Lowassa kuwa mgeni rasmi ktk ujenzi wa kanisa RC Kyela

aliyomfanyie Mwakyembe awe makini asijepingwa mawe na wananchi.View attachment 47211Tazama picha hii ujue binadamu hana huruma kwa mwenzie.

Nilikuwa Kyela kama wiki mbili zilizopita. Mwakyembe kapoteza umaarufu sana huko kwao. naona EL ameamua kwenda kummalizia sasa. Kwa heri Dr. Mwakyembe
 
Huko jimboni kwetu, Kyela, afikirie mara mbili kwenda,
Pamoja na kuwa Mwakyembe ni mbunge wao lakini bado ni ndugu na jamaa yao, kwa mila za Kinyakyusa,
Watu wa kule wanajua nini maana ya UJASIRI na kuwa MKWELI,
Watamuonesha ujasiri wao kwa njia yeyote ile
,
Na watamwambia ukweli bila kujali.
Haya na tusubiri!

Tanzania ya leo na jinsi watu walivyo kibiashara zaidi (hata makanisani), hapo kwenye red sidhani kama uko sahihi. Pesa sabuni ya roho (usemi wa zamani ila bado una mantiki kwa umaskini tulionao watanzania). Harambee za EL zinakuwa za nguvu ambayo naamini hata wakienda Mwakyembe na Sitta wakafaanya ya kwao hiyo hela haiwezi fikia ya El na (marafiki zake)
 
Lowassa hakuna alichokosa maishani mwake, anacho tafuta sasa ni kiti cha uraisi kwani ndicho kitakacho weza kumsaidia kulipiza kisasi kwa wabaya wake wa kisiasa! Walhah! . . . Lowassa akiukosa urais atakufa mapema sana!

Ukweli ndio huo atakufa upesi sana na wapambe wake watahangaika sana kwa ombwe atakaloliacha!! Tapeli wa Nigeria kamdanganya kuwa atafanikiwa; akiwa na akili atajua kuwa watabili hucheza na probabilities which in many cases are ZERO!!
 
Lowassa ni mgonjwa ! Kwa waliomwona kwa karibu hivi karibuni watakubaliana nami. Namshauri apumzike. Hatuhitaji raisi mgonjwa.

Mchungaji observation yako ni sahihi; kwa wale waliokuwa bungeni recently na wakamuona Lowassa watakubali kuwa jamaa afya yake ina mgogoro na akiendelea hivyo by 2015 he will be bed-ridden!! Urais anaoutafuta unamtesa sana mentally and physically!
 
Mwalimu Nyerere alisema kuwa kuna watu wanajaribu hata kumhonga Mungu ili wapate urais, recentely kumekuwa na move za kwenda makanisani na misikitini, na kwenye vikao vingi vya ajabu. Leongo ni kukitafuta kiti, Lowassa atatupeleka pabaya. Nakumbuka sehemu ya maneno ya mwalimu ilikuwa ni "wa kuwaogopa kama ukoma". Lowassa anautafuta urais kwa nguvu, inabidi tujue ni kwanini anautafuta urais kwa nguvu, for sure si kwa ajili ya kuleta mazuri kwa Tanzania, lakini ni vizuri tukijua ni kipi anachotaka.

Na wewe vipi? ana utaka urais, hayo ya Nyerere -merehemu yanakujaje hapa

Kikwete aliupigania miaka 10 na akawa rais na mka mpa kura kwa vishindio! HAYO YA NYERERE WANANCHI HAWAYAJUI still mwenye makosa ni mtaka kwenda ikulu??? I dont get it,ebu fikiria kidogo!!

ANAJIALIKA?? mbona watu hamuangalii upande wa pili? whats happening with our senses??
 
Hivi hapa nchini hakuna shughuli zingine za kijamii zinazofanyika zaidi yab hizi za makanisani?

Tumeshamchoka bana! yako mashule mengi yenye upungufu wa madarasa si aende akahamasishe na huko?

anajialika? anajiandika? anakulazimisha umsome??

