Salaam, shalom!!
Hapo bungeni, mpo Kwa ajili ya wananchi.
LUGHA YA WANANCHI.
Wananchi tunataka kuona wabadhirifu walioiba pesa za umma, walioguswa na Ripoti ya CAG , wananchi tunataka watu hao wafungwe wote, na pesa yetu irudi. Wakamuliwe Hadi sent ya mwisho, Mali zao ziuzwe pesa irudi.
LUGHA YA WANASIASA.
Zimesikika sauti ndani ya nyumba Ile "Vunja Barazaaa"!!! Ni kama hawajui wapi Hasa lilipo tatizo.
Wengine wamekaa Mahali wanachanga karata zao, wanaotumia mwanya wa ubadhirifu uliotokea kutaka kupita na koti la kaka mkubwa ,kiranja mkuu wakiamini tutahadaika na kuona wamechukua hatua stahiki.
Kaka mkubwa Hana mkono mrefu maskini wa watu, Eti wale wale waliozipiga, Wanataka tena Yeye Abebe lawama za wizi wao.
HATUDANGANYIKI 😳
Tumeshajifunza nini kilitokea Awamu ya nne, Mzee wetu aliondolewa na pesa zetu hazikurudi.
Ikiwa pesa za umma zinaibwa, na pesa zenyewe ni za MKOPO ,sisi wananchi tupate wapi pesa za kurudi kulipa mkopo na riba wakati pesa zetu hazikufanya KAZI yoyote zaidi ya kuibwa?
Nani wa kumfunga paka kengele?
Tukutane kwenye Sanduku la kura baada ya Kupata kwanza Tume huru ya Uchaguzi na KATIBA mpya.
NB: Mungu aliyemsaidia Majaliwa kuokoa majeruhi wa Ajali ya ndege Mwanza, ndiye huyo atamsaidia kiranja mkuu kuepuka zengwe mbele yake.
Karibuni 🙏
Elli
Hapo bungeni, mpo Kwa ajili ya wananchi.
LUGHA YA WANANCHI.
Wananchi tunataka kuona wabadhirifu walioiba pesa za umma, walioguswa na Ripoti ya CAG , wananchi tunataka watu hao wafungwe wote, na pesa yetu irudi. Wakamuliwe Hadi sent ya mwisho, Mali zao ziuzwe pesa irudi.
LUGHA YA WANASIASA.
Zimesikika sauti ndani ya nyumba Ile "Vunja Barazaaa"!!! Ni kama hawajui wapi Hasa lilipo tatizo.
Wengine wamekaa Mahali wanachanga karata zao, wanaotumia mwanya wa ubadhirifu uliotokea kutaka kupita na koti la kaka mkubwa ,kiranja mkuu wakiamini tutahadaika na kuona wamechukua hatua stahiki.
Kaka mkubwa Hana mkono mrefu maskini wa watu, Eti wale wale waliozipiga, Wanataka tena Yeye Abebe lawama za wizi wao.
HATUDANGANYIKI 😳
Tumeshajifunza nini kilitokea Awamu ya nne, Mzee wetu aliondolewa na pesa zetu hazikurudi.
Ikiwa pesa za umma zinaibwa, na pesa zenyewe ni za MKOPO ,sisi wananchi tupate wapi pesa za kurudi kulipa mkopo na riba wakati pesa zetu hazikufanya KAZI yoyote zaidi ya kuibwa?
Nani wa kumfunga paka kengele?
Tukutane kwenye Sanduku la kura baada ya Kupata kwanza Tume huru ya Uchaguzi na KATIBA mpya.
NB: Mungu aliyemsaidia Majaliwa kuokoa majeruhi wa Ajali ya ndege Mwanza, ndiye huyo atamsaidia kiranja mkuu kuepuka zengwe mbele yake.
Karibuni 🙏
Elli