Lowassa anakusudia kujitoa mbio za Urais

Lowassa anakusudia kujitoa mbio za Urais

Status
Not open for further replies.
Lowassa anakusudia kujitoa mbio za urais, hali ya kambi yake ni tete, mtifuano kati ya wanaotaka ajitoe na wanaotaka apigane mpaka tone la mwisho umeshindwa kufikia mwafaka dakika chache zilizopita.

Hali ni tete sana!
Except I shall see in his hands the print of the nails, and put my finger into the print of the nails, and thrust my hand into his side, I will not believe..... John 20:25
 
mkuu hata Mimi nashangaa wakati alituahidi kuwa atalitolea ufafanuzi
Ule ni moto mkuu alikuwa anajifariji tu ,ujue katika jambo baya ambalo amefanya lowasa sitakuja kumsamehe ni ishu ya Richmond alitufanya watanzania kama majuha halafu kundi lake wote wanakashifa sijui tutakuwa na viongozi wa aina gani.
 
Lowasa akijitoa kuna wengi watajuta maana wamezoea kumfanya shamba la bibi
Ila chakushangaza eti hajui kama wenzake wanamfanya ATM sijui huyu mzee yupoje watu wanamvuna halafu yeye anaona ndiyo jamaa zake hatari kweli.
 
Watu mtashangaa, mtu pekee anayeweza kuhcakikisha usalama na interest za mkuu ea kaya ni Lowassa, mtu pekee anayeza kulinda maslahi ya watu walioifaidi hii inchi for past ten years ni Lowassa, hawa watu kwss pamoja wako salama kama Lowasa anakua rais, mkuu kaya anajua amecheza michezo gani ya hatar, hawezi kirahisi hvo kumwachia mtu from no where kwani yeye hajipendi, Lowasa si chaguo la watanzania bt ni chaguo la watawala na wapiga dili, time will tel!!
 
Mnamfahamu Edward Ngoyai Lowassa au mnamsikia.....mnajiuliza maswali na kujijibu wenyewe,Lowassa ndo rais 2015 mtake msitake
 
Uongo ni dhambi

Kwanini isiwezekane? Naona ameona watia nia ni Wengi sana kinyume cha matarajio kwamba watu wangeogopa baada ya yeye kutangaza nia. Na wenzake wanakuja na mambo muhimu ya kulisaidia taifa, si yeye aliyekuwa anaambiwa acheze wakati wa kutangaza nia, wakati afya mgogoro.
 
mkuu kuna thread ulianzisha asubuhi ukataja top 5 watu wakakubeza ila ukiangalia kuna ukweli fulani maana naona edo mambo yanaanza kuharibika
Sure mkuu edo kiukweli hafiki kokote wazee na watanzania wapenda haki sidhani kama watakuwa tayari kumwachia eti Edo ndiyo awe Rais litakuwa taifa la ajabu sana.Watanipinga lakini ipo siku watakumbuka andiko langu mkuu.
 
Aaaaaaaaaaaa mambo gani haya akijitoa watu watapata wapi hela za kula ngoja wale kwanza mpaka mwishoni kabisa.
Simiyu Yetu ccm hakuna wagawa pesa hii kauli umeitoa wapi?
Nitapingana na wewe hadi mwisho
 
Last edited by a moderator:
Yericko hajawahi kutudanganya na habari zake huwa kama vile nae yupo CC (correct 100%).... Hii itakuwa ni Mara kwanza. Hivi leo kwenye ile listi ya majina yaliyotangazwa Jana TBC kuwa watachukua fomu jina La Lowassa lilikuwemo na alitakiwa kuchukua leo saa saba mchana. Swali mbona hakutokea? tunaomba majibu teamlowasa
 
Except I shall see in his hands the print of the nails, and put my finger into the print of the nails, and thrust my hand into his side, I will not believe..... John 20:25

Lowasa amwekeza sana kweny urais both psychologically and financially. Alianza juhudi hizi tangu mwaka 1993 baada ya kuvuna rundo kubwa sana la hela kutokana na nafasi yake ya uwaziri wa ardhi na uwaziri katika ofisi ya waziri mkuu. Kuanzaia hapo mawazo yake yamekuwa ni Magogoni tu; hawezi kujitoa kirahisi hivyo.
 
Aende zake tumechoshwa kuongozwa na mafisadi, DHAIFU na wasio na sifa hata moja ya kuliongoza Taifa letu. Mtu unagombea Urais halafu issue zinazoliangamiza Taifa wizi, rushwa na ufisadi unazikwepa kiaina. Hatufai kabisa huyu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom