Lowassa: Nitadhibiti rushwa kwa siku 100

Lowassa: Nitadhibiti rushwa kwa siku 100

Lowasa atamuacha magufuli na mbali sana,ccm wasijaribu wala kufikiria kuiba kura maana watajuta na ndio watalaumiwa milele,lowasa amesema kile anawwza tekeleza sasa si mtoe ahadi zenu pia?kwani mumekatazwa?si uhuru wa kuahidi kile mtaweza mnao?
 
We Ocampo kwa nini unadanganya kile ambacho Lowasa kakisema na tulikisikia wenyewe! Hata hilo gazeti la rafiki yake (Rostam) ie Mtanzania halikuandika hivyo!

Gazeti hilo limeandika: 'Ndani ya siku 100 atapambana na rushwa kwa kuanzisha kituo kimoja kila wilaya kitakachotoa huduma zote za serikali - yaani one spot services center'.

Aliongea sentensi hiyo moja tu kuhusu swala la rushwa kama kawaida yake na gazeti hilo limejitahidi kuinukulu vyema bila kuongeza longo longo kama wewe unavyofanya hapa!

Sasa wenye akili timamu wanajiuliza: Hicho kituo kimoja kitakachotoa huduma zote za serikali kinawezekana kweli? Yaani kituo hicho kitoe huduma za matibabu, za kimahakama, za usalama wa raia (polisi, traffic), TRA, tanesco, ardhi na huduma zote zingine zitolewazo na idara na tasisi zote za serikali zilizokithiri kwa rushwa; inawezekana? Kwa mfano pale Muhimbili Hospital kitoe huduma za moyo, mifupa, magonjwa ya akili nk. Hata kama kingekuwa paying center hakiwezi kuondoa rushwa. Rushwa na ufisadi ni suala complex na liko nchi zote duniani isipokuwa labda Vatican. Limekuwapo tangia kuumbwa kwa Mwanadamu. Huwezi ukalimaliza kwa simple thinking ya aina hiyo wala kwa kimiujiza miujiza.

Ocampo tambua kuwa tunatafuta Rais wa nchi na si rais wa chama cha siasa. Tunatafuta Mkuu wa nchi na Amiri Mkuu wa Majeshi yetu ya ulinzi na usalama. Zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania si wanachama wa chama cho chote cha siasa, mimi nikiwa mmoja wao. Tuache ushabiki usio na tija kwenye suala hili mhimu kwa taifa letu. Kampeni si kudanganyana na kusema uwongo. Watanzania watawapima wagombea kwa weledi wao wa kujenga hoja na mikakati thabiti za kutatua matatizo ya wananchi. Watawapima kwa uadilifu wao na uchapakazi wao nk

Nimekosa neno zuri la kukwambia Mkuu,
zaidi labda em yaishi haya unayoyazungumza maana ni logic tupu! ur such a bright person.....
 
Azidhibiti kwanza mambo ya kujinyea hadharani ndio tuamini mengine.
 
Katika watu wa Hovyo wewe ni No.1 Je? Baada ya kuondoka Lowasa ccm Rushwa na Ufisadi umeisha?.

Hata Ibilisi ana wasaidizi wake lakini hakuna mkubwa wa kumshinda.


Je? Chenge, Mwambalaswa, Prof. Muhongo, Prof. Tibaijuka, Ngeleje na Mkapa Kiwira si Mafisadi na Wala Rushwa?
Kama ndiyo.

Wote hao ni wachafu lakini hakuna anayegombea uraisi.


Je? ilikuwaje wahusishwe na Escrow na Kiwira?

Kwa vile ni wachafu.


Je? Kwanini Magufuli anahusishwa na Ufisadi wa kuhonga Nyumba?

Ni umbea tu. Kuhonga nyumba ni kitu rahisi sana kuthibitisha. Hata Tanzania Daima ya MBOWE wangeweza kuchapisha ushahidi. Ila kama ndio uchafu pekee waliouona wa Magufuli ukilinganisha na madhambi ya FISADI PAPA LOWASSA, sio ajabu ndio maana MA:lock1: anapata 69% ya kura za maoni.


Je? Bado unaimani na CCM au ni sehemu ya wanufaika?

CCM Bado ndio chama pekee kinachowawakilisha Watanzania wa dini zote, kabila zote, rangi zote n.k. Zaidi ya hapo, CCM wanaye mgombea bora anayefaa kushughulikia ujenzi wa taifa na kushughulikia mafisadi kwani yeye ni msafi.
 
Hivi zile bil 90 za escrow alipewa nani pale magogoni?

Tuambie wewe unaezijua hizo za Escrow mpaka zilipogawanyiwa. Nijualo mimi ni kuwa, Raisi Mtarajiwa MAGUFULI, Hajapokea Rushwa na Wala Hajatoa Rushwa.

