benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Jeshi la Polisi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu, limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa 26 na kufikishwa mahakamani Oktoba 26, 2023 katika Mahakama ya Wilaya ya Lushoto mkoani Tanga wakikabiliwa na tuhuma mbalimbali zikiwepo; unyang'anyi wa kutumia nguvu na shambulio la kudhuru mili dhidi ya Dagmara Anna Ikiert.
Watuhumiwa hao walikamatwa kutokana na tuhuma za kuingia katika Hoteli ya Mambo View iliyopo katika kiji cha Mambo, Kata ya Sunga Tarafa ya Mtae Wilaya ya Lushoto, moani Tanga Oktoba 23, 2023 na kudaiwa kufanya uhalifu mbalimbali.
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na taasisi nyingine wanaendelea kukamilisha ukusanyaji wa ushahidi ambao unahitaji chunguzi zaidi ili kesi hiyo iweze kwenda katika hatua inayotakiwa.
Hivyo, Jeshi Jeshi la Polisi linatoa wito kwa mwenye ushahidi mwingine wa ukweli asisite kuufikisha Polisi ili uweze kufanyiwa kazi.
Aidha kwa yeyote yule atakayebainika kuhusika kwa namna yeyote ile au kwa kupanga, kuhamasisha, kutoa taarifa za uwongo au kufadhili, Jeshi la Polisi halitasita kumkamata na kumfikisha mahakamani.
Watuhumiwa hao walikamatwa kutokana na tuhuma za kuingia katika Hoteli ya Mambo View iliyopo katika kiji cha Mambo, Kata ya Sunga Tarafa ya Mtae Wilaya ya Lushoto, moani Tanga Oktoba 23, 2023 na kudaiwa kufanya uhalifu mbalimbali.
Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na taasisi nyingine wanaendelea kukamilisha ukusanyaji wa ushahidi ambao unahitaji chunguzi zaidi ili kesi hiyo iweze kwenda katika hatua inayotakiwa.
Hivyo, Jeshi Jeshi la Polisi linatoa wito kwa mwenye ushahidi mwingine wa ukweli asisite kuufikisha Polisi ili uweze kufanyiwa kazi.
Aidha kwa yeyote yule atakayebainika kuhusika kwa namna yeyote ile au kwa kupanga, kuhamasisha, kutoa taarifa za uwongo au kufadhili, Jeshi la Polisi halitasita kumkamata na kumfikisha mahakamani.