Lowassa anakusudia kujitoa mbio za Urais

Lowassa anakusudia kujitoa mbio za Urais

Status
Not open for further replies.
Kwenye wodi ya wazazi uwa kuna wauguzi, wakunga na watu wa usafi. Katika wote hao uwezi kukosa mwenye bikra mkuu.

Jaribu kuelewa, anaposema kutafuta bikira kwenye wodi ya wazazi kwa uelewa wangu anamaanisha waliolazwa humo wodini ambapo kiuhalisia bikira hawezi kuwepo, Sasa nikuulize mkuu mfano Bugando kuna wodi inaitwa C1 wanalazwa vichaa na wenye mtatizo ya akili je wanapoiita wodi ya vichaa ina maana Wauguzi, Madaktari na watu utakaowakuta humo wote ni vichaa/wana mtatizo ya akili?
 
Lowassa anakusudia kujitoa mbio za urais, hali ya kambi yake ni tete, mtifuano kati ya wanaotaka ajitoe na wanaotaka apigane mpaka tone la mwisho umeshindwa kufikia mwafaka dakika chache zilizopita.

Hali ni tete sana!

ukawa wanajitekenya
 
WanaJF,

Mambo yanazidi kuwa mabovu kwa teamLowassa.

Hii leo kuna taarifa ya mhe Lugola na Serukamba kujiondoa kwenye teamLowassa.

Hadi sasa haijafahamika sababu hasa lakini imeelezwa katika tetesi ni kutokana na wawili hao kugundua kuwa hakuna tena uwezekano wa Lowassa kupitishwa katika ngazi za maamuzi ya chama kufuatia team yake kujaa watu wenye kashfa za rushwa, kukosa maadili na ufisadi.

Aidha, mbali na kujitoa kwa wawili hao, Lowassa mwenyewe anaendelea na safari yake ya matumaini mpaka kieleweke.
Mkuu sema ukweli tu yaliyojiri.
Kwani kina Lugola na Serukamba hawakujua toka mwanzo kuwa wafadhili wakuu wa Lowassa ni mafisadi a.k.a marafiki wa Lowasa?
 
Kama ni kweli, atakuwa kafanya uamuzi wa busara japo wale kupe na ndorobo wanaomzunguka wataumia sana.
Lakini bora kuumia kwa kupe na ndorobo wachache kuliko watanzania katika ujumla wao.
Kuna heshima atapata akifanya hilo kutegemea atatoa sababu ipi. Bora aseme afya imegoma.

hawa CHADOMO wanajitekenya
 
Kama ni kweli, atakuwa kafanya uamuzi wa busara japo wale kupe na ndorobo wanaomzunguka wataumia sana.
Lakini bora kuumia kwa kupe na ndorobo wachache kuliko watanzania katika ujumla wao.
Kuna heshima atapata akifanya hilo kutegemea atatoa sababu ipi. Bora aseme afya imegoma.

Mkuuuu ushaambiwaa lowasa ni #joshuaa wetu ku give up ni makosaa makubwa.. Sanaa..
 
Jaribu kuelewa, anaposema kutafuta bikira kwenye wodi ya wazazi kwa uelewa wangu anamaanisha waliolazwa humo wodini ambapo kiuhalisia bikira hawezi kuwepo, Sasa nikuulize mkuu mfano Bugando kuna wodi inaitwa C1 wanalazwa vichaa na wenye mtatizo ya akili je wanapoiita wodi ya vichaa ina maana Wauguzi, Madaktari na watu utakaowakuta humo wote ni vichaa/wana mtatizo ya akili?

Sipendi kujibizana na vilaza, ila ngoja nikupe elimu kidogo.

Wodi ni jengo, kama ilivyo shule tu. Unaposema wodi, basi uwezi kuitenganisha na hao niliowataja. Ukitaka kutenganisha, basi huko ni katika kulazimisha maana uitakayo wewe iwe sahihi ilhali sio.

