita nilikwenda hospitali ya Aga Khan iliyopo Sea View Dar es Salaam kwa ajili ya matibabu, kama taratibu zilivyo niliwasilisha kadi yangu ya bima ya afya ilipokelewa na nikapewa jibu kuwa siwezi kutibiwa kwenye hospitali hiyo! Haikuwa shida kwangu, nikaenda hospitali ya Shree Hindu Mandal iliyopo Upanga na lakini walipoona tunawabana wakatufungulia matawi uswazi na madakitari wetu wakiswazi tumaliziane huku huku.

Mimi ni mswahili raia wa kawaida tu nina kawaida ya kuwaplka watoto wa dada yangu wana NHIF fast track na sijawahi kuridshwa nao wala kubaguliwa kwa lolote bima yako pengine bima yako haikidhi matibabu ya hapo
 
Yawezekana ni gharama sana,ungehoji vema.Mbona mimi rafiki yangu alilazwa Agakhan,na akahudumiwa vema,alifanyiwa major operation na tunawashukuru kwa kuokoa maisha yake,japo ni ghali sana gharama zao.Ungewahoji vema.Mfano, yawezekana baadhi ya bima,hazikubaliwi pale,kama ulikua na bima.Anyway,pole sana kwa hiyo adha uliyoipata.
 
Yawezekana ni gharama sana,ungehoji vema.Mbona mimi rafiki yangu alilazwa Agakhan,na akihudumiwa vema,alifanyiwa major operation na tunawashukuru kwa kuokoa maisha yake,japo ni ghali sana gharama zao.Ungewahoji vema.Mfano, yawezekana baadhi ya bima,hazikubaliwi pale,kama ulikua na bima.Anyway,pole sana kwa hiyo adha uliyoipata.
Lipo tawi lao uswazi natibiwa hapo kwa bima ileile, pia Hindu Mandal huwa hakuna shida nayo ni hospitali kubwa.
 
Hivi vijijiji wanaishi vipi? mbona wana afya njema na hakuna hizo Aga khan?
Mkuu usiseme hivyo,watu kwasababu ya kutofanya check up, yawezekana kwasababu ya kutokua na pesa au bima za afya,unakuta mteja anapelekwa hospitali akiwa katika hatua mbaya,au wengine unakuta anadondoka tu,anakufa kumbe alikua mgonjwa muda mrefu,anajikaza anakunywa Panadol.Kuna mama amefariki juzi,yaani aliugua ghafla,akakimbizwa hospitali,sikuamini nilipokuja kuambiwa amefariki,ilikua ghafla sana,kuuliza wadau wakajibu kua alikutwa maini yameharibika pamoja na figo pia,nikasikitika sana.
 
Yawezekana ni gharama sana,ungehoji vema.Mbona mimi rafiki yangu alilazwa Agakhan,na akihudumiwa vema,alifanyiwa major operation na tunawashukuru kwa kuokoa maisha yake,japo ni ghali sana gharama zao.Ungewahoji vema.Mfano, yawezekana baadhi ya bima,hazikubaliwi pale,kama ulikua na bima.Anyway,pole sana kwa hiyo adha uliyoipata.

Ukienda na cash au Bima inayokubaliwa hakuna mtu anakurudsha hapo
 
Hata wewe na mleta mada wabaguzi wakubwa nyie.Waswahil8 wengi wamefu gua hospital kubwa tu za binafsi hamuendi mumekomaa kwenda kutibiwa hospitalli.za wahindi

Wabaguzi nyie
Nimewahi kwenda hospitali ya Mwananyamala mapokezi nililipa 30,000/= na mambo mengine mengi ambayo hayaeleweki kabla ya mgonjwa kulazwa nilikuwa nimekwisha lipa zaidi ya 80,000/=, na lia daktari akimuona anaandika dawa za kununua!
 
Mkuu usiseme hivyo,watu kwasababu ya kutofanya check up, yawezekana kwasababu ya kutokua na pesa au bima za afya,unakuta mteja anapelekwa hospitali akiwa katika hatua mbaya,au wengine unakuta anadondoka tu,anakufa kumbe alikua mgonjwa muda mrefu,anajikaza anakunywa Panadol.Kuna mama amefariki juzi,yaani aliugua ghafla,akakimbizwa hospitali,sikuamini nilipokuja kuambiwa amefariki,ilikua ghafla sana,kuuliza wadau wakajibu kua alikutwa maini yameharibika pamoja na figo pia,nikasikitika sana.
Ni kweli, watu tunaogopa kufanya check up unaweza kukutwa na gonjwa kubwa huwezi kulitibu ukaishia kuishi kwa stress maisha yako yote
 
Back
Top Bottom