Ila JENEZA LINALOTEMBEA LOWASSA ananuka rushwa kwenye kila orifice yake.
 

Wapiga kura wa JENEZA LINALOTEMBEA = LOWASSA, wanajua kimombo kweli kweli!

CPGylfCWsAAiPqB.jpg
 
Wapiga kura wa JENEZA LINALOTEMBEA = LOWASSA, wanajua kimombo kweli kweli!

CPGylfCWsAAiPqB.jpg

Wewe kubwajinga usiingilie kazi ya Mungu anayepanga hata oct 25 unaweza usiione halafu unabeza wengine. Wewe ni Mungu wa wapi? Ila ishakuwa kawaida ukiwa cc lazima mdomo wako utoe matusi tu
 
Na kuna watu wanashangilia!! Amesema ataidhibiti vipi? MBona hili linatukumbusha zile ahadi za yule genius mwingine... Kikwete?
 
Wamasai nawaamini wakisema nakata anakata kweli kwann usimpe kura LOWASA AFANYE MAAMUZI MAGUMU SI KUCHEKACHEKA TU.
 
tuambie wewe unaezijua hizo za escrow mpaka zilipogawanyiwa. Nijualo mimi ni kuwa, raisi mtarajiwa magufuli, hajapokea rushwa na wala hajatoa rushwa.

Ila jeneza linalotembea lowassa ananuka rushwa kwenye kila orifice yake.

kumbe kubwa jinga ila angalia usije ukatumia ulimi na akili zako vibaya kila mtu ni jeneza linalotembea yuko wapi celina kombani leo?
 
Anaweza kutimiza hayo ndani ya siku 100. Mbona akiwa waziri wa Arthi walalahoi tuligawana bati za mafisadi waliouziwa uwa wa nje wa nchi? mnazi mmoja mtakumbuka palizungushwa bati tayari kwa ujenzi kuanza kwa aiyeuziwa. Lowasa akiwa ungeni Dodoma aliwaamrisha wananchi wavunje huo uzio baada ya aliyedai kuuziwa eneo kukaidi kuvunja mwenyewe.
Lowasa ni mtu wa kazi na si longongo!
 
Wakati wa sakata la wahujumu uchumi watu walitupa viroba vya noti maporini.Sasa zamu ya walarushwa na mafisadi.mtaona matendo ya lowasa na hamtaamini.Mungu twakuomba umlinde raisi wetu wa awamu ya tano EDWARD LOWASA.
 
kumbe kubwa jinga ila angalia usije ukatumia ulimi na akili zako vibaya kila mtu ni jeneza linalotembea yuko wapi celina kombani leo?

  1. RIP Celina. Yeye hakuwa Mgombea Uraisi.
  2. JENEZA LINALOTEMBEA LOWASSA ni mgombea uraisi, anatakiwa awe wazi juu ya afya yake.
CPbF5AGWUAA7PjL.jpg
CPLwttlXAAA4VPX.jpg
 
Wewe kubwajinga usiingilie kazi ya Mungu anayepanga hata oct 25 unaweza usiione halafu unabeza wengine. Wewe ni Mungu wa wapi? Ila ishakuwa kawaida ukiwa cc lazima mdomo wako utoe matusi tu

Mola katupa Macho ili tuone, akili ili tufikirie na midomo ili tuseme. Kila bin-adam ana siku yake lakini sio kila mmoja wetu yuko mahututi lakini bado anang'ng'ania kugombea uraisi.

FISADI LOWASSA = JENEZA LINALOTEMBEA

CPLwttlXAAA4VPX.jpg
 
Lowassa anachekesha sana, Naona ule wa wimbo wa ndiyo Mzee Prof Jay unamhusu.!
 
Watanzania wenzangu tusidanganywe kuwa Magufuli atabadilisha hii nchi... hawezi watoa mabalozi, wakuu wa wilaya na mikoa waliowekwa wiki iliyopita, hawezi ondoa mizizi ya JK, hawezi ondoa mtu pale Bandarini maana wao ndo walimuweka pale.
Lowasa pekee anaweza maana akiingia mabalozi, wakurugenzi, wakuuu wa wilaya na mikoa wote watabalishwa na nchi itapaa hadi watuoneee gere

Lowassa sio atabadilisha nchi bali atabadilisha walaji tu.!
 
Jamani kwa uongo huu ebu mwogopeni shetani pia!!!!! Nikiwahi kusikia ktk east afrika yetu hii kwa muda wa siku 100, kiongozi wa kenya angefanya jambo. Lakini alishindwa. Leo rushwa!! Nyumba za nyasi, kivuko bure na elimu pia!! Basi kama mnatenda dhambi ya usiseme uongo nawashauri mwogopeni shetani.
 
Back
Top Bottom