Lowassa: Nitamtoa Babu Seya gerezani

Status
Not open for further replies.
Pia amtoe Sheikh Ponda.Lakini kwa jinsi nilovyoiona CV ya Lowassa katika Wikipedia,nadhani atawatoa watu wengi magerezani. Wewe you are shocked kusikia mtu anataka kuwaweka huru wafungwa. But we grew up listening to Malcolm X. Tunawachukia polisi na polisi wanatuchukia.

Je, si ulisoma ama kusikia na wale askari waliomuua Kombe, nao waliachiwa huru na JK kutoka gerezani kabla ya kumaliza kifungo chao? Je, wewe ni mgeni na serikali ya JK ambayo ilimwachia huru Ditopile baada ya kumwua dereva wa daladala?

Sasa kwanini kwa Lowassa akisema hivyo, sio katenda, iwe NONGWA?
 
Kama babu seya aliingizwa kwa magumashi, atatolewa kwa magumashi!

....ina maana hata baada ya kukata rufaa na kushindwa, bado kuna watu wanaamini umagumashi ktk ufidhuli wa babu seya? mbona tunakuwa tumejawa fikra za kimajungujungu...? ndivyo tunavyotegemea kwa kiwango hiki cha majungu kujenga nchi?
 
hv amekosa hoja kwel za kueleza ule umati wote na kutoa hoja isiyo ya msingi kama hii yan afadhali hata yule wa mil 50 kila kijiji na laptop kila mwl
Mkuu pengine ujue tu kwamba Lowasa anapesa hana uwezo wa kiakili na mawazo ya kufanya jambo lenye mtazamo wa kimaendeleo kwa watanzania anaweza majungu tu.
 
Nimestuka Lowassa kudharau utawala wa sheria. Babuseya alikata rufaa mahakama kuu ya Tanzania na kushindwa kwa kosa la ubakaji na udhalilishaji watoto.

Je Lowassa hautambui mhimili wa mahakama? Je utaachia wafungwa wote?

Lowassa ataleta mgongano wa kidola.

Chanzo: Raia Tanzania

Siungi mkono kauli ya Lowassa, ila kama ulifuatilia wakati kesi ikisikilizwa mahakamani kulikuwa na hila nyingi sana na minong'ono kuwa ushahidi uliotolewa kwa asilimia kubwa ulikuwa ni wa kutengeneza! hata mie sielewi ukweli halisi ila kwa mahakama zetu zilizojaa rushwa lolote linawezekana!! Ila lisemwalo lipo..
 
nikweli inawezekana kabisaaa maana hata mm ukiniuliza nitakwambia sielewi kosa la babu sea kabisaaaa
 
....ina maana hata baada ya kukata rufaa na kushindwa, bado kuna watu wanaamini umagumashi ktk ufidhuli wa babu seya? mbona tunakuwa tumejawa fikra za kimajungujungu...? ndivyo tunavyotegemea kwa kiwango hiki cha majungu kujenga nchi?

Mkuu, kwa mahakama za Tanzania zilizojaa rushwa haki kutandeka ni ndoto! Inawezekana unasema hivyo kwa sababu hujakumbwa na yatakayokufanya ukautafuta mlango wa mahakama! Masikini au myonge kupewa/kupata haki yake ni kama ngekewa!!
 
Rejea katika katiba, utaona raid amepewa mamlaka ya kuwapa msamaha wafungwa wa sina gani/ makosa yepi then ndio ucomment tena...
Nini babu seya mafisadi wote mramba,yona na yule wa Tbs atawatoa fu.ukawa mpaka sasa hawajishughulishi na ilani wapo busy kuzunguka na lowasa kutafuna mihela yake,wanategemea kushinda kwa umaarufu mgombea kitu ambacho si sahihi
 
Nimestuka Lowassa kudharau utawala wa sheria. Babuseya alikata rufaa mahakama kuu ya Tanzania na kushindwa kwa kosa la ubakaji na udhalilishaji watoto.

Je Lowassa hautambui mhimili wa mahakama? Je utaachia wafungwa wote?

Lowassa ataleta mgongano wa kidola.

