Ludovick Joseph akamatwa na Polisi...

Ludovick Joseph akamatwa na Polisi...

Chadema wameshikwa abaya sana this time!
embu elezea manake nini chadema inaweza kushikwa pabaya enzi hizi enzi za MACCM zilishaisha wamebaki kupopolewa mawe kuna mahali Raisi inabidi aombe ruhusa kwa wenyewe ndio akanyage ardhi ya huko
 
Ebu tuambie mkuu labda imewakaba koo secta gani!!!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
na hii nawaletea

Haya status chache za Joseph mmoja zipo hivi
zote hizi zinaonekana na public as hazijawekewa privacy so msidhani ni rafiki fb kaiba huko.


14Aug2012
MACCM Yameanza mbio za uongozi.kaeni mikao ya kula.unaweza kustukia unaitwa na kuambiwa ukafuturishwe na mtu ambaye hata ramadhani hajui maana yake nini

21Dec2012
NDIYO LEMA kashinda na picha kaweka

30Dec2012
niko iringa,nimetua jana usiku kutokea dar,nina kikao cha kazi.naweza kurejea dar leo usiku au kesho kwa ajili ya kufunga mwaka

04Jan2013
Niko Iringa usiku huu
hapa mtu akakomenti "upo juuuuuuuuuuuuuu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!1 kama mafia hv"
akajibu " weweee!!! shhhhh"

31Jan2013
HAPA KAWEKA MANENO HAYA NA PICHA YENYE CHAKULA KITAMU CHA KUVUTIA NDIZI ZA KIHAYA
"
Walaaniwe wafedheheshwe,wanaodhuru nafsi yangu..warudishwe nyuma..waaibishwe,warudishwe nyuma nyuma ,waaibishwe!!!!"

10Feb2013
Hii ikiwa na picha ya Dr.Slaa akihutubia
"Rais Dr.Slaa anahutubia sasa.watu wanamuita hivyo hapa.ndipo hapa orodha ya mafisadi ilianzia.Kikwete akiwa namba moja.Godbless Lema ametoa namba ya spika makinda 07544*****,na namba ya Ndugai 07626***** (mie nimeondoa namba)kwa wananchi ili kila mara na kila siku watu wampigie simu na kumwambia aachie uspika.waandike meseji na kusema hivyohivyo hadi hawa madudu watoke.hakuna atakayefatilia namba zenu."

huku kwenye like amelike mUVCCM mmoja na rafiki yake mmoja wa fb ni mwigulu nchemba

