Lowassa kurudi CCM ni ahueni kwa "wasaliti"

Mzalendo_Mwandamizi

JF-Expert Member
Dec 12, 2007
1,117
4,764
Tulioamua kuacha kuiunga mkono Chadema baada ya kumpokea "fisadi" Lowassa Julai 2015 tuliitwa kila aina ya majina mabaya. Juu kabisa ya orodha ndefu ya majina hayo ni "wasaliti." Dokta Slaa pia hakusalimika kutopachikwa jina hilo.

Fast forward to March 2019, Lowassa aliyepelekea baadhi yetu kuitwa wasaliti ametupatia ahueni baada ya kuachana na Chadema na kurudi CCM.

Nadhani huu ni wakati mwafaka wa kujadili dhana ya "usaliti" kwenye siasa zetu. Na tunaweza kuanzia mjadala huu kwa kufanya tafakuri jadidu kwenye jambo hili:

"Kabla ya Lowassa kujiunga na Chadema, alikuwa Mtanzania anayeongoza kwa kuandamwa na chama hicho, akituhumiwa kuwa ni fisadi mkubwa kabisa. Kwa minajili ya kumbukumbu, Lowassa alianza kuandamwa Februari 2006 na akaendelea kuandamwa hadi alipojiunga na Chadema Julai 2015."

Je, kama baadhi ya tulioiunga mkono Chadema (+Dkt Slaa) tuliitwa wasaliti kwa "kosa" la kubadili msimamo, kwanini basi Chadema nayo si wasaliti kwa kufanya "kosa" hilohilo?

Ni picha iliyozoeleka: mwanasiasa wa CCM akihamia upinzani anageuka shujaa lakini mwanasiasa wa upinzani akihamia CCM anageuka msaliti. Kwa bahati mbaya, picha hiyo hutukumba hata sie "political civilians."

Kwa mtazamo wangu, tatizo ni udikteta. Kwamba "usipoafikiana nami basi wewe msaliti." Kwamba sote tunatakiwa kuwa na mitazamo inayofanana,kitu ambacho si tu hakiwezekani hata kama sote tungekuwa mapacha bali pia ni hatari. Imagine kabla ya uhuru, sote tungekuwa na mtazamo kama huu "wakoloni waliletwa na wamisionari. Wamisionari walileta neno la Mungu. Kwahiyo wakoloni si wabaya kwa sababu waliletwa na watu walioleta neno la Mungu."

Tofauti za kimtazamo ni muhimu sana kwa ajili ya mustakabali wa Tanzania yetu. Tunapokerwa na "mitazamo ya kidikteta ya kina Kabudi wanaotaka wote tuimbe mapambio ya kumsifu Jiwe" basi pia tukerwe na kasumba ya kutaka wenzetu wote wawe na mitizamo inayofanana nasi.

Je tutarajie "samahani" kutoka kwa waliotuita wasaliti kwa "kuikimbia Chadema kisa ujio wa Lowassa"? No way. Utamaduni wa kuomba msamaha bado ni mgeni katika Tanzania yetu. Na ukiona mtu anaomba msamaha basi ujue ana matarajio flani zaidi ya kusamehewa. Anyway life goes on but I hope ni funzo muhimu kwa jamii.
View attachment 1038469

Sent using Jamii Forums mobile app
 
1551789293608.png
 
Evarist Chahali ,

..sasa Lowassa amewafuata huko
CCM mlikohamia.

..Je, na nyinyi mtamkimbia kurudi CDM?

..na Magufuli mliyemsaidia utawala wake umekuwa wa MABAVU na UHARIBIFU ktk kila anachojaribu.

..kwa maoni yangu mlipaswa kubaki CDM na kusaidia ktk kampeni za vijana wengi wataka mabadiliko waliokuwa wakigombea UBUNGE na nafasi za UDIWANI.

..Nadhani athari za UKAWA kuwa na wabunge chini ya asilimia 40 kila mpenda mabadiliko anaziona.
 
Tatizo letu tuna wanasiasa wasio wasikivu, hii inawahusu wa vyama vyote.
Tuna wanasiasa wenye tamaa na ulafi wa madaraka washibishe matumbo yao na ya watoto wao. Hawajali wapiga kura wao
Hawajali wafuasi wao wataumizwa kiasi gani na maamuzi yao ya ajabu.
 
Kwahiyo kama ni nafuu kwa wasaliti, vipi kwako wewe uliyeamuwa kuacha kuisapoti chadema fisadi alivyokuja? Ameondoka, wasaliti wamepata haueni, na wewe imekuwaje? Umefuhi? Then what?

What is the solution? Au pambio tu na blah blah? We jasusi bana!
 
Kwa hiyo ndugu Chahali unadhani lengo haswa la upinzani nchi hii ni nini? Ni kupiga harakati na kupigwa mabomu na polisi kama kina Martin Luther King Jr na kina Malcom ? Au lengo ni nini haswa? Mimi naamini lengo la upinzani wa Tanzania ni kumtoa CCM madarakani na kutengeneza mfumo mpya utakaojali maslahi ya taifa kuliko mtu au chama.

Na ndiyo maana sisi kama CHADEMA (including Dk Dlaa,namuheshimu sana) tukaona Lowasa ana nguvu na mtaji wa kutuwezesha kufanya hayo, na ndiyo maana tukamkaribisha. Kufeli kwa hilo hakuna majuto yoyote kwa sababu tupo tayari hata CHADEMA ife lakini CCM watoke madarakani na kuondoa utawala wa mazoea.

HATA CHADEMA IKIFA LEO HATUNA MAJUTO,LENGO LETU CCM ATOKE,IWE CHADEMA AU CUF IWE TLP AU UDP,SISI WAPINZANI TUNAOAMINI CCM HAIWEZI KUTUFIKISHA POPOTE KAMA TAIFA HATUTAKUFA NGUVU YA KUPAMBANA.
Aluta continua.
 
Evarist Chahali ,

..sasa Lowassa amewafuata huko
CCM mlikohamia.

..Je, na nyinyi mtamkimbia kurudi CDM?

..na Magufuli mliyemsaidia utawala wake umekuwa wa MABAVU na UHARIBIFU ktk kila anachojaribu.

..kwa maoni yangu mlipaswa kubaki CDM na kusaidia ktk kampeni za vijana wengi wataka mabadiliko waliokuwa wakigombea UBUNGE na nafasi za UDIWANI.

..Nadhani athari za UKAWA kuwa na wabunge chini ya asilimia 40 kila mpenda mabadiliko anaziona.
Mnachanganya mambo. Wengi ilipofika dakika ya kuchagua either El aende ikulu au JPM, Chadema ilitulazimisha kuchagua mgombea wa CCM kuliko mtu ambaye wenyewe Chadema walitusaidia sana kumfahamu kwa mabaya yake kulinganisha na mgombea wa CCM.

Wengi wanaojielewa hawakuhamia CCM kama dhana mnayojaribu kuijenga. Ule mstari ndio ulioamua uelekeo wa upinzani hata sasa. Mmekazania kujenga dhana kama vile EL alipokaribishwa CDM watu walijiunga na CCM!

Uasi dhidi ya mgombea wa upinzani mliyemleta ndio ugomvi wa kujadili maana naona mnaanza kukimbilia kuhoji tutafanya nini kama vile mnahoji makada wa CCM.

Tuambieni mlicheza karata gani? Wewe binafsi ulifanya juhudi gani kushawishi uongozi kutofanya yale makosa walau hata kwa maandishi tu humu JF kama ulikuwa hukubaliani na hatua ile? Huoni ulishiriki indirectly kama wafuasi wengi humu wanaojifanya sasa hawakuwa wanakubaliana na ule mpango?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabla Lowassa Hajarudi CCM
Lowassa Kajinye anavalishwa Pampasi -Msukuma
Lowassa hafai hata kwa ugali wa Kulumangia -Fisadi - PolePole
Lowassa Fisadi anatembea kama Kobe - Magufuli
Lowassa Fisadi Mroho wa Madaraka -Nape
Lowassa Hawezi Kamwe Kupewa Nchi Fisadi -Ridhiwani Kikwete
Lowassa anaugonjwa wa Prkisonism hawezi hata kushika tonge la ugali -Ikulu hatupeleki wa Wagonjwa _Kibajaji
 
Back
Top Bottom