Lowassa anasafishwa!

Itapendeza sana kumuona Lowassa kwa mara nyingine.
Ngoja tudikie atasemaje.
 
Hivi JK hawezi kusoma nyakati????? hii nchi kweli itakuja kubadilika kweli?????

Nyambala;

kinachotofautisha Utu na hali nyingine kwnye mazingira yetu ni swala la "Time". kuna dhibitisho kuwa kwnyemaumbile vitu vyote na wanyama wote hawawezi kupersive time. Yaani vyote havijui kuwa kuna muda na kuwa muda huwa unapita. They are dead stiil in moment time.

Utu na ubinaadamu ni tofauti na unjyama.

inabidi kla skunde ya maisha kuweza kudhibitisha utu wako...au sisi tutakuweka wapi?

Kudhibisha utu, ni pamoja na kuweza kuonyesha wazi kuwa unaweza kujitofautisha na muda/nyakati..lazima ujimabandue na ubanduke kwnye muda na kuweza kuusoma. Lazmia uwe objective na nyakati.

Uwezo huo unakupa fursa kuweza kumiliki mazingira tofauti na viumbe wengine. Inasikitisha kuona viogozi wengi walivyo subjective to nyakati. nyakati zimewameza na hawazi kuzisoma.

Msoma nyakati mzuri mapema kabisa angewaza kuona EL alipokuwa anaelekea ... anguko... !!!

Msoma nyakati mzuri anaona President asivyokuwa objectve and to "his own". anaona kuwa akiedelea kujishikiza kwa watu weingine ..atakwenda na amfuriko.

According to the time!

Hakuna mabacho mtu yeyote anageweza kukifanya kumzuia EL asiondoke.

Na

According to the time!!

Hakuna mtu yeyote naweza kumuatach EL na uongozi wa Taifa Uhuru La Tanzania Kwa sasa taifa likabaki salama.

JKNyrere ni mmoja kati ya binaadamu walioweza kuona mbele au mbali..that means he was not subjective to time..and we all his understanding kuhusu EL

Naturaly huwezi kusema EL hana mchango kwa kuendelea kwa taifa la Tz."UPO". Kuna kitu kinaitwa Negative progress. Kwa EL kufanya alivyofanya na kulifanya Taifa kuwa katika hali "ILE.." Watu wengi waliaamka. Palihitajika PM kufanya alivyofanya EL ili kupiga hatua fulani za msingi na muhimu. PM ni ngazi ya juu ambayo...Ingeweza kufanya somo muhimu kueleweka Technicaly!! EL bado tuna muhitaji ili Ku_activate some sublte Understanding kuhusu Mtu,Utu,Haki Na UOGOZI!!! Kusoma mambo haya vitabuni hakutoshi kwenye hali kama hizi. Let Him be there and do what They Plan..and it will always be kwa Faida ya HAKI ya mlala Hoi....aliyesahauliwa kabisa kiuchumu katika nchi yake yeye mwnyewe aliyopewa na Mungu wake...Kwani kwa Msoma nyakati mzuri anatambua fika kuwa hilo ndilo litakalo tokea...!!
 
JF hureeeeeeeeeeee nimekuwa nikisikia tu, Asante Mwema na Manumba!!
Lowasa awe fair enough aruhusu na maswali itapendeza sana

Week end njema

Karibu Mwanamtama, nadhani sasa ni wakati wa kuumwaga huo mtama hapa. Karibu sana

Kwa hakika Lowasa anachekesha sana, hivi haoni kama kwamba amechafuka mpaka basi. TVT hatasema lolote la maana. Anao uwezo wa kusema kamati ni waongo, au wamembambikizia au wanachuki naye?

Nitafurahi kama akitaja aliyrkuwa naye ktk hili dili.
 
Mimi nimekaa mkao wa kula nangoja kusikia anatoa hoja gani .Sibanduki hapa kwenye TV hadi nione analonga nini kwa kweli .
 
The only place we need Lowassa is in a court of law, answering charges.
 
Lunyungu,

Mimi sishangai hata kidogo.Lowassa kupewa muda TVT maana yake ni kuwa JK amekubali. JK kukubali kujiuzulu kwa Lowassa ni kwa sababu alikuwa hana jinsi.Wale wote waliomsifu JK hawakuelewa kwamba JK hafanyi move kama hii ila kwa sababu ya kujisafisha ili approval ratings zipande, sasa zishapanda wanataka kuleta makida makida kwenye kuendesha serikali.

Ingekuwa inakera vya kutosha kama angestaafu bila kuchukuliwa sheria, sasa wanataka kumrudisha kwenye uongozi? Wakifanya hivyo watakuwa wametutukana Watanzania wote matusi ya nguoni.