06Mar2013
NIMETEKWA LEO USIKU.
Ndugu,leo usiku yapata saa tano na nusu niliachana na Maggid Mjengwa maeneo ya Shekilango tukitokea Rose Garden.yeye alielekea hotelini alikofikia,sehemu fulani kariakoo,nami nikasubiri kigari kuelekea nyumbani kwangu.hapo shekilango,magari yalichelewa kidogo,pembeni ilipaki bajaji ikiwa na watu 2 na dereva.ndipo wakaniambia twende tuchangie mia tano tu kwenda ubungo mataa.nikakaa katikati ya hao jamaa.
Ghafla wakakata kona na kuanza kuelekea mabibo na wakiulizana kama wako kamili,na mwingine kujibu yuko kamili.nikajua tayari niko mikononi mwa majambazi na sikujua wako kamili namna gani,kwa hiyo nikaamua kuwa mtulivu.Tulipofika relini karibu na mabibo,wakanipokonya begi lakini hawakulifungua.( ndani yake kulikuwa na laptop,toshiba kubwa,na chaja yake,kamera ndogo ya digital na USB yake,modem ya zantel na card reader.).tulipofika maeneo ya loyola sekondari nikawasihi wanishushe ili nirudi mwenyewe,wakaniambia safari ile inaishia jangwani.nikaingiwa na wasiwasi mkubwa na nia yao hasa.maana wameshanipokonya begi,kwa nini wasiniachie? lakini niliendelea kuwa mtulivu ili kutowa provoke.
Tulipovuka kigogo mwisho kwenye giza karibu na msikiti,wakasimama pembeni ya barabara na kuniamuru kushuka.nikashuka na kuanza kuwadai begi langu.ndipo mmoja akasema wamekuwa wastaarabu mimi naanza kuwadharau.Ghafla akanivuta kwa nguvu kunirudisha kwenye kibajaji,akamwambia mwenziye wanisachi kama nina vitu vingine.wakanisachi na kuchukua pesa (nilikuwa na elfu 35) na simu mbili ndogo za nokia.moja yenye line mbili.kisha mmoja akatoa order nivuliwe nguo.Nikavuliwa viatu,T shirt na suruali.nikabaki na nguo za ndani pekee.wakanishusha na kuniacha hapo.
Kurudi nyuma kama hatua kumi tu ndipo kituo kidogo cha polisi Kigogo.nikaanza kutoa maelezo hapo kwa zaidi kama ya saa 2 nikiwa uchi na nguo za ndani tu.Nikiwa hapo nikasikia polisi wakiwasiliana juu ya tikio la kupigwa vibaya ABSALOM KIBANDA kwenye redio calls.ilikuwa yapata saa nane.baada ya kuchukuliwa maelezo,polisi walinipatia gari nikaelekea hotelini kwa Maggid,ambaye saa kumi aliamshwa na kunichukulia chumba hapo nikapumzika.ameniazima nguo zake ndizo nimevaa bado hadi sasa.naelekea kituo cha polisi Magomeni kwenda kupewa mpelelezi wa kesi yangu.namba ya case yangu kigogo ni KIG/RB/318/2013 (WIZI KUTOKA MAUNGONI).
Namshukuru Mungu hawajanijeruhi wala kunipiga.namshukuru Maggid kwa msaada wake hadi sasa.MUNGU NI MWEMA



na yeye ni huyu hii imetokea huko kwenye mtandao alipojiandikaga kwa wenzake (yote yapo public) humo pia ameposti issue ambayo pia ameipost kwenye fb page yake alikuwa anatafuta ushauri so ndio maana nikajua ndie huyu aliyejieleza hapa chini
16/17Jan2013
Mimi naitwa Joseph Rwezahura Ludovick Mulokozi .cheti cha ubatizo
kinanitambulisha kama Rwezahura Joseph,kile cha kuzaliwa kama joseph
Ludovick,cha shule ya msingi hadi form six nimejulikana kama Joseph
Ludovick,lakini Chuo kikuu na sasa kwenye vyeti vya degree UDSM
natambulika kama Ludovick Joseph.

Bali nilisoma falsafa kwenye chuo cha kanisa,wao walitaka niandike
majina ya ukoo,huko vyeti vinaonyesha naitwa Rwezahura Mulokozi
Ludovick.Haya kwenye kusajili line za simu na kadi za benk wakataka
majina matatu.huko najulikana kama Joseph Rwezahura Ludovick na benk
Joseph Ludovick Rwezahura.sijawahi kurudia darasa acha mbali kufeli
wakati wowote ule.sasa juzi hapa nimenyimwa hela western union kwa
sababu ya mkanganyiko huu.hivi kwa mkato mimi majina yangu yanapaswa
kuwa yapi?
 
mkuu napa huamini yaliyotokea! taratibu unang'amua kuwa mna kikundi cha mafia

Halafu kwa nini unapenda sana "sisi" na "nyie"?

Kwa vile tuu kichwa chako kiko kama tikitimaji basi unadhani JF ni "yenu" na "wao" tuu?

Stop putting people into boxes. Tena ukome kabisa.
 
