Lowassa: Nitamtoa Babu Seya gerezani

Status
Not open for further replies.

assadsyria3

JF-Expert Member
Apr 9, 2013
6,904
4,050
Nimestuka Lowassa kudharau utawala wa sheria. Babuseya alikata rufaa mahakama kuu ya Tanzania na kushindwa kwa kosa la ubakaji na udhalilishaji watoto.

Je, Lowassa hautambui mhimili wa mahakama?

Je, utaachia wafungwa wote?

Lowassa ataleta mgongano wa kidola.

Chanzo: Raia Tanzania


Kuachiwa kwa Babu Seya ndio hitaji la watanzania?

Na Charles Charles
IPOKUWA katika ziara zake za kutafuta wadhamini 200 ili kukidhi matakwa ya kisheria, mgombea wa kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Edward Lowassa aliahidi kuingilia mpaka uhuru wa mahakama nchini.


Akihutubia katika Uwanja wa Nzovwe mjini Mbeya, Ijumaa iliyopita, Lowassa alisema moja kati ya mambo atakayoyashughulikia kwa haraka kama atashinda uchaguzi mkuu ujao, ni pamoja na kumwachilia huru Babu Seya.

Mbali na Mbeya, mgombea huyo wa urais anayeungwa mkono na vyama vyote vinavyounda kundi linalojiita Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), aliirudia tena kauli yake hiyo siku moja baadaye alipokuwa katika jiji la Arusha.

"Tukiingia madarakani tutamwachia huru Babu Seya", alisema, kauli iliyoibua mshangao mkubwa miongoni mwa watu makini waliokuwa wakimsikiliza uwanjani, na pia ikashangaza wengi waliokuja kuisoma katika gazeti moja litolewalo kila siku nchini, kesho yake.

Nguza Viking, mwanamuziki mpiga solo, mwimbaji na mtunzi ambaye ni maarufu zaidi kama Babu Seya, anatumikia kifungo cha maisha jela katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam tokea mwaka 2004.

Alitiwa hatiani na Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu, Ilala katika jiji hilo, kisha akahukumiwa kutumikia adhabu hiyo kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Kujamiiana ya Mwaka 2001.

Hata hivyo, mawakili wake wakiongozwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Mabere Marando walikata rufaa katika Mahakama Kuu ya Tanzania wakipinga hukumu hiyo kwa madai kuwa hakutendewa haki.

Katika hatua hiyo, Mahakama Kuu iliyosikiliza rufaa hiyo iliitupilia mbali, hivyo adhabu dhidi yake ikaendelea kama ilivyotolewa na Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu.

Lakini pia, mawakili wa Babu Seya bado hawakuridhika, hivyo wakakata tena rufaa katika Mahakama ya Rufani Tanzania, kule ambako ilisikilizwa na jopo la majaji watatu kama sheria inavyoelekeza.

Hata hivyo, jopo hilo nalo liliridhia hukumu hiyo dhidi ya Nguza, lakini bado Marando akaonyesha nia ya kuendelea kumpigania mteja wake huyo.

Katika hatua hiyo, wakili huyo aliomba, kuwa Mahakama ya Rufani iteue jopo la majaji watano ili waipitie tena adhabu hiyo akiamini mteja wake huyo alizushiwa tuhuma hizo zote.

Ili kumpa haki yake, mahakama hiyo ilikubaliana na maombi ya Marando ya kuteua jopo hilo la majaji watano, wale ambao pia waliridhika pasipo na shaka kuwa hukumu ya kifungo cha maisha dhidi ya Babu Seya ilikuwa ya haki.

Katika kesi ya msingi dhidi yake na wenae watatu, wawili kati yao wakifanikiwa kuachiliwa huru baadaye, Babu Seya alituhumiwa kubaka, kunajisi na kulawiti watoto wadogo, wale ambao kuna wengine walikuwa na wastani wa miaka 10 tu!

Miaka 11 baada ya hukumu hiyo kutolewa dhidi yake, mgombea urais anayetaka kuwa kiongozi mkuu wa nchi hii anakuja na ahadi ya kumwachilia huru mhalifu huyo endapo atashinda uchaguzi mkuu ujao!

Siyo kazi yangu kumwandikia hotuba za kuzungumza anapokuwa mikutanoni, na pia si jukumu langu kumwelekeza cha kusema hususan kero au mahitaji ya Watanzania.

Pamoja na hayo na hata vinginevyo, Watanzania bila ya kujali itikadi zao za kisiasa, dini zao, makabila yao, rangi za ngozi zao, kazi zao, maeneo yao, rika zao ama jinsia zao na kadhalika kamwe hawana hitaji la kutaka kuachiliwa kwa mhalifu yeyote.