Wanyakyusa lazima wamle nyama kwa jinsi alivyo watesea kipenzi chao Mwakyembe

c kweli ...mm natoka huko!
 
Unauhakika ni yeye aliyemfanyia?! Angalia , usitudanganye maana aliyemfanyia sasa anahaha kutafuta mtu wa kumtupia zigo- isijekuwa amekutuma uje kuhadaa jukwaa la JF.
aliyomfanyie Mwakyembe awe makini asijepingwa mawe na wananchi.View attachment 47211Tazama picha hii ujue binadamu hana huruma kwa mwenzie.
 
KILAINI na PENGO vipi nyumba za mungu mnazifanyia pango la wala rushwa na ufisadi? Ni vipi mnashiriki kumsafisha alie mchafu kwa fedha zake? hivi nyie ndo mlikua mnapiga kelele za ufisadi kipindi hicho mpaka KILAINI ukatupwa BUKOBA ili watu walale? Dhamana mliyopewa ya kuongoza KANISA mtakuja ulizwa na MUNGU.....ufisadi mnaukemea lakini fedha za ufisadi mnazitaka shauri yenu....
 
Tanzania ya leo na jinsi watu walivyo kibiashara zaidi (hata makanisani), hapo kwenye red sidhani kama uko sahihi. Pesa sabuni ya roho (usemi wa zamani ila bado una mantiki kwa umaskini tulionao watanzania). Harambee za EL zinakuwa za nguvu ambayo naamini hata wakienda Mwakyembe na Sitta wakafaanya ya kwao hiyo hela haiwezi fikia ya El na (marafiki zake)

Bitabo mkuu,
Nilichokisema nakiamini na nakijua kwa sababu mimi ni mnyakyusa wa Kyela,
Ulizia habari ya Nyerere na Kawawa, huko Kyela walifanyiwa nini?
Pesa ina sehemu yake, but Ujasiri wa hawa watu ni tofauti! Najua ninachokisema
 
BY OLE WAO
Kuntakint,
Unatufanya sisi wengine hatuna vichwa ila tumebandikwa nazi. Kwamba malalamiko aliyotoa mwakyembe polisi juu ya kutishiwa usalama wa maisha yake ilikuwa komedi. Na sasa jaribio la kumuua limefanyika kweli. Kama unafikiri hivyo, basi Lowassa na aje Kyela atatukuta. Kama anajiamini kiasi hicho na aje. Ila nakuhakikishia jambo moja tu kuwa atapata majibu ya uchungu wa wana-kyela atakapofika nyumbani kwetu. Tunaomba sana aje atatukuta.

Ni kupoteza muda kuendelea kumwamini Mwakyembe aliyelidanganya bunge na Taifa kwakuficha kwa kuficha mambo muhimu kwenye taarifa ya Richmond atashindwajwe kuidanganya polisi kwa sababu zake za kujiongezea umaarufu wa kisiasa? Siasa ni kama wacheza soka ukimgusa tu akiwa eneo la hatari anajiangusha ili kupata penalt
 
Ni kupoteza muda kuendelea kumwamini Mwakyembe aliyelidanganya bunge na Taifa kwakuficha kwa kuficha mambo muhimu kwenye taarifa ya Richmond atashindwajwe kuidanganya polisi kwa sababu zake za kujiongezea umaarufu wa kisiasa? Siasa ni kama wacheza soka ukimgusa tu akiwa eneo la hatari anajiangusha ili kupata penalt

Kuna tofauti kati ya kudanganya na kutoelezea.....Mwakyembe alisema kuna mambo tumeyaacha ili kulinda heshima na hadhi ya serikali.
Mambo mengi yanasitishwa kwa lengo hilo hilo, tumeona jinsi wanasiasa walivyotoka bungeni kupinga mambo fulani utaratibu uliomuweka rais madarakani, lakini hao hao wakapeleka malalmiko yao kwa rais huyo huyo, aliewekwa na taratibu zile zile.