Umahiri katika kazi hauji kwa watendaji kutaka tu, unakuja kwa watendaji kuwajibishwa na wananchi.Tuendelee kufuatilia kwa karibu na kuwawajibisha ipasavyo.
Kwanza nianze kwa kuwapongeza hawa wenzetu waliofanikisha kurudisha mtando wetu hewani na nesema mwema na mafisadi wote walaaniwe daima.
Pundit naona jk sasa kakubali kuachia nchi kwa vyama vingine maana sisi watz hatuwezi kushuhudia upumbavu kama huu na kukaa kimya.Sisi si ndio wapiga kura bwana ngoja tuone mwisho wao na huo ushikaji wao .jamani hiki kipindi cha tvt tutaweza kupiga kura? au jamaa alishahojiwa?Sisi tunaamini lowassa ni fisadi na ndio mana tunasema wafilisiwe mapema mana kuna uwezekano wa kuhamisha mali jamani
 
Mwache tu Lowassa ajieleze,unajua kujisafisha kunaweza kuwa na matokeo ya aina mbili. Anaweza akajikuta badala ya kujisafisha ndio kajipaka ile mbaya.

Ndio maana ni muhimu mno kuwaruhusu watu waseme, kwani kwa kusema, ni rahisi kugundua pumba na mchele.

Ningependa kweli kusikia mahojiano hayo ya Lowassa. Ningelikuwa mimi mshauri wake, ningemwambia aende kwanza Monduli na kupumzika. Wahenga walisema ng'ombe akiumia malishoni, hujikokota zizini kusaidiwa, kwa yeye zizi lake ni kule Monduli. Huko ndiko kuna watu wanaoweza kumsamehe kwa makosa yote. Huku kwingine sisi tutamlima tu bila kumwangalia usoni.
 
Mwache tu Lowassa ajieleze,unajua kujisafisha kunaweza kuwa na matokeo ya aina mbili. Anaweza akajikuta badala ya kujisafisha ndio kajipaka ile mbaya.

Ndio maana ni muhimu mno kuwaruhusu watu waseme, kwani kwa kusema, ni rahisi kugundua pumba na mchele.

Ningependa kweli kusikia mahojiano hayo ya Lowassa. Ningelikuwa mimi mshauri wake, ningemwambia aende kwanza Monduli na kupumzika. Wahenga walisema ng'ombe akiumia malishoni, hujikokota zizini kusaidiwa, kwa yeye zizi lake ni kule Monduli. Huko ndiko kuna watu wanaoweza kumsamehe kwa makosa yote. Huku kwingine sisi tutamlima tu bila kumwangalia usoni.

Mtanzania kama atakuwa LIVE be sure nitakupeni kila jambo.Nimejaza mapesa kwenye TTCL narindima sasa .Nangoja kuona kama kweli atajitokeza .
 
Nina mashaka hii kitu si live mana nllibahatika jana kuona vijipande kwenye tvt akiwa anajitetea na kusema muda mwingi sasa atakuwa akichunga ng'ombe.Tusubiri mana kama si live watakuwa wameshaedit mambo mengine.
 
Nina mashaka hii kitu si live mana nllibahatika jana kuona vijipande kwenye tvt akiwa anajitetea na kusema muda mwingi sasa atakuwa akichunga ng'ombe.Tusubiri mana kama si live watakuwa wameshaedit mambo mengine.


Kuchunga hawezi .Kazoea wizi na kushikja pesa na dirty deals so simwamini kabisa kwa hili .
 
Posted Date::2/23/2008
Lowassa ajitetea kutopata chochote kutoka Richmond
*Asema ni mkewe pekee aliyejua kuwa atajiuzulu
*Askofu Laizer akataza Wamasai kuitwa Richmond



Na Daniel Mjema, Arusha

WAZIRI Mkuu mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa jana alipokelewa kama shujaa katika uwanja mdogo wa Arusha na katika Jimbo lake la Monduli huku msafara wake ukikadiriwa kuwa na magari zaidi ya 100.

Akihutubia katika mkutano wa hadhara jimboni kwake, Lowassa alisema jana kuwa, alikuwa amesubiri kwa hamu na kwa muda mrefu siku hiyo ili aeleze kile anachokifahamu kuhusu kampuni ya Richmond Devolopment iliyomfanya ajiuzulu.

"Siku nilipoamua kujiuzulu nilimuuliza mke wangu uko tayari? Na yeye akaniuliza na wewe uko tayari?Niwaambie ukweli hakuna mtu mwingine zaidi ya mke wangu aliyekuwa anajua nakwenda kujiuzulu," alisema Lowassa.

Akizungumzia suala la Richmond, Lowassa alisema ukame wa mwaka 2006 ulifanya taifa kuwa na tatizo la umeme. Kutokana na tatizo hilo, serikali iliamua kutafuta mitambo ya dharura.

Wakati Serikali ikifanya hivyo, wataalamu wakamuarifu kuwa liko tatizo la kupata mitambo hiyo kwa sababu mingi ya mitambo hiyo ilikuwa ikipelekwa nchini Iraki.

"Ikumbukwe kuwa Net Group Solutions wakati huo walikuwa wameomba kuongezewa muda wa kuendelea kuliendesha shirika la umeme TANESCO wakakataliwa hivyo wakawa na usongo na Serikali," alisema na kuongeza;


"Tulivyokazana kuwaambia waagize mitambo hiyo, wao walikuwa wanapiga chenga ili ionekane kuwa bila wao isingewezekana kupata mitambo hiyo? hapa tukagundua kuwa wanatuhujumu."

Lowassa alifichua kuwa, ndani ya Net Group Solutions kulikuwepo na baadhi ya mabosi wa kampuni hiyo ambao nao walikuwa na nia ya kuagiza mitambo hiyo kwa maslahi yao jambo ambalo yeye alilishitukia.

Waziri Mkuu huyo aliyejiuzulu alisema, hapo ndipo walipoamua kuachana na TANESCO na kuamua kutumia timu ya wataalamu wa Serikali wakiongozwa na Mwanasheria mkuu wa Serikali Johnson Mwanyika.

Alisema baada ya kupatikana kwa kampuni ya Richmond alianza kusikia minong'ono huku vyombo vya habari vikiandka juu ya kuwepo kwa matatizo katika mchakato mzima wa kuipata kampuni hiyo.

"Nikaanza kusikia minong'ono nikamwita Waziri mwenye dhamana(Hakumtaja kwa jina) nikamuuliza mbona naanza kusikia harufu mbaya kuhusu Richmond lakini Waziri akanihakikishia kila kitu kiko sawa," alisema.

Kadri siku zilivyozidi kelele juu ya Richmond zikazidi hivyo akaamua kuwaita wakubwa wote serikalini wakiongozwa na katibu mkuu kiongozi, Philemon Luhanjo na kuwambia waangalie uwezekano wa kuvunja mkataba huo.

Lowassa alijitetea kuwa, wakubwa hao wakaomba awape muda wa saa moja kupitia vipengele vya mkataba huo na baada ya hapo walikuja na maneno kuwa isingewezekana kuvunja mkataba huo kwani serikali ingepata hasara.

"Lakini mimi niliwauliza mbona tumevunja mkataba na City water wakaniambia aah mzee achana na hilo jambo kwa sababu liko mahakamani, hii ndio hali halisi ya mkataba wa Richmond,"alisema Lowassa.

Alisema binafsi amekubali kuwajibika kwa makosa ya walio chini yake lakini alirejea kauli yake kuwa kamati teule ya Bunge haikumtendea haki kwa kutomhoji kwani anaamini kama ingemhoji isingeandika taarifa kama ile.

"Niliona nisipoachia ngazi hali ya mambo katika chama changu ingekuwa mbaya. Napenda niweke jambo hili sawa kuwa sikuwajibika kwa sababu nilipata chochote Richmond."

Lowassa aliwataka wananchi wa Jimbo la Monduli kutembea kifua mbele, huku wakitambua kuwa yeye hajawahi kupokea rushwa wala hana mpango wa kufanya hivyo bali amewajibika kwa makosa ya walio chini yake.

Kwa upande wake, Askofu wa Dayosisi ya mkoani Arusha ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania(KKKT), Thomas Laizer alitumia nafasi huyo kuwapiga vijembe wale wanaodhihaki kujiuzulu kwa Lowassa.

"Ukuni ulioko kwenye kona usiucheke ukuni ulioko jikoni ukiungua kwa sababu nao unasubiri kuungua," alisema Askofu Laizer bila kufafanua lakini akashangiliwa na mamia kwa maelfu ya wananchi waliohudhuria mkutano huo.

Hata hivyo baada ya kijembe hicho ndipo Askofu Laizer alipotoa kauli yeye utata akitaka kila mtu abebe mzigo wake na akakemea tabia iliyoibuka hivi sasa ambapo kila Mmasai anayeonekana mjini anaitwa Richmond.

"Kuhusu ufisadi na rushwa sisi hatujui kilichotokea lakini kama ni ufisadi basi tunaungana na Rais Jakaya Kikwete kupita vita rushwa, kejeli dhidi ya wamasai kuitwa Rinchmond haifai kila mtu anabeba mzigo wake," alisema.

Lowassa aliwasili katika uwanja mdogo wa ndege wa Mjini Arusha saa 6:51 mchana na kulakiwa na viongozi mbalimbali wa chama cha mapinduzi(CCM) na wale wa kidini pamoja na umati mkubwa wa wananchi.