Chadema wameshikwa abaya sana this time!
Ccm ndo imeshikwa pabaya, wameshindwa politics wamekuja na style tofauti kabisa na siasa, nadhani walianza kuona dalili za wazi kwamba through jukwaa hawawezi kupambana na M4C so better wabadili tecnics, and yes why not, wana serikali, wana pesa nini cha kuwazuia?
lakini here me, TUTASHINDA!
 
Mwigulu, Je hii ni video ndio uliyoitaja siku ile kuwa unayo ..'' Watu tunaangalia movie kama za the ''Mentalist;; lazima tuwashike tu"' a.ka. Patrick Jane the steringi.
 
Mimi naitwa Joseph Rwezahura Ludovick Mulokozi .cheti cha ubatizo
kinanitambulisha kama Rwezahura Joseph,kile cha kuzaliwa kama joseph
Ludovick,cha shule ya msingi hadi form six nimejulikana kama Joseph
Ludovick,lakini Chuo kikuu na sasa kwenye vyeti vya degree UDSM
natambulika kama Ludovick Joseph.

Bali nilisoma falsafa kwenye chuo cha kanisa,wao walitaka niandike
majina ya ukoo,huko vyeti vinaonyesha naitwa Rwezahura Mulokozi
Ludovick.Haya kwenye kusajili line za simu na kadi za benk wakataka
majina matatu.huko najulikana kama Joseph Rwezahura Ludovick na benk
Joseph Ludovick Rwezahura.sijawahi kurudia darasa acha mbali kufeli
wakati wowote ule.sasa juzi hapa nimenyimwa hela western union kwa
sababu ya mkanganyiko huu.hivi kwa mkato mimi majina yangu yanapaswa
kuwa yapi?

Kumbe mtu mwenye CHIZI sasa hiyo STORY na kupokea HELA western union wapi na wapi?
mtu anapokutumia hela western union lazima awe anakujua!!!! isitoshe wakati wa kupeana maelezo ya siri kama
jina lililotumika lina makosa alitakiwa kumwambia mtumaji, Western union wanataka kitambulisho chenye picha na kinachokubarika,
no wonder hata video ya Lwekatare ina makosa kibao kama watu wenyewe ni hawa
 
king ilunga si mpeleke hizo video zote mlizonazo polisi ili tupate ukweli.
 
Kumbe mtu mwenye CHIZI sasa hiyo STORY na kupokea HELA western union wapi na wapi?
mtu anapokutumia hela western union lazima awe anakujua!!!! isitoshe wakati wa kupeana maelezo ya siri kama
jina lililotumika lina makosa alitakiwa kumwambia mtumaji, Western union wanataka kitambulisho chenye picha na kinachokubarika,
no wonder hata video ya Lwekatare ina makosa kibao kama watu wenyewe ni hawa

umesahau kwamba huyu ni mhaya?.
 
Kama jina la Ludovic linatajwa katika clip ambayo wengi tunahisi ni fake, je tunapataje faraja kwa kukamatwa kwa character anayetajwa kwenye fiction?
 
Hii video sio Bad lips, nimeangalia mara 4 tena, chadema waongee na Lwakatare kawauza very cheap
 
Yaani hizi siasa kweli uchwara watu watolewe sandakalawe kwa kupelekwa mabwepande, wafe bila ya sababu, watekane watoane macho and all the rest of the nonsense just to point fingers at each others (regardless who done it).

Whatever happened to mashindano ya sera, hii nchi sasa imekuwa na siasa za "Sicily, Italy". Its time wananchi waache kutoa sympathies na wasikilize sera za chama maana nao wanachangia muendelezo wa siasa za kihuni kwa kutodai haki zao na kufuata siasa za ushabiki ndio matokeo yake haya.
 
Nimekumbana na hii article ya Absalom Kibanda na sijui huyu jamaa aliyekuwa CRITIC ambaye jina lake linafanana na aliyekamatwa ndiye yeye au?. His comment is further below after kibanda article.


