Kila mzazi anajua uchungu wa mototo na mahangaiko anayopata mazazi katika kumlea mwanae, halafu anatokea "Mario" mwenye akili timamu anaanza kuchezea watoto wa wenzie anakamatwa anafikishwa katika vyombo vya sharia anahukumiwa anakata rufaa anashindwa nayeye anaridhika.
Halafu anatokea mtu mmoja kwa sababu anazozijua yeye anasema atamwachia huru mtu aliyepatikana na hatia ya kunajisi watoto, hapana kabisa huo upumbavu siwezi kuungana nao hata kama kwa namna gani.
Sote tunajua uchafu unaofanywa na hawa akina "Mario" sasa wanadhibitiwa mtu mmoja kwa njaa yake ya madaraka anataka kuwaachia huru, tutawatia kiberiti labda akiwaachia awarudishe makwao.
Wapo waliopatikana na hatia wakitetea haki zao, mfano fransis cheka, mbona hasemi atamwachia? wapo wanaohangaika jela kwa kutetea imani za dini yao kama sheikh Ponda na wapo walioko jela kutetea maslahi yao kama sheikh Farid hao kwake sio kitu ila huyu mbakaji tu.
Zipo NGO nyingi zimehangaika kutetea haki za watoto kama kuzuia ukeketaji, mimba za utotoni na haki ya elimu. Zimetumia fedha nyingi na rasilimali nyingi kupambana na matatizo ya watoto, leo mtu aliyewahi kushika nafasi za juu serikalini hili kwake sio hoja, anaona wabakaji ni watu wanaofanyiwa fitina tu, hapana.
Wakati wa sakata la Richmond bungeni, Niliwahi kumsikia mama kilango akilalamika kuletewa ki memo na chifupa kutoka kwa mheshimiwa sasa naamini hapa sio bure kwa huyu mwenzetu, tuchukue tahadhari.