Lt. Gen Abrahaman Amir Shimbo kustaafu kesho

Lt. Gen Abrahaman Amir Shimbo kustaafu kesho

Hakujua kama yatamfika kama wastaafu wengine. Na asubiri 2015 kama hajajipeleka mwenyewe kota gadi.Hopeless soldier.
 
Hautapita muda mrefu tutasikia kateuliwa kuwa mwenyekiti wa board! Years of looting lakini bado atapata pension!
Atapewa ubalozi iliakatumbue jasho la watanzania vizuri....chezea Kikwete wewe
 
maadam nyumban kwake napafahamu ntaenda kumuomba hata sh 1milion kama mgao ktk kodi yangu alioiiba
 
Inakisiwa zilizowekwa Uswis ni kama Bilioni 390 ambayo haifiki hata robo ya bajeti ya Tanzania ya Trilioni 11. Fikiri tena kama ana trilioni 4 maana yake ana mara 10 ya pesa za watanzania zilizoko Uswis!! Au kwa lugha rahisi ni zaidi ya pesa zote zilizofichwa Uswis na Waafrika mashariki!!

Au labda hufahamu tofauti ya Trilioni na Bilioni.......Tuanzie hapo!
??

Unajua % zilizo patikana kwenye ununuzi wa zile Ndege zinazo tumia marubani 5, Tracks, Tanks, Guns, Allowance za Maaskali, Maduka ambayo hayalipi kodi wakati bei za vitu ni kama za posta-Kwa ujumla unalijua Jeshi wewe?
 
"ukiyaona ya Musa utastaajabu ya firauni"

Karibu MBWENI JKT kwenye Jumba lako la kifahari Jirani na Mwamunyange Kamanda.
 
platozoom

Wewe unamtetea kwa lipi, au ni shemeji mtu? kwani hujui kuwa Shimbo yumo katika ile list ya 30 billionaires of TZ, ambaye utajiri wake unakadiriwa kuwa ni mabilioni ambayo ameyaficha uswisi, kutokana na dili alizozifanya, ikiwemo Meremeta?! Sasa tunaanza kupata picha kuwa aliamua kujikusanyia mapesa hayo ayatumie wakati wa kustaafu.

Lakini ushauri wa bure ninaompa, ni bora pesa zetu hizo akaamua kuturejeshea nchini, lakini akiamua kakaidi ushauri huu, kwa mkakati unaoandaliwa, ashishangae, badala ya kustaafu kwa amani, akajikuta anapandishwa kizimbani Kisutu!!

Ndio maana nikasema tufikirie kidogo kama ishu kama hizi zikiendeshwa kwa mihemuko tutakuwa kila siku tunakula za uso mahakamani. Hoja yangu haikuwa ameiba ama hajaiba, amehifadhi fedha au hajahifadhi. Mashaka yangu yalikuwa kwa wale waosema ni trilioni nne nikaeleza trilioni nne ni sawa na bajeti ya Wizara ya ulinzi kwa muda zaidi ya miaka 5 ambayo inazidi hata miaka aliyokaa kwenye wadhifa wake!!

Hata hayo mabilioni yaliyopo Uswis changanya na za Kenya Na Uganda hazifikii hizo trilioni 4! Au labda tueleze wewe Zilizoko Uswis (pesa za Watanzania ni sh. ngapi).....?

Sina undugu na Shimbo zaidi ya kumuona kwenye kioo tu ila kwa hilo najaribu kufikiri as GT.
 
Unajua % zilizo patikana kwenye ununuzi wa zile Ndege zinazo tumia marubani 5, Tracks, Tanks, Guns, Allowance za Maaskali, Maduka ambayo hayalipi kodi wakati bei za vitu ni kama za posta-Kwa ujumla unalijua Jeshi wewe?

Hebu tuache ubishi. Hoja haiko kaiba ama hajaiba kwangu ni hizo figures (na hilo ni muhimu,kwa sababu kosa moja inatosha kutilia shaka tuhuma) Na usisahau akina Zombe walishinda kesi kilaini kwa sababu ya makosa ya kupeleka kesi mahakamani kwa sababu ya "mhemko".

Unasema % kwenye ununuzi wa ndege za kijeshi, trucks n.k. Unafikiri fedha zote zinatoka wapi kama si wizara ya Ulinzi? Na nimesema bajeti ya Wizara yoote ya Ulinzi ya miaka 4 haijafikia hizo trilioni 4!
Na hiyo meremeta ilikomba si zaidi ya bilion 400 ambayo haifikii hata robo ya hiyo trilioni 4!! Hayo mapesa yametoka wapi?

 
we are bracing for a new chief of staff..,
as usual ntawajuza as soon as possible
 
Sijui kama kuna mtu atamkumbuka huyu jamaa kwa lolote..
 
Namwamuru kwanza arudishe zile trilion zetu alizomtunzia swaiba wake jk. hawa mafisadi hawafikishwi mahakamani, walio jela ni wezi wa kuku na wale waliobambikiwa kesi na polisi tu.
 
Ni tatizo la kitaifa ni afadhali aondoke kwanza mwizi hana uadilifu wowote.
 
Mgombe Ubunge kupitia CCM 2015 Jimbo flani stay tune........wakati akisubiri 2015 atalambishwa Umwenyekiti wa bodi flan stay tune:flypig:
 
Mnadhimu mkuu wa jeshi (chief of staff) lt. gen Shimbo ataagwa rasmi kesho.

Kamanda huyu anastaafu kwa mujibu wa sheria za jeshi za kutimiza umri wa kustaafu baada ya kuongezewa muda wa kustaafu kipindi cha nyuma japo umri wake wa kustaafu ulishafika.

Shughuli ya kumuaga itafanyika kesho makao makuu ya jeshi, Upanga.

Ikumbukwe, alipata wadhifa wa unadhimu wa jeshi mwaka 2007 ambapo yeye na CDF Davis Mwamunyange walichukua madaraka kutoka kwa general Waitara.

Nitawajuza yatakayojiri kesho kwenye shughuli ya kumuaga huyu chief of staff.

Source: MOSHE DAYAN

Pesa za askari waliokwenda comoro kalipa au anaondoka nazo kuendeleza mradi wa matrekta?
 
Mnadhimu mkuu wa jeshi (chief of staff) lt. gen Shimbo ataagwa rasmi kesho.

Kamanda huyu anastaafu kwa mujibu wa sheria za jeshi za kutimiza umri wa kustaafu baada ya kuongezewa muda wa kustaafu kipindi cha nyuma japo umri wake wa kustaafu ulishafika.

Bila shaka mtu huyu anaonekana ni muhimu sana na hakuna mtu kama yeye nchi nzima ya Tanzania.
 
Back
Top Bottom