22/11/2012Juma Mzuri
Na Absalom Kibanda


Kwa mara nyingine tena, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeandika historia
mpya baada ya kufanya mabadiliko mazito katika safu yake ya uongozi wa
kitaifa.

Uzi wenyewe unapatikana hapahttps://groups.google.com/forum/m/#!topic/wanabidii/j0hGBGnCOEw

Wazungu wanasema Huku ndiyo kuunga dots kwa kuangalia mtazamo wake kwa Absolom Kibanda
Na hii imekaaje?

Tukio la Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom Kibanda, kutekwa, kupigwa, kung’olewa meno, kukatwa kidole na kung’olewa kucha limeanza kuhusishwa na mlengo wa kisiasa.
Taarifa kutoka sehemu mbalimbali zinahusisha tukio hilo na msimamo wa mwanahabari huyo katika siasa za kitaifa. Kibanda anahusishwa moja kwa moja kwenye mtandao wa Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, ambaye anatajwa kuwa miongoni mwa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kuwa watakiwakilisha kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.

Wanaofuatilia siasa za kitaifa wanasema kwamba uamuzi wa Kibanda wa kuhama kutoka Kampuni ya Free Media, inayomilikiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe kwenda New Habari (2006) Ltd inayomilikiwa na mfanyabiashara Rostam Aziz, umelenga kwenda kuimarisha nguvu za Lowassa. Kwa miaka mingi, Lowassa anatajwa kuwa na urafiki wa karibu mno na Rostam. Wawili hao ndiyo waliokuwa vinara wa mtandao uliomwingiza madarakani Rais Jakaya Kikwete mwaka 2005.

Kwa upande wake, JAMHURI imezungumza na Lowassa kuhusu ukaribu wake na Kibanda, na kama kweli hiyo ndiyo sababu ya mwanahabari huyo kujeruhiwa.

Lowassa amesema kwa kifupi, “Jamani, tuna ushahidi gani? Haya ni maisha ya mtu, hata wakubwa tusiwatuhumu hivyo, tuwe na ushahidi tukitaka kutoa tuhuma nzito kama hizi.”
“Kibanda wanamhusisha na kundi la [Edward] Lowassa. Wanaona Kibanda analipa nguvu kundi hilo kwa kuwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri na baadhi ya watu ndani ya vyombo hivi wanadhani kuwa Kibanda ana-set (anatengeneza) mazingira ya Lowassa kuwa rais. Hii inawaogofya wenye nia mbaya,” kilisema chanzo chetu. Mara kadhaa Kibanda ameweka wazi msimamo wake wa kumuunga mkono Lowassa, akisema anastahili kuwa rais wa Tanzania baada ya Kikwete.
Maana katika upelelezi hakuna kuacha kitu.
 
Ni kweli habari nimeipata kwenye wall post ya mjengwa ambae ni swahiba wake katika kazi lakini post hiyo haikukaa muda mrefu mjengwa akaiondoa


Usiturushe roho mkuu km ni kweli Ebu weka uthibitisho hapa stejini tuuchakate

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Huyu Manyerere anatakiwa ahojiwe na police, hii wiki ikiisha hajafanyiwa hivyo nitaanza kupata mashaka ni hii series. Jamaa anaonekana mchezo wote anaujua ameamua kuwahi kuja kupima upepo tu hapa baada ya mambo kuwa magumu kaamua kuwawahi wenzake kama alivyofanya Ben na movie yao ya masalia.
 
Huyu Manyerere anatakiwa ahojiwe na police, hii wiki ikiisha hajafanyiwa hivyo nitaanza kupata mashaka ni hii series. Jamaa anaonekana mchezo wote anaujua ameamua kuwahi kuja kupima upepo tu hapa baada ya mambo kuwa magumu kaamua kuwawahi wenzake kama alivyofanya Ben na movie yao ya masalia.

kula like mkuu japo natumia haka kasimu mchina
 
Back
Top Bottom