Chanzo: Raia Tanzania

Ni vizuri wakati mwingine mtu unapo quote kitu kingine inabidi uchanganye akili yako ,na ya mkeo pamoja na ya baba mkwe wako kabla ya hicho kitu ulicho quote akakiweka hadharani, Magazeti ya Kitanzania kwa kuandika rubbish hayajambo sio vizuri ku quote rubbish akaanza kusambaza
 
Kila mzazi anajua uchungu wa mototo na mahangaiko anayopata mazazi katika kumlea mwanae, halafu anatokea "Mario" mwenye akili timamu anaanza kuchezea watoto wa wenzie anakamatwa anafikishwa katika vyombo vya sharia anahukumiwa anakata rufaa anashindwa nayeye anaridhika.

Halafu anatokea mtu mmoja kwa sababu anazozijua yeye anasema atamwachia huru mtu aliyepatikana na hatia ya kunajisi watoto, hapana kabisa huo upumbavu siwezi kuungana nao hata kama kwa namna gani.

Sote tunajua uchafu unaofanywa na hawa akina "Mario" sasa wanadhibitiwa mtu mmoja kwa njaa yake ya madaraka anataka kuwaachia huru, tutawatia kiberiti labda akiwaachia awarudishe makwao.

Wapo waliopatikana na hatia wakitetea haki zao, mfano fransis cheka, mbona hasemi atamwachia? wapo wanaohangaika jela kwa kutetea imani za dini yao kama sheikh Ponda na wapo walioko jela kutetea maslahi yao kama sheikh Farid hao kwake sio kitu ila huyu mbakaji tu.

Zipo NGO nyingi zi

mehangaika kutetea haki za watoto kama kuzuia ukeketaji, mimba za utotoni na haki ya elimu. Zimetumia fedha nyingi na rasilimali nyingi kupambana na matatizo ya watoto, leo mtu aliyewahi kushika nafasi za juu serikalini hili kwake sio hoja, anaona wabakaji ni watu wanaofanyiwa fitina tu, hapana.

Wakati wa sakata la Richmond bungeni, Niliwahi kumsikia mama kilango akilalamika kuletewa ki memo na chifupa kutoka kwa mheshimiwa sasa naamini hapa sio bure kwa huyu mwenzetu, tuchukue tahadhari.

Eddy wewe ñdiye Mkulu mwenyewe au unatoka katika familia ya Mkulu?Just asking!
 
Mkuu, kwa mahakama za Tanzania zilizojaa rushwa haki kutandeka ni ndoto! Inawezekana unasema hivyo kwa sababu hujakumbwa na yatakayokufanya ukautafuta mlango wa mahakama! Masikini au myonge kupewa/kupata haki yake ni kama ngekewa!!

...inawezekana mkuu hapa na pale haki ikashindwa kutendeka ktk mahakama za tanzania, na kwa kiasi kikubwa hili linatokea hata katika mahakama za nchi zilizoendelea..lakini kwa aina ya kesi ya babu seya, kama ilivyoripotiwa...tukiwasikia na kuwaona watoto waliofanyiwa vitendo vya kishenzi na babu seya..majungu, na uzushi usiokuwa hata na ushahidi , ambavyo vililenga kutuhadaa kuwa babu seya alifanyiwa mitindo aingie matatizoni vingeweza mpatia haki babu seya na wanae kwenye rufaa "zake" alizokata....kama kungekuwa na ukweli...babu seya na mwanae, mpaka upatikane ushahidi mpya utakaoonesha namna walivyofanyiwa fitna waonekane na hatia, ni wahalifu wa kiwango cha juu cha uhalifu ambao kifungo cha maisha ni astahili yao...kuwaonea huruma itakuwa ni unafki na ni kusheherekea uhalifu wao...kusheherekea unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto wadogo...watanzania pamoja na mapungufu yetu mengine yote, tuko juu sana juu ya hilo..
 
Babu Seya kasingiziwa mbona watoto walitoa ushahidi wamebakwa familia nzima waje wawatoe wawili tu. Mbona Lulu kaua kabisa kipenzi chetu Kanumba atesa uraiani.Kapuya amebaka mbona hats rumande hajafika. Papyyyyy Siku zako zakutoka zinahesabika!
 
Khaa!! Mbona ahadi nyingi bana? Amrudishe kwanza Gavana Balali ndiyo aanze kutoa ahadi nyingine. Sisi siyo watoto :mvutaji:
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom