Lowassa: Nitadhibiti rushwa kwa siku 100

Lowassa: Nitadhibiti rushwa kwa siku 100

Waziri Mkuu mstafu na mgombea wa umoja wa Ukawa Ndg. Edward Lowassa katema cheche na kusema Ukawa wakipewa ushindi, ndani ya siku 100 ataziba mianya yote ya rushwa, ufisadi akianza na bandarini ambapo zaidi ya Billioni 21 upotea kwa siku..

Lowassa kasema kuwa serikali ya Ukawa itakuwa na wajibu mmoja tu, ambao ni kutoa huduma iliyobora kwa wananchi na kwa wakati. Hiyo ndio serikali ninayotaka kuiona, na hayo ndio mabadiliko wanayoyataka wananchi. Hili litaendana na kuziba mianya ya rushwa, na nawahidi ndani ya siku 100 mianya hiyo itazibwa.... Alisema

Kwa hii hatua na kauli ya Lowassa ni wazi wananchi wanaelekea kufaidi matunda ya nchi yao, na sio kikundi kidogo cha watu.. Hatua kama hizi zilifanikiwa sana Singapore, Malaysia, Taiwan na Korea Kusini.. Na hata Rwanda baada ya Kagame kuingia ndani ya siku chache alifanikiwa kuthibiti rushwa, ufisadi na aina zote za dhuluma...

Mytake: Nafurahi kuona serikali ya Ukawa kutupeleka katika speed ya maendeleo kama Singapore, Korea Kusini au Malysia....

Hapo Bandarini yupo rafiki na mfadhili wake Nazim Karamagi!
 
Mfa Maji Haishi Kutapatapa. Mwenzetu ni Mgonjwa na Ana Ndoto za Mwendawazimu.

Hivi LOWASSA Hajaacha Tabia Yake ya Kuwalaghai Watanzania? Zile Mvua za Thailand Ziliishia Wapi?

We kweli kubwajinga kama jina lako.... Mtazidi kusema ni mgonjwa ila sisi tunazidi kutafuta kura kwa wananchi vijijini
 
Ajiandae mapema... Manake kila dili kubwa zilizofanyika awamu hii ya 4 jamaa yupo... Ana mali za kufuru, ni wazi serikali ya Ukawa itataka majibu ya jinsi alivyozipata...

Za Lowassa umejua alivyozipata !?
 
Kubwajinga Mvua ya thailand ilikuwa ni sehemu ya kuonyesha kuwa Lowassa ni mtu wa kuthubutu na anapenda kujaribu teknolojia mpya. Nyie bado mnawaambia wakulima waendeleze kilimo kwa Jembe la Mkono na kutegemea mvua inayonyesha kwa Kudra ya Mwenyezi Mungu!! Lazima tuwang'oe Mwaka huu ili nchi yetu iendelee kwa kuakisi Rasirimali tulizonazo.
 
Kubwajinga Mvua ya thailand ilikuwa ni sehemu ya kuonyesha kuwa Lowassa ni mtu wa kuthubutu na anapenda kujaribu teknolojia mpya. Nyie bado mnawaambia wakulima waendeleze kilimo kwa Jembe la Mkono na kutegemea mvua inayonyesha kwa Kudra ya Mwenyezi Mungu!!

Na hiyo technologia ipo sana tu.... Thailand wanaitumia, Ufaransa kaskazini na hata Benin wanatumia hiyo technolojia..... CCM wamefanya watu kuwa wajin.ga sana, yaani hata vinavyowezekana wenyewe wanona kama haviwezekani
 
Last edited by a moderator:
Ccm mna miaka mingapi kwenye madaraka?? Na kama mlishindwa kuyafanya miaka yoote hiyo sasa ivi ndio mtaeza???? Uko timamu wewe mtoto??