Katika eneo hilo la uwanja, makundi ya vijana,wanawake na wanaume wakiwa wamebeba mabango mbalimbali ya kumkaribisha Lowassa huku mengine yakimtambulisha kama Shujaa wa karne.

Baadhi ya mabango hayo yalisomeka "Shujaa wetu umeonyesha mfano usife moyo, Tupo pamoja nawe, Wana Monduli tunakuamini na Mheshimiwa Lowassa wewe ni Mbunge wetu 2005-2025."

Mara baada ya kusalimiana na baadhi ya viongozi na wananchi waliojitokeza kumlaki uwanjani hapo, Lowassa alipakia katika gari aina ya Toyota Landcruiser likiwa limewekewa ngao ya jadi mbele ya namba za usajili za gari hilo.

Msafara wa Lowassa ambao haujawahi kuonekana kutokana na wingi wa magari na wananchi ulianzia katika uwanja huo wa ndege huku magari yakifunga barabara ya Arusha-Monduli yakitembea pande zote mbili za barabara.

Hii ilifanya magari yaliyokuwa yakitokea Babati, Hanang, Mto wa Mbu, Karatu na mikoa mingine kwenda Arusha yanayotumia barabara hiyo kujikuta yakiegeshwa pembeni ya barabara ili kupisha msafara huo.

Alipofika Jimboni kwake alikwenda moja kwa moja hadi nyumbani kwake na kupumzika kwa muda kisha alikwenda katika eneo aliloandaliwa kuhutubia huku akiwa ametandikiwa zulia jekundu kama viongozi wa kitaifa
 
Habari ambazo zimepatikana hivi punde kutoka kwa chanzo chetu zinasema kwamba, kuna baadhi ya waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vya habari inasemekana wamehongwa na mmoja wa aliyekuwa waziri ktk baraza la mawaziri lililovunjwa aliyekuwa anahusishwa na ufisadi wa richmond ili wamsafishe kwa kumwandika vizuri na kuwa tume haikumtendea haki, chanzo chetu kinasema kuwa waandishi hao wenye roho za kimaskini na wasio na uchungu na nchi yao wamehongwa kiasi kikubwa cha pesa na hivyo wamehaidi kuifanya kazi hiyo.kwa mtindo huu jamani ufisadi utaisha?
 
Mmmhh mwandishi naye wa habari....nadhani alipata bahasha zile za kakhi...Lowassa ana kazi kubwa sana kujiweka sawa maana wa tanzania tupo macho!
 
First thing first, we dare talk openly so lets name names.

Richmond/Arusha/Waziri/Tume/Hongo/Kujiosha = Who else but Lowassa?

Si tushaanza kuwaona hata humu wanakuja na lecture za "mtu" na kwamba Lowassa anahitajika bado.Kwani tulizaliwa jana?

Lowassa atasajiliwa na historia kama Waziri Mkuu wa kwanza Tanzania kuingilia uhuru wa habari kwa kutishia wahariri na kuhonga waandishi.

The only place Lowassa belongs is in a court of law answring charges.
 
...Lowasa huenda akaenda Ubalozini...

Lowassa ni too senior kwenda kuwa balozi...
At most may be kwasababu kuna mwanamtandao UN (Dr. Migiro), kwa mtazamo wangu finyu, Lowassa anaweza pewa kazi ya heshima kusimamia mambo fulani serbia huko etc lakini Lowassa mwenyewe akitaka. Otherwise ni kubanana banana humu humu tu Tanzania.

Kumetolewa highlights kidogo za mahojiano kwenye taarifa ya habari ya jioni leo on TVT kwahiyo kitachorushwa on TVT 8PM GMT ni kitu already recorded... Mahojiano yalifanyikiwa monduli na kuudhuriwa na maelfu ya wananchi wa maeneo ya huko.
 
Taarifa ni kwamba mahojiano ya Lowasa na TVT yatarushwa muda mfupi baada ya taarifa ya habari ya saa mbili usiku huu .Hii itakuwa si LIVE bali a recorded interview so kazi kwenu .
 
Na Askofu KKKT haoni aibu???

Hutetea hata kondoo aliye mchafu??

Naskia EL huwa anatoa fungu kubwa sana kanisani!
 
Na Askofu KKKT haoni aibu..Naskia EL huwa anatoa fungu kubwa sana kanisani!

Lowasa amekuwa anatumika Kanisa na KKT ku boost sifa zake na alikuwa aninuia kugombea Urais sasa sijui itakuwaje kwa muda huu .Ila ukweli jamaa na kanisa lake la KKT ilisha kuwa balaa .
 
Back
Top Bottom