Watanzania sasa amua wenyewe. Lowassa kwa mara nyingine amemshinda Kikwete je Bunge letu litaendelea kuchekelea kwa vile wote ni nyani wana mikia?
Haya chini ni maneno mazito aliyomwaga Lowassa akiamua kumwaga mboga baada ya Kikwete kutaka kumwaga ugali.
"Mwenyekiti utakumbuka kwamba mimi nilishaamua kuvunja mkataba wa Richmond mapema, lakini baada ya kukupigia simu ukiwa katika safari nje ya nchi ulisema tusubiri kwani ulikuwa umepata ushauri wa makatibu wakuu wa wizara, sasa leo hii ninahukumiwa nakuitwa fisadi kwanini?".
"Nilijiuzulu kuwajibika kwa ajili ya kuilinda Serikali yangu na kwa heshima ya chama changu, sasa kwanini leo nahukumiwa kwa jambo hili, tena natukanwa na wana CCM wenzangu na siyo wapinzani nchi nzima kwamba mimi eti fisadi?,"alinukuliwa akihoji Lowassa.
Kadhalika kada huyo wa CCM alinukuliwa akimkumbusha Rais Kikwete kwamba: "Mwenyekiti nikukumbushe mwaka 1997 kule Zanzibar, kina Mzee Daudi Mwakawago walikuja na mafaili yakiwa na tuhuma dhidi ya mtizamo hasi wa jamii dhidi yako, kwa hiyo wakati ule kama si busara za kina Mzee Mkapa (Benjamin) leo usingekuwa hapo ulipo".
sasa nimeamini Lowasa anataka urais kwa gharama yoyote ile na anaungwa mkono na Rais jk,lkn niwakumbushe wenzangu mwaka 1997 kikwte hakuwa amechafuka kwa jamii alichafuka kwa viongozi wenzake tena kwa mambo yao ya starehe zao lkn leo EL amechafuka kwa jamii nzima.Akimsingizia Nape leo atakuwa anamuonea tu mana amechafuka kabla nape hajakuwa mwenezi anachotakiwa aje barabarani atueleze ukweli sisi watu wa site na pia atuambie kwanini baba wa Taifa alimkataa toka mwaka 1995 pale dodoma atueleze tu jee tukimpa huo urais anaoupigania Hatutapata laana ya baba wa Taifa?otherwise sitamkubali Lowasa
wacha hasira mkuu lowasa anaonekana ana mengi ya kutueleza ila ukumbuke mwanasiasa huongea ukweli kwenye jina lake tuu na sio hoja zake na mengineyo...lowasa haitaji huruma za jk bali jk ndio anahaha atamfadhili vipi lowasa kwa kufichiana siri...ikumbukwe kama jk angejiuzulu yeye ingekuwa balaa zaidi ndio maana akamuomba lowasa abebe adhabu yake ili aweze kujilinda na kumlinda yeye siasa mchezo wa hila
OK, alitaka kuvunja mkataba huo kama walivyokuja kufanya baadaye na matokeo tunadaiwa mabilioni. Lowasa anaweza kuueleza umma wa watanzania ni nani aliyewezesha Richmond kupewa mkataba huo aliotaka kuuvunja?Lowassa amekana rasmi kuwa yeye hahusiki na mkataba wa Richmond!
Nanukuu:
mwisho wa kunukuu
Hii leo si sahihi hata yeye (Lowassa) kuhukumiwa kwa kuzingatia kile kinachodaiwa kuwa ni mtizamo wa umma dhidi yake unaompa sura ya ufisadi, jambo ambalo amedai kwamba siyo la kweli.
Chanzo: Mwananchi
Tabia hii ndiyo ninayoikataa mimi kuwa mwanaCCM maana yake unatakiwa ufanya kama huna akili timamu vile, unapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa. Hata kama ungekuwa na upeo gani utadumazwa tu na kuishia kufanya usanii wa maigizo kama binti kawawa anavyofanya kama si mtoto wa mzee wa Simba wa Nyika.
Badala ya kufikiria mambo muhimu ya taifa letu wao ni sherehe na ulaji wa ushindani.
Ni mtazamo wako, lakini Lowasa hajatamka kwamba anataka urais, ila anajisafisha ilivyo hulka ya kibinadamu. Kumwandama peke yake haileti mantiki kwa vile wapo wengi na wapo walio wabaya zaidi yake, iweje leo aandamwe yeye?
Uchaguzi wa Igunga Lowasa hakuwako kule, lakini tumeshuhudia magamba yakifanya hujuma za kijasusi hadi kuangamiza roho za watu kwa ajili ya kugombea ubunge, je hayo yaliyofanyika wangefanya wapinzani nini kingetokea?
Lowasa alishatamka tangu tatizo la Arusha linaanza kuwa jambo hilo lisuluhishwe kwa kukaa pamoja na kujadili, lakini walimsakama na kumwambia anaongea mambo nje ya vikao, sasa angesubiri leo walipo Dodoma ndio awaambie wakae pamoja na Chadema kusuluhisha tatizo wakati sasa damu zimeshawagika? Wangemsiikia Lowasa yanayoendelea leo Arusha yasingetokea.
Maselef shukrani sana kwa kuipenda Title yangu. Hata picha yangu bomba sema mvivu mmoja ajiitaye washawasha ameikopi kiasi cha kunidhalilisha. Naye ni gamba tena la kiakili. Tuendelee kujadili CCM inavyoendelea kubaka taifa letu huku fisadi mkuu Jakaya Kikwete akijifanya atapambana na magamba wakati yeye ndiye gamba kuu.
Wewe usihangaike na huyo, kama hakuna mgogoro muulize CC imekabidhiwa kazi gani na NEC, kama CCM walijua hakuna magamba kwa nini walianzisha dhana ya kuvuana walikuwa wanamvua nani ikiwa wote walikuwa wasafi, utakumbuka Wassira baada ya kutoka Arusha alitamba amemaliza mgororo wa vijana lakini jana akaanza kuwashambulia tena, kwa hiyo wengine hatutashangaa wakitoka kule na kufanya pati kuwa wamemaliza ugomvi wakati sote tumeona kabisa M/kiti kaufunika.Waulize fisadi Rostam, Mwakyembe aliyelambishwa vya kulambishwa, Sitta anayeitwa mnafiki na baadhi ndani ya magamba kwa kutetea maslahi ya nchi dhidi ya malipo ya kifisadi, Wabunge ndani ya magamba ambao hawaridhiki na utendaji wa Kikwete na hivi karibuni walikaribia kumuomba abwage manyanga. Pia usisahau kwamba ukipenda basi chongo utaita kengeza...Kama huoni vitisho ya kutaka kumuua Sitta na Mwakyembe na wahusika kusema hadharani hivyo kwamba wamepokea vitisho vya kunyang'anywa uhai wao kwa njia za simu, basi hutaona lolote lile la kuonyesha mpasuko mkubwa ndani ya magamba. Kwenye upinzani wa kweli ndani ya chama chochote kile cha siasa kunakuwa hakuna vitisho vya kutoana roho, vitisho kama hivi vya kuchukua uhai wa baadhi ya wahusika ndani ya magamba au chama chochote kile huwa vinaashiria mpasuko mkubwa sana.
Wewe usihangaike na huyo, kama hakuna mgogoro