Ukisema shule, uwezi kutenganisha walimu, wanafunzi na vifaa vya kufundisha nk

Kama kujifungua tu kwako ndio wodi, basi hata kwenye madaladala nako ni wodi maana kuna wajawazito uwa wanajifungulia kwenye madaladala.

Wodi ya wazazi lazima iwe equiped na pia lazima iwe na personel maalumu kwa ajili ya kazi hizo za kukaribisha viumbe wapya. Hii ndio maana sahihi.

Naamini ukilaza wako kuhusu hili utakuwa umetokomea.
 
Ule ni moto mkuu alikuwa anajifariji tu ,ujue katika jambo baya ambalo amefanya lowasa sitakuja kumsamehe ni ishu ya Richmond alitufanya watanzania kama majuha halafu kundi lake wote wanakashifa sijui tutakuwa na viongozi wa aina gani.

Ile timu ni balaa

1. Lowassa

2.Chenge

3.Karamagi

4.Rostam

5.Tibaijuka

6.Kingunge-umiliki wa stand ya ubungo..

Hii timu kama imekaa mkao wa kufanya biashara ikulu hivi..
 
SAFARI YA MA TUMAINI
Kauli mbiu hii bado inanisumbua kwakweli. Watanzania tuna matatizo mengi yanayotukabili na tunataka yatatuliwe. Matatizo ya ayfa, uchumi, ufisadi elimu nk.
Mtu akipimwa akakutwa na HIV anashauriwa kuishi kwa matumaini. Yaani alikubali tatizo na kufuata masharti, hii ikimaanisha tatizo lake kwa sasa bado halina ufumbuzi lakini kwa kurefusha maisha huenda akaishi mpaka dawa itakapogunduliwa. Safari ya matumaini ina maana hiyo? Je, ufumbuzi wa matatizo yetu bado haujapatikana na badala yake sasa tuishi kwa matumaini? Maana ya kauli mbiu hii hebu iwekeni vizuri. Tutasafiri kwa matumaini mpaka lini? Na ni kwa nini iwe hivyo?
 
Lowassa anakusudia kujitoa mbio za urais, hali ya kambi yake ni tete, mtifuano kati ya wanaotaka ajitoe na wanaotaka apigane mpaka tone la mwisho umeshindwa kufikia mwafaka dakika chache zilizopita.

Hali ni tete sana!

Jambo la maana, kumbe bado anaweza kufikiri. Hata nami nilitaka nimshauri ajitoe
 
Watu mtashangaa, mtu pekee anayeweza kuhcakikisha usalama na interest za mkuu ea kaya ni Lowassa, mtu pekee anayeza kulinda maslahi ya watu walioifaidi hii inchi for past ten years ni Lowassa, hawa watu kwss pamoja wako salama kama Lowasa anakua rais, mkuu kaya anajua amecheza michezo gani ya hatar, hawezi kirahisi hvo kumwachia mtu from no where kwani yeye hajipendi, Lowasa si chaguo la watanzania bt ni chaguo la watawala na wapiga dili, time will tel!!

Mtukane JK matusi yote lakin suala la JK kufanya deal za wizi hayupo.Rais Kikwete sio mwizi na hana wizi, tatizo lake ni kutokuwa mkali sana kww wezi.
 
ONYO:Habari nyingi za Yericko ni hadithi za ndoto tu za kufikirika anazozipata kichwani mwake pindi anapokuwa kwenye stimu za bangi, sio za kuziamini ata kidogo.
 
Lowassa anakusudia kujitoa mbio za urais, hali ya kambi yake ni tete, mtifuano kati ya wanaotaka ajitoe na wanaotaka apigane mpaka tone la mwisho umeshindwa kufikia mwafaka dakika chache zilizopita.

Hali ni tete sana!
Kama hii ni kweli, basi inaonyesha asivyoweza kuunda oganizesheni makini. Ina maana anaweza kuunda serikali ambayo mawaziri, wakuu wa mikoa na mabalozi hawatakuwa wanaongea lugha moja kuhusu ajenda yake.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom