Lowassa: Nitamtoa Babu Seya gerezani

Lowassa: Nitamtoa Babu Seya gerezani

Status
Not open for further replies.
Mwanamke ukimuudhi hii ni mifano ya silaha zake,atakwenda kinyume na matakwa yako ili mradi akukomoe!
 
Lowasa alkuwa akiwajibu wananchi walioulza kwa shauku kubwa kutaka kujua hatma ya Babu Seya endapo atapewa nchi hapo October ambapo wengi walihisi Babu Seya amefungwa kutokana na hila
 
Na akisha mtoa italeta manufaa gani kwa watanzania? Naona sera za kijinga zimeanza
 
Mbona Kinana na viongozi wenzie wanamaliza wanyamapori wetu hafungwi jela!watoto wa viongozi wakubwa serikalini wanauza unga hawapelekwi gerezani!haya ni matokeo ya double standard.
 
Sisi wengine tumeishi Sinza karibu na watoto wale waliolawitiwa. Siwezi kusema mengi kwani mkielezwa undani wa suala hili wengi humu mtatoa machozi huko mliko. Eti sasa huyo Lowasa anataka kumwachia huyo Babu Seya. Sawa afanye hivyo. na tutaona mwisho wake wa huyo Mlawiti.x
 
Ukibahatika kumuona jk uso kwa uso kipindi hiki ambacho EL ana run siasa za upinzani utaona kabisa sura yake ina tabasamu la kulazimisha,kadhoofu kimwili na ana onekana hana amani moyoni maskini baba wa watu JK kuna kitu kina mtafuna sana ndani ya nafsi yake!
 
eti lowassa na babu slaa nani zaidi maana wale wachagga wa mbeya ni balaa jana

yaani
CCM YAMETUFIKA HAPPA

Kwahiyo mmeamua kuchagua ccm b !? MO11
 
Last edited by a moderator:
Wekeni clip ya hotuba ya Lowasa akisema atamtoa gerezani babu Seya!msipoweka hiyo huo ni uzushi!
 
Ukibahatika kumuona jk uso kwa uso kipindi hiki ambacho EL ana run siasa za upinzani utaona kabisa sura yake ina tabasamu la kulazimisha,kadhoofu kimwili na ana onekana hana amani moyoni maskini baba wa watu JK kuna kitu kina mtafuna sana ndani ya nafsi yake!

hv mada inamzungumzia jk yupoje au anaonekanaje kwa sasa au ndo kila sehemu tunaweka ushabiki?
 
Kila mzazi anajua uchungu wa mototo na mahangaiko anayopata mazazi katika kumlea mwanae, halafu anatokea "Mario" mwenye akili timamu anaanza kuchezea watoto wa wenzie anakamatwa anafikishwa katika vyombo vya sharia anahukumiwa anakata rufaa anashindwa nayeye anaridhika.

Halafu anatokea mtu mmoja kwa sababu anazozijua yeye anasema atamwachia huru mtu aliyepatikana na hatia ya kunajisi watoto, hapana kabisa huo upumbavu siwezi kuungana nao hata kama kwa namna gani.

Sote tunajua uchafu unaofanywa na hawa akina "Mario" sasa wanadhibitiwa mtu mmoja kwa njaa yake ya madaraka anataka kuwaachia huru, tutawatia kiberiti labda akiwaachia awarudishe makwao.

Wapo waliopatikana na hatia wakitetea haki zao, mfano fransis cheka, mbona hasemi atamwachia? wapo wanaohangaika jela kwa kutetea imani za dini yao kama sheikh Ponda na wapo walioko jela kutetea maslahi yao kama sheikh Farid hao kwake sio kitu ila huyu mbakaji tu.

Zipo NGO nyingi zimehangaika kutetea haki za watoto kama kuzuia ukeketaji, mimba za utotoni na haki ya elimu. Zimetumia fedha nyingi na rasilimali nyingi kupambana na matatizo ya watoto, leo mtu aliyewahi kushika nafasi za juu serikalini hili kwake sio hoja, anaona wabakaji ni watu wanaofanyiwa fitina tu, hapana.

Wakati wa sakata la Richmond bungeni, Niliwahi kumsikia mama kilango akilalamika kuletewa ki memo na chifupa kutoka kwa mheshimiwa sasa naamini hapa sio bure kwa huyu mwenzetu, tuchukue tahadhari.

Umenena vema mkuu.
 
Sisi wengine tumeishi Sinza karibu na watoto wale waliolawitiwa. Siwezi kusema mengi kwani mkielezwa undani wa suala hili wengi humu mtatoa machozi huko mliko. Eti sasa huyo Lowasa anataka kumwachia huyo Babu Seya. Sawa afanye hivyo. na tutaona mwisho wake wa huyo Mlawiti.x

Kina kitu umekisema hapa ni mara ya pili nakisia! Hapa kuna jambo kubwa limejificha nyuma ya pazia😕
 
Mbona Kinana na viongozi wenzie wanamaliza wanyamapori wetu hafungwi jela!watoto wa viongozi wakubwa serikalini wanauza unga hawapelekwi gerezani!haya ni matokeo ya double standard.

We una akili kweli wewe! Unafananishaje tembo na maisha ya watoto mabinti wa darasa la tatu ambao wanataraji mengi katila uhai wao ambao unakwenda kukatishwa na mibaba yenye tamaa za ngono au ushirikina, na kupoteza matumaini yao yote ya maisha ya watoto hao ya baadae!! Hivi una watoto kweli wewe? Ukute zee zima limemf.....ra binti yako wa darasa la pili au tatu we kama mzazi utaanza kulinganisha na kosa la waua tembo kweli!? Hebu weka ushabiki wako usio na maana kichwani mwako. Babu seya amajaribu kwa kila namna kukata rufaa na kesi ikarudiwa na kurudiwa bado ushahidi uko tight inakuaje mnaingia na kirusi cha ujinga all of the sudden!!
 
Kama Lowasa anadai atamtoa isivyo kisheri labda kwa kutumia mamlaka aliyopewa kisheria kama atakuwa raisi ni fika anajua mtu uyo amefungwa kimagumashi..anapataje nguvu ya kusema atamuachia uyo mtu??? Kuna jambo alikuwa sawa juu ya kifungo chake.
 
hv amekosa hoja kwel za kueleza ule umati wote na kutoa hoja isiyo ya msingi kama hii yan afadhali hata yule wa mil 50 kila kijiji na laptop kila mwl
 
Kwa umakini alionao Mh Lowassa na ukizingatia umahiri wa timu ya wanasheria inayomzunguka hawezi kutoa kauli tata namna hii.
Nikiwa kama mzazi ninalaani vitendo vyote vya udhalilishaji wanavyofanyiwa watoto.Tuwalinde watoto.
 
Nimestuka Lowassa kudharau utawala wa sheria. Babuseya alikata rufaa mahakama kuu ya Tanzania na kushindwa kwa kosa la ubakaji na udhalilishaji watoto.

Je Lowassa hautambui mhimili wa mahakama? Je utaachia wafungwa wote?

Lowassa ataleta mgongano wa kidola.

Chanzo: Raia Tanzania

anachotaka tujue ni kuwa babu seya hakufungwa kwa kukosa bali alifungwa na mungu mtu wa nchi hii
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom