Lowassa could've done better...

Swali zuri, nadhani list of shame ilianza kabla ya kuvuana gamba. Ile pressure ndo JK akasema “vua gamba”, chadema wakahnganisha “vua gamba, vaa gwanda”
Akashindwa kutafuta court redress?!
 
Wakati mwingine huwa nawaza sijui sasa hivi ingekuwaje kama Lowassa ndiye angekuwa mgombea wa CCM na hatimaye rais wa Tanzania!

Je, hawa makamanda waliomuunga mkono akiwa mgombea wa CHADEMA wangemuunga mkono akiwa CCM au wangeendelea kumpinga na kumwita fisadi?

Hapo ndo unaona umuhimu wa 'consistency' ya msimamo wa Mzee Mwanakijiji. Alimpinga akiwa CCM na akampinga akiwa upinzani/ CHADEMA/ UKAWA.

No expedient flip-flopping! Just good 'ol fashioned principled consistency!
 
Hayakamatiki walituibia "kitaalam" kamanda, kwani umewahi kumuona chenge akikamatwa kwa ufisadi?!
ila ndo hivyo naye ni fisadi kama edo tu
 
Umemix madawa jombaa!

Umesahau ya kamati ya Mwakyembe bungeni? Kwahiyo uwaziri mkuu alijiuzulu kwasababu ya chadema?

Chadema wangekuwa chama tawala, maybe hii pumba yako ndo ingekuwa point.
 
Nilikuwepo bongo kipindi hicho cha uchaguzi. Watu wengi niliokuwa nawafahamu walikuwa ni Lowassa. Mimi siasa na habari za siasa nimeenda na mentality ya ki JF. Ilibidi niwe nanyamaza tu, maana hata kusema simpigii kura sikuweza. Nikasema siendeshwi tena na upepo kama ilivyonitokea enzi za Mrema!

Kwahiyo nikapiga kura kama mwana JF halisi. Siwezi kumlaumu Mzee Mwanakijiji hata kidogo.
 
Magufuli ni rais bora kabisa kuwai kutokea. Acheni akili fupi za kiafrika, huyo lowassa kwa mfano angefanya nini ambacho magu hafanyi zaidi ya wizi yeye na genge lake la kina rostam karamagi
Msukule
 
Hata mimi nilikuwepo bongo kipindi hicho cha kampeni na uchaguzi.

Nilichokiona ni kwamba wale watu wengi walokuwa mstari wa mbele kumlaani Lowassa kwa ufisadi wake ndo waligeuka kuwa wafuasi na washabiki wake.

Watu wakubali wakatae....ukweli ni kwamba CHADEMA waliwachanganya sana watu na mwishowe kuonekana ni watu wasioaminika, walio vigeugeu, na wasio na msimamo.

Nadhani kama Lowassa angehama tu chama na kujiunga CHADEMA na kuwa mwanachama wa kawaida hapo labda watu wangeweza kuelewa.

Lakini siyo kuhama CCM na ndani ya miezi 2 anapewa nafasi ya kugombea urais na ghafla anageuka anakuwa msafi na si fisadi tena ilhali kwa miaka karibu 10 walikuwa wakimwita ni fisadi.

Watu wanamkasirikia bure tu Mzee Mwanakijiji lakini kusema kweli hakuna alichobadilika. Waliobadilika ni hao wanaomchukia. Yeye msimamo wake kuhusu Lowassa haujabadilika....ni uleule.
 
Magu je??? Sitawaangusha..!
 
Napata mkanganyiko inaposema Lowasaa hajashtakiwa kwahiyo sio fisadi.
Na aliyeuza nyumba za serikali hajashtakiwa kwahiyo sio fisadi ni mtu safi?
 
Napata mkanganyiko inaposema Lowasaa hajashtakiwa kwahiyo sio fisadi.
Na aliyeuza nyumba za serikali hajashtakiwa kwahiyo sio fisadi ni mtu safi?
Wewe unadhani ni kwanini Lowassa hajashitakiwa?
 
Ikulu sio hospitali kiasi kwamba ianze kupokea na wagonjwa
 
Rais wangu ni magufuli endeleeni kulalamika ila jamaa ni jembe
 

Yes sir.. angalia yalivyotokea Kenya sasa. Rais aliyeungwa mkono na CHADEMA anaenda kufanya madudu ambayo wao wanamlaumu nayo JPM; hawajasimama kupinga kuuawa kwa wapinzani wala kusema lolote kwa sababu waliamua kubadili safari angani.
 
Magufuli ni rais bora kabisa kuwai kutokea. Acheni akili fupi za kiafrika, huyo lowassa kwa mfano angefanya nini ambacho magu hafanyi zaidi ya wizi yeye na genge lake la kina rostam karamagi
Wewe ndiyo mwenye akili fupi labda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…