hippocratessocrates, Mkuu wangu suala la makundi ndio demokrasia yenyewe mfano tumeona Marekani makundi ndani ya Republican, Democrat, na Tanzania upande wa Chadema kuna makundi ya Dr Slaa, Zitto Kabwe, John Shibuda, Freeman Mbowe.
Aina haja ya kwenda Monduli angalia rekodi yake ya utendaji na alivyokuwa karibu na shughuli za kijami bila kujali itikadi za kisiasa wala dini.
Lowassa, anatoka Kaskazini ambapo ni ngome kuu ya Chadema, kuna uwezekano mkubwa kama Lowassa atapenya kuperurusha bendera ya chama chake mwaka 2015 basi ataisambalitisha vibaya Kaskazini na kuwaacha Chadema hawana la kufanya.
Mkuu Ritz, have to say it was concrete thinking while answering..INGAWA umeacha maswali MENGI ambayo bado nahitaji majibu roka kwako mkuu wangu.
Nadhani, Differences between Republican and Democratic parties is far way beyond our "democracy" may comprehend..maana kuna kutofautoana kwa mawazo(ambako mwishoni waheshimiwa HIJIRUDI lakini nilichoongelea ndani ya makundi esp. ya CCM kama ulivyosema hapo juu ni "UMIMI" na hii ndiyo inayoiharibia reputation CCM.
Mtazamo wangu mkuu Ritz, sidhani kama kuwepo kwa Mh. EL ingawa ni mzuri kiutendaji though ana mabaya yake mengi(personal experience, u can PM me)..bado haitoshi kusema CCM iko katika hali nzuri. Kwasababu,
1. MAJIVUNO/KUJIKWEZA: Viongozi wengi wa CCM hawajishushi/kujinyenyekeza na inadhihirika wazi kupitia kauli zao tukianzia na mwenyekiti Mh. JK , mawaziri n.k.
2. KISASI/ KINYONGO: Mkuu Ritz, Some people are only alive because it's illegal to kill them, Wananchi wengi wana kinyongo/kisasi...na hawana namna ya kutatua matatizo.Hapa namaanisha makundi mfano ya taaluma Walimu, madaktari, waandishi wa habari n.k..hawa hawana chakufanya wanasubiri "kulipiza kisasi" kwa ajili ya udhalimu waliofanyiwa! Hata kama haikuwa hivyo, makundi haya yanatafsiri hivyo.
3. DHARAU/KEJELI: Ni wanchama hao hao, na viongozi wa CCM wenye kubeza kuwa wafuasi wa vyama fulani ni "vijana wa mtaani" (CHADEMA) , wadini ( CUF) n.k..wakisahau makundi haya ndiyo makubwa na yenye kuweza kuweka mustakabali ya Rais hapo 2015.Kwani ni "vijana wa mitaani" hao hao waliomaliza elimu yao juu lakini wapo huko "mitaani" hawana kazi!
4.UFISADI: Sikatai ulikuwepo toka kipindi kile cha Hayati Mwl Nyerere, lakini je ulisikika hivi? Haukukemewa? Leo hii hata Mh. EL amekuwepo katika kashfa mbalimbali za Ufisadi!! Na tabia ya KUWAWAJIBISHA wachache kwa faida ya wengi( TAIFA) kwa sasa inapotea.
5. UTANDAWAZI: Kwa dunia ya leo ya hiki kizazi tukiitacho dotcom(.com), , wananchi hawadanyiki, hawalogeki, kura wanalinda wenyewe(hawaibiwi kura) mbinu ambazo tulizizoea kwa CCM kutumia kwa miaka kadhaa!
Mkuu Ritz, enzi zile ilikuwa mnaweza kuweka jiwe(stone) kwa CCM na binadamu(human being),na jiwe lingeweza kushinda ....KWA SASA
Haijalishi ni nani atakayesimama katika CCM IWAPO suala la uwajibishwaji halitafanyika, na kwa mtazamo wangu, waheshimiwa wengi watahama kutoka CCM kwa kuwa sasa wanahofu ya kutoeleweka ndani ya chama.
So, iwapo CCM itaendelea kufanya inayoyafanya haijalishi atakayekupo Mh. EL/Membe/Sitta/Magufuli...!!2015 nina imani itakuwa mwisho huo...Kumbuka wengi hawaendi upinzani kwa sababu ya Upinzani kuwa na Sera zilizotoka sayari nyingine ila kwa sababu ya CCM KUFUMBIA MACHO na wakati mwingine KUHALALISHA maovu!