Jiulize lowasa kawa serikalini kwa miaka mingapi ndio uje uhoroje
 
Msituaminishe ujinga ninyi CCM, mngekuwa mnajua mna nafasi kubwa yakupita katika Uchaguzi huu msingetumia Nguvu nyingi kiasi hiki.

Kukodi akina Mtikila na Startv kupiga kampeni ya kumuangusha Lowasa.

Lowasa anaweza, CCM na mafisadi wanajua kuingia kwa Lowassa ikulu nikuwapolezea mbali mafisadi na kuziba mianya ya wizi wao.

kama ingekuwa ccm wanamkataa Lowassa kwasababu wanaipenda nchi hii KIKWETE narudia BWANA JAKAYA MRISHO KIKWETE asingekaa hadharani kutuaminisha pesa ya Escrow si pesa ya Serikali.

CCM na watu wake, wangetuambia Akaunti za Stanibic ambazo hazina majina ni za nani? Mnatuambia Lowasa ni Mwizi? Vipi escrow pia kaiba yeye? Na vipi hizo akaunti pia moja ni ya Lowasa? Kama ni zake tajeni leo. Kama sio basi wenye akaunti wako CCM hadi sasa.

CCM wanawadanganya wajinga wachache sana hapa Tanzania, uwezi kutuambia Lowasa ndie ametufikisha hapa tulipo wakati miaka 8 baada ya kuachia madaraka bado nchi ina kashifa kubwa na ambazo zimetetewa hadi na Rais Jakaya Mrisho Kikwete mmoja wa Washauri wa kikwete ni MAGUFULI mgombea wa ccm kupitia baraza la MAWAZIRI.

Ni bora kuishi na mchawi mmoja kuliko kuishi na wachawi kumi watakaokuwa wakikuwangia kwa Zamu.

Nasema ni bora kuishi na mwizi mmoja kuliko wezi 20 ambao watakuibia kwa zamu kila uchwao.

Kashifa za LOWASA haiwezi kuwa kigezo cha kusema CCM inafaa, au haitoi kibali cha CCM kuwa watakatifu. basi tuambieni Lowasa hafai na Magufuli hafai... Kisha mtupatie anaefaa, lkn kama ni kusema LOWASA hafai kisha CCM iendeleee ni UJINGA tena ujinga uliotukuka.

Hatuwezi endelea kwa mtindo huu, LOWASA atafanya MABADILIKO nchi hii, akishindwa miaka mitano mpk kumi tutaondoa utawala wao, lakn kuikumbatia CCM eti kwasababu lowasa alijiuzulu kwa kashifa ni UJINGA.

Kwani huko CCM kinana si anatuhumiwa kwa biashara ya MENO ya TEMBO kaondoka CCM?

Huko CCM kikwete na Familia yake wanatuhumiwa kwa kujitwalia UKWASI mkubwa na hawakanushi mpk leo, hao familia yake si ndio viongozi hadi sasa?

Na baba anaendelea kuwa mwana ccm, tena mwenyekiti wa CCM au anaondoka ccm ili tuwaone ni wasafi kuliko Lowasa!? Au anakuja CHADEMA ili tuseme mafisadi wameamia CHADEMA?

Huko CCM chenge si ana kashifa za Rushwa na matumizi mabaya ya madaraka, KAONDOKA?

MAMA tibaijuka si anatuhuma za mgao wa kashifa ya ESCROW, kahama ccm Ili tuione ni safi kuliko uchafu wa anaeitwa Lowasa?

MAGUFULI ripoti ya CAG imetuhumu wizara yake kwa ubadhirifu wa mabilioni ya fedha. Keshajibu? Kasema zilienda wapi?

Magufuli anatuhuma za kununua kivuko chakavu kwa pesa nyingi tofauti na thamani yake halisi. Huo ni utakatifu kuliko uchafu wa lowasa?

Hapa sigusi tuhuma za kuuza nyumba kwa mpenzi wake asie mfanyakazi wa serikali lkn nizungumzie hili, kama udhaifu wa magufuli kikazi..