Aidha, Watanzania nikiwemo mimi hawahitaji, kwa namna yoyote ile kuachiliwa kwa mhalifu wa aina ya Babu Seya aliyetiwa hatiani kwa makosa ya ubakaji, kunajisi au kulawiti hadi watoto wa miaka 10 tu!

Tumeona maendeleo makubwa kabisa yaliyoletwa na serikali zilizopita hadi hii ya sasa, zote zikiongozwa kwa makini na viongozi waliotokana na Chama Cha Mapinduzi, kile ambacho wengi wanakijua kwa kifupi cha CCM.

Ilianza Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya uongozi thabiti wa Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Ilifuatia Serikali ya Awamu ya Pili, nayo ikiongozwa na mwalimu kitaaluma, Alhaji Ali Hassan Mwinyi kuanzia Novemba 5, 1985 hadi Novemba 21, 1995.

Hiyo nayo ilifuatiwa na Serikali ya Awamu ya Tatu, safari hii ikiongozwa na mwandishi wa habari na mwanadiplomasia, Benjamin Mkapa aliyekuja kujulikana zaidi kama 'Mzee wa Ukweli na Uwazi'.

Huyo alipong'atuka Novemba 21, 2005 iliingia madarakani Serikali ya Awamu ya Nne, pia ikiongozwa na mwanadiplomasia mwingine na afisa mwandamizi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Kanali Jakaya Kikwete.

Katika mpangilio wake huo na chini ya viongozi hao kila moja kwa wakati na enzi zake, serikali zote hizo zilikuja na mikakati yake ya maendeleo kwa taifa na wananchi wake.

Sitaki kurejea nyuma hadi wakati wa utawala wa hayati Mwalimu Nyerere, Alhaji Mwinyi au Mkapa, lakini serikali ya sasa, chini ya Rais Kikwete nayo imefanya mambo mengi makubwa ya maendeleo.

Mfano ni pamoja na mikoa takribani yote nchini hivi sasa, kwa kiwango kikubwa kabisa kuunganishwa kwa barabara za lami.

Akizungumza katika hafla ya wizara yake ya kumuaga Rais Kikwete kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam wiki iliyopita, Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli alisema mtandao wa barabara za lami uliopo hivi sasa nchini ni kilomita 17,700 kutoka chini ya 6,000 zilizokuwepo mwaka 1995.

Mafanikio mengine ni pamoja na ujenzi wa shule za sekondari kwa kila kata, kupandishwa hadhi kwa hospitali zote za mikoa kuwa za rufaa, kuongezeka kwa vyuo vikuu ama vyuo vikuu vishiriki na hata kuwepo kila mkoa nchini na kadhalika.

Pamoja na kusahihisha kidogo kauli yake kuhusu Babu Seya alipokwenda Arusha, bila shaka baada ya kusutwa na viongozi wenzake, suala zima la mfungwa huyo, tena aliyetiwa hatiani kwa makosa ya ubakaji, ulawiti na kunajisi watoto wadogo kabisa kamwe siyo hitaji la Watanzania wa leo wala wa kesho.

Hata miye nisiyekuwa mwanasheria ninafahamu, kwamba makosa hayo kwa mhalifu aliyefungwa kwa kuyatenda kamwe hapewi msamaha wowote ukiwemo wa rais.

Kama siyo udhaifu wa kufikiri kama mgombea urais, nani kamdanganya Lowassa kuwa hitaji la Watanzania ni kuachiliwa huru Babu Seya?

Napatikana kwa Simu Na. 659 220 220 na 0787 088 870
 
Ni dhahiri atakuwa anafahamu kuwa hawakuwa na hatia yeyote ndio maana wakawekwa ndani kama ambavyo ilivyowahi kunenwa.

Lowasa na Jakaya walikua maswahiba wakubwa. Kama Nguza alifungwa kwa shinikizo basi yeye ni mshiriki mkubwa. Hawakukutana barabarani.
 
Ni dhahiri atakuwa anafahamu kuwa hawakuwa na hatia yeyote ndio maana wakawekwa ndani kama ambavyo ilivyowahi kunenwa.

Jamani huu ujinga mwingine kama tukiukubali tutakuwa watu wa hovyo na tutachekwa watu dunia nzima, kuna taratibu za kuendesha mtu, after all babu seya ni nani katika kutafuta maendeleo ya nchi hii? Ama kweli akili ni nywele......
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom