Lowassa: Nitadhibiti rushwa kwa siku 100

Lowassa: Nitadhibiti rushwa kwa siku 100

Kubwajinga Mvua ya thailand ilikuwa ni sehemu ya kuonyesha kuwa Lowassa ni mtu wa kuthubutu na anapenda kujaribu teknolojia mpya. Nyie bado mnawaambia wakulima waendeleze kilimo kwa Jembe la Mkono na kutegemea mvua inayonyesha kwa Kudra ya Mwenyezi Mungu!! Lazima tuwang'oe Mwaka huu ili nchi yetu iendelee kwa kuakisi Rasirimali tulizonazo.

Allen,
  1. LOWASSA ni mwizi na TAPELI. Ukweli ni kuwa hakuna mvua ya kutengeneza inayotumika kiuchumi mahali popote duniani, achilia mbali Thailand ambao kuna ufuska na utapeli zaidi kuliko mashamba na viwanda. Hiyo mvua ingekuwepo California wangekuwa wanaitengeneza hivi sasa kuondoa ukame walionao.
  2. LOWASSA; Alikuwa anatafuta jinsi nyingine ya kuliibia taifa na wakati huo huo kulizima nyeti la Richimonduli ambalo lilikuwa linamkalia kooni wakati ule.
  3. LOWASSA; Angekuwa ameacha faili la aliyemuahidi mvua ya kujaza mabwawa ya umeme, kama ingekuwa ni kweli, na serikali ya Pinda ingeweza kuendeleza alikoacha wakati na yeye akilisukuma akiwa bungeni. Hayo hayakutokea.
Kwa hiyo ingawa ubunifu tunauhitaji, tena sana, lakini tuwe makini na matapeli kama LOWASSA ambao kila wanachofanya, kwanza wanaangalia maslahi gani binafsi watapata, bila kuangalia hasara gani watalipa taifa.
 
Allen,
  1. LOWASSA ni mwizi na TAPELI. Ukweli ni kuwa hakuna mvua ya kutengeneza inayotumika kiuchumi mahali popote duniani, achilia mbali Thailand ambao kuna ufuska na utapeli zaidi kuliko mashamba na viwanda. Hiyo mvua ingekuwepo California wangekuwa wanaitengeneza hivi sasa kuondoa ukame walionao.
  2. LOWASSA; Alikuwa anatafuta jinsi nyingine ya kuliibia taifa na wakati huo huo kulizima nyeti la Richimonduli ambalo lilikuwa linamkalia kooni wakati ule.
  3. LOWASSA; Angekuwa ameacha faili la aliyemuahidi mvua ya kujaza mabwawa ya umeme, kama ingekuwa ni kweli, na serikali ya Pinda ingeweza kuendeleza alikoacha wakati na yeye akilisukuma akiwa bungeni. Hayo hayakutokea.
Kwa hiyo ingawa ubunifu tunauhitaji, tena sana, lakini tuwe makini na matapeli kama LOWASSA ambao kila wanachofanya, kwanza wanaangalia maslahi gani binafsi watapata, bila kuangalia hasara gani watalipa taifa.

Hivi zile bil 90 za escrow alipewa nani pale magogoni?
 
Waziri Mkuu mstafu na mgombea wa umoja wa Ukawa Ndg. Edward Lowassa katema cheche na kusema Ukawa wakipewa ushindi, ndani ya siku 100 ataziba mianya yote ya rushwa, ufisadi akianza na bandarini ambapo zaidi ya Billioni 21 upotea kwa siku..

Lowassa kasema kuwa serikali ya Ukawa itakuwa na wajibu mmoja tu, ambao ni kutoa huduma iliyobora kwa wananchi na kwa wakati. Hiyo ndio serikali ninayotaka kuiona, na hayo ndio mabadiliko wanayoyataka wananchi. Hili litaendana na kuziba mianya ya rushwa, na nawahidi ndani ya siku 100 mianya hiyo itazibwa.... Alisema

Kwa hii hatua na kauli ya Lowassa ni wazi wananchi wanaelekea kufaidi matunda ya nchi yao, na sio kikundi kidogo cha watu.. Hatua kama hizi zilifanikiwa sana Singapore, Malaysia, Taiwan na Korea Kusini.. Na hata Rwanda baada ya Kagame kuingia ndani ya siku chache alifanikiwa kuthibiti rushwa, ufisadi na aina zote za dhuluma...

Mytake: Nafurahi kuona serikali ya Ukawa kutupeleka katika speed ya maendeleo kama Singapore, Korea Kusini au Malysia....