Magufuri ndie aliepiga kelele Tanesco ibomolewe kwakuwa ipo barabarani lkn alinyamazishwa na alitii sauti ya Bosi wake.

Magufuli alizuia malori mazito yasipite katika barabara yakiwa yamezidi uzito, sawa hapa alisimamia sheria lkn Mh mizengo pinda akasema hapana, magufuli akanywea. Hapa nauona udhaifu na uoga wake.

Kama angekuwa na credibility ya utendaji na usimamiaji wa sheria kwa watu makini magufuli angejiuzuru lkn alitii sauti ya Mafisadi wenye malori barabarani.

Sasa leo ndio magufuli ataweza kusimamia kile anaamini? Nimesema kinana ambae ni katibu mkuu wa CCM anatuhuma mitaani za kuwa katika biashara ya meno ya TEMBO, magufuli anaweza mfikisha mahakamani kinana kujibu tuhuma? Wakati huyo ndie anaemnadi na kuzunguka nae nchi nzima katika kampeni?

Kama Kikwete inadaiwa alikuja na Majina matano katika mkutano mkuu likiwepo la magufuli, je kesho akiwa Rais, Magufuli anaweza chunguza tuhuma za ufisadi za familia ya Kikwete? Atawezaje atuambie.

Anasema ataanzisha mahakama ya Mafisadi na Majizi, sawa, Tunakubali anamlenga Lowasa, tukubali lowasa atafungwa na kukutwa na hatia.

Je iyo mahakama itakuwa ya lowasa pekee? Wenye tuhuma kama chenge, kikwete, tibaijuka, mwakyembe, na wengine wengi Magufuli atuambie atawashikia wapi, atawafikishaje? Na atawezaje ikiwa anao ndani ya CCM na ndio wanabeba kampeni zake. Au iyo mahakama ni kwaajili ya Lowasa pekee?

Maana bila shaka akianzisha iyo mahaka atapaswa serikali yake yote iwe mahakamani akianza na yeye na wanaompigia kampeni hadi leo.

Ukweli unabaki hatuwezikataa LOWASA ili CCM ibaki madarakani iyo nikujiibia pesa kushoto na kuweka mfuko wa kulia na Kujisifu eti mimi ni mwizi bora. (kwa wale wanaodhani lowasa kuitwa fisadi ni nafuu ya kuwapa nafasi CCM walikojaa wezi) waendelee kutawala. NI UJINGA NA UJINGA MKUU.

WATANZAIA mnaomkataa Lowasa, tupatieni mbadala wa Lowasa (Chadema) mbali na (CCM) na Magufuli.

Lakn kama hakuna mbadala wa CCM na magufuri anapokataliwa Lowasa na CHADEMA . MIMI NASEMA, BORA lowasa na CHADEMA mara elfu, kuliko CCM na mtekenyaji wake anaebeba NDOTO hewa MAGUFULI.

BORA KUISHI NA GONJWA MOJA UTAKALOTIBU KWA AMANI KULIKO KUISHI NA MAGONJWA MIA KATIKA MWILI MMOJA. UTAKUFA TU

LOWASA KUITWA FISADI SI NAFUU YA CCM KUENDELEA KUAPATA HAKI YA KUIIBIA NCHI HII.
 
Anatafuta ugomvi na wachagga.

Kuna mtu ananambia ukienda idara ya yoyote ukikuta kuna mchagga ujuwe tatizo lako limeisha, unamnunuwa kwa thamani ndogo tu. Mwiko mchagga kukataa pesa.
 
Anatafuta ugomvi na wachagga.

Kuna mtu ananambia ukienda idara ya yoyote ukikuta kuna mchagga ujuwe tatizo lako limeisha, unamnunuwa kwa thamani ndogo tu. Mwiko mchagga kukataa pesa.