Huhitaji kuwa mitazamO MGandO, bali uone beyond what you see with your eyes.
Yeye alionyeshwa uungwana kwa kusema wazi kuwa kuna mambo wayaacha kwenye report yao, hakusema hatukuyachunguza. pIA SI UGUNDUZI WAKO KUWA YALIFICHWA, BALI NI KAULI YAKE DHAHIRI KUWA WAMEYAACHA.
 
Pamoja na ukweli kuwa Mwakyembe katika awamu ya pili alianza dharau kwa watu wa Kyela ,baada ya kuteuliwa unaibu waziri bado anabaki ni mwanitu,aliambiwa na wana Kyela kuwa huko aendeko siko ,yeye hakusikia na yamempata ,lakini bado damu ni nzito kuliko maji ,kwa ninavyowajua wanyakyusa wa Kyela nina wasiwasi kusije kukatokea uvunjivu wa amani ,wakati wa hiyo harambee huko saiti,watu wa maknisa wangefikiria mara mbili mbili kwa kitendo cha kumwalika Mr Harambee huko Kyela na wangesoma alama za nyakati.Sitegemei na siamini kama hiyo harambee ndio itakuwa suruhisho la ujenzi wa hilo kanisa ,mbona hiyo harambee haikufanywa miaka ya nyuma,iweje iwe sasa kwani huo ujenzi haujaanza leo.Nafikiri hawa watu waliomwita Mr Harambee wamesahau vurugu ambazo zimewahi kutokea Kyela ,watu wa Kyela si wajinga kama wengi wanavyofikiri ,pamoja na wengi wao kutokuwa wasomi,wamekuwa ni zaidi ya hao wasomi.Akina Mwakipesile mwambieni mwenzenu,wawaache wana Kyela wafanya shughuli zao.
 
Bitabo mkuu,
Nilichokisema nakiamini na nakijua kwa sababu mimi ni mnyakyusa wa Kyela,
Ulizia habari ya Nyerere na Kawawa, huko Kyela walifanyiwa nini?
Pesa ina sehemu yake, but Ujasiri wa hawa watu ni tofauti! Najua ninachokisema
Kikolo naona kwa wale wasiowajua watu wa Kyela wangekuwa na muda wa angalau kupitia historia za watu wa Kyela,si Nyerere,Kawawa ,Aboud Jumbe na maraisi waliofuata wamefanikiwa katika malengo ya kuwagawa wana Kyela,afadhali umewakumbusha kwa hilo,wazee wetu hawakuogopa Kawetere bana
 
Hii thread imeanzishwa na lowasa mwenyewe kwa lengo la kupima upepo wa wana kyela na mbeya kwa ujumla. Lowasa ndo mwenye njama zote za kumuua mwakyembe kwa sumu. Ajaribu kutua kyela au mbeya aone watu walivyofula kwa hasira juu yake. Namwambia lowasa km anapima upepo basi nasema namba anayopiga haipatikani na haitakuja kupatikana. Lowasa aendelee kudanganya watu mabwege wa mikoa mingine na si wana mbeya kwani wako imara sana hawatishwi na fedha wanakupopolea mawe mchana kweupee hata uwe na nguvu ya dola
 
tanzania ya leo na jinsi watu walivyo kibiashara zaidi (hata makanisani), hapo kwenye red sidhani kama uko sahihi. Pesa sabuni ya roho (usemi wa zamani ila bado una mantiki kwa umaskini tulionao watanzania). Harambee za el zinakuwa za nguvu ambayo naamini hata wakienda mwakyembe na sitta wakafaanya ya kwao hiyo hela haiwezi fikia ya el na (marafiki zake)

kuna kitu usicho kijua kwa wanyakyusa nasa kyela hata ungekuwa na pesa gani watakuonesha tu,kama kweli anaenda basi siku zake zimetimia,uliza matukio ya nchi hii toka uhuru,
 
Back
Top Bottom