Ahadi za kusadikika katika nchi ya wasadikika
 
Allen,
  1. LOWASSA ni mwizi na TAPELI. Ukweli ni kuwa hakuna mvua ya kutengeneza inayotumika kiuchumi mahali popote duniani, achilia mbali Thailand ambao kuna ufuska na utapeli zaidi kuliko mashamba na viwanda. Hiyo mvua ingekuwepo California wangekuwa wanaitengeneza hivi sasa kuondoa ukame walionao.
  2. LOWASSA; Alikuwa anatafuta jinsi nyingine ya kuliibia taifa na wakati huo huo kulizima nyeti la Richimonduli ambalo lilikuwa linamkalia kooni wakati ule.
  3. LOWASSA; Angekuwa ameacha faili la aliyemuahidi mvua ya kujaza mabwawa ya umeme, kama ingekuwa ni kweli, na serikali ya Pinda ingeweza kuendeleza alikoacha wakati na yeye akilisukuma akiwa bungeni. Hayo hayakutokea.
Kwa hiyo ingawa ubunifu tunauhitaji, tena sana, lakini tuwe makini na matapeli kama LOWASSA ambao kila wanachofanya, kwanza wanaangalia maslahi gani binafsi watapata, bila kuangalia hasara gani watalipa taifa.

Stupid
 
mi naamini kabisa Lowasa anaweza hata hizo siku100 ni nyingi sana kwasababu Lowasa ana uzoefu na hayo mambo
 
We Ocampo kwa nini unadanganya kile ambacho Lowasa kakisema na tulikisikia wenyewe! Hata hilo gazeti la rafiki yake (Rostam) ie Mtanzania halikuandika hivyo!

Gazeti hilo limeandika: 'Ndani ya siku 100 atapambana na rushwa kwa kuanzisha kituo kimoja kila wilaya kitakachotoa huduma zote za serikali - yaani one spot services center'.

Aliongea sentensi hiyo moja tu kuhusu swala la rushwa kama kawaida yake na gazeti hilo limejitahidi kuinukulu vyema bila kuongeza longo longo kama wewe unavyofanya hapa!

Sasa wenye akili timamu wanajiuliza: Hicho kituo kimoja kitakachotoa huduma zote za serikali kinawezekana kweli? Yaani kituo hicho kitoe huduma za matibabu, za kimahakama, za usalama wa raia (polisi, traffic), TRA, tanesco, ardhi na huduma zote zingine zitolewazo na idara na tasisi zote za serikali zilizokithiri kwa rushwa; inawezekana? Kwa mfano pale Muhimbili Hospital kitoe huduma za moyo, mifupa, magonjwa ya akili nk. Hata kama kingekuwa paying center hakiwezi kuondoa rushwa. Rushwa na ufisadi ni suala complex na liko nchi zote duniani isipokuwa labda Vatican. Limekuwapo tangia kuumbwa kwa Mwanadamu. Huwezi ukalimaliza kwa simple thinking ya aina hiyo wala kwa kimiujiza miujiza.

Ocampo tambua kuwa tunatafuta Rais wa nchi na si rais wa chama cha siasa. Tunatafuta Mkuu wa nchi na Amiri Mkuu wa Majeshi yetu ya ulinzi na usalama. Zaidi ya asilimia 70 ya Watanzania si wanachama wa chama cho chote cha siasa, mimi nikiwa mmoja wao. Tuache ushabiki usio na tija kwenye suala hili mhimu kwa taifa letu. Kampeni si kudanganyana na kusema uwongo. Watanzania watawapima wagombea kwa weledi wao wa kujenga hoja na mikakati thabiti za kutatua matatizo ya wananchi. Watawapima kwa uadilifu wao na uchapakazi wao nk
 
Siku 100 ni miezi 3 , hv lowasa anadhani anaowaahidi ni dhaifu kama yeye? Vita ya rushwa anaijuwa kweli? Naanza kuamini wanaomuunga mkono lowasa wameathiliwa na nguvu ya giza
 
Sasa lini, na wapi uliona mwizi akashiriki kumpiga hadi kumuua mwizi mwenzie? yeye ni mwizi, fisadi, mlanguzi halafu eti ataziba mianya ya rusha? namcheka kwa dhakau hah..hah.hahahh.. awadanganye ma mbumbumbu tuu wenye akili timamu wameshashitukaa! NAMI LEO HII NAAPA KWA MUNGU LOWASA AKISHINDA URAIS, MIMI NITABADILI JINSIA YANGU
 
one stop centre,,,,??,shule ya vidudu humohumo,soko la vitunguu humohumo,asee lowasa ni mbunifu sana
 
Veni,vidi,vici. I came,I saw,I conquered. Oh this man Lowassa!
 
Tulia dawa ikuingie wewe gamba....

GAMBA = LOWASSA = CHADEMA.

Mambo mbona yanabadilika haraka-haraka kama una kiongozi mjinga, MBOWE.

CPG4p-tWcAA9r_L.jpg
 
Back
Top Bottom