Ndio maana wakazikubali za Lowassa
 
Ha ha ha kituko cha mwaka shetani kusema ataanza kumuabudu mungu



Katika watu wa Hovyo wewe ni No.1
Je? Baada ya kuondoka Lowasa ccm Rushwa na Ufisadi umeisha?
Kama ndiyo.
Je? Chenge, Mwambalaswa, Prof. Muhongo, Prof. Tibaijuka, Ngeleje na Mkapa Kiwira si Mafisadi na Wala Rushwa?
Kama ndiyo.
Je? ilikuwaje wahusishwe na Escrow na Kiwira?
Je? Kwanini Magufuli anahusishwa na Ufisadi wa kuhonga Nyumba?
Je? Bado unaimani na CCM au ni sehemu ya wanufaika?
 
Mkuu panua Akili usipanue vidole ni lini lowasa akawa na dhamira ya dhati ya kukemea rushwa



Katika watu wa Hovyo wewe ni No.1
Je? Baada ya kuondoka Lowasa ccm Rushwa na Ufisadi umeisha?
Kama ndiyo.
Je? Chenge, Mwambalaswa, Prof. Muhongo, Prof. Tibaijuka, Ngeleje na Mkapa Kiwira si Mafisadi na Wala Rushwa?
Kama ndiyo.
Je? ilikuwaje wahusishwe na Escrow na Kiwira?
Je? Kwanini Magufuli anahusishwa na Ufisadi wa kuhonga Nyumba?
Je? Bado unaimani na CCM au ni sehemu ya wanufaika?
 
Elewa ujumbe. Atadhibiti maana yake zote zitakuwa zake. Hatakubali deal zichukuliwe na wengine.



Katika watu wa Hovyo wewe ni No.1
Je? Baada ya kuondoka Lowasa ccm Rushwa na Ufisadi umeisha?
Kama ndiyo.
Je? Chenge, Mwambalaswa, Prof. Muhongo, Prof. Tibaijuka, Ngeleje na Mkapa Kiwira si Mafisadi na Wala Rushwa?
Kama ndiyo.
Je? ilikuwaje wahusishwe na Escrow na Kiwira?
Je? Kwanini Magufuli anahusishwa na Ufisadi wa kuhonga Nyumba?
Je? Bado unaimani na CCM au ni sehemu ya wanufaika?
 
Ni upofu tu wa pesa ndio umekufikisha hapo huko nyuma hukuwa hivyo

Fisadi huku kwetu nanjilinji wanajuwa n lowasa ambaye yuko ukawa



Katika watu wa Hovyo wewe ni No.1
Je? Baada ya kuondoka Lowasa ccm Rushwa na Ufisadi umeisha?
Kama ndiyo.
Je? Chenge, Mwambalaswa, Prof. Muhongo, Prof. Tibaijuka, Ngeleje na Mkapa Kiwira si Mafisadi na Wala Rushwa?
Kama ndiyo.
Je? ilikuwaje wahusishwe na Escrow na Kiwira?
Je? Kwanini Magufuli anahusishwa na Ufisadi wa kuhonga Nyumba?
Je? Bado unaimani na CCM au ni sehemu ya wanufaika?
 
Katika watu wa Hovyo wewe ni No.1
Je? Baada ya kuondoka Lowasa ccm Rushwa na Ufisadi umeisha?
Kama ndiyo.
Je? Chenge, Mwambalaswa, Prof. Muhongo, Prof. Tibaijuka, Ngeleje na Mkapa Kiwira si Mafisadi na Wala Rushwa?
Kama ndiyo.
Je? ilikuwaje wahusishwe na Escrow na Kiwira?
Je? Kwanini Magufuli anahusishwa na Ufisadi wa kuhonga Nyumba?
Je? Bado unaimani na CCM au ni sehemu ya wanufaika?

Naamua kukusamehe maana umekua juzi , hujui unachoandika Bali naishia kusema una Akili za nyumbu
 
Back
Top Bottom