Ni wakati wa kuwasema hadharani vyombo vya habari vya Tz. Acheni unafiki, mlichagua kumbeba Lowassa, sasa kama ni 'kufa kufeni naye kama ni kuzikwa zikweni naye na kama ni kufufuka fufukeni naye'. Acheni unafiki wa kuhamishia habari zenu kwa Magufuli kwa sababu kama hakuwa wa maana kwenu kwa nini sasa hivi mumuone wa maana badala ya Lowassa?.
Vyombo karibia vyombe vya habari kuanzia magazeti na TV, mlimbeba sana Lowassa. Ingawa wanahabari walilamikiwa kuwalisha wananchi habari nyingi za kumpendelea Lowassa huku wakiacha habari zingine zenye umuhimu kwa taifa, mliweka pamba masikioni. Kama ni kwa mapenzi yenu ya dhati kwa Lowassa au ilikuwa ni nguvu ya pesa au u-opportunist wenu basi endeleeni kugandamana naye. Ilikuwa ni jambo ka kushangaza magazeti kama Mwanaanchi, ITVii, Tanzania wa Daima, na magazeti ya Habarii Corp na nk. Kumpamba Lowassa kana kwamba EL amekuwa lulu au amegeuka malaika.
Na kama kwa unafiki wao wanahabari wanamgeukia Magufuli pekee basi waendelee hivyo hivyo hata kama ataangukia pua kwa CDM na UKAWA kwa ujumla wake. Sijui kwa nini wanahabari wanaamua kwa makusudi kuacha kutumia taaluma zao vizuri na badala yake wanaongozwa na mihemuko na maslahi yao binafsi. Sasa wakome kwa tabia zao za kikajanja na waachane kabisa na Magufuli bali wafe, wazikwe na wafufuke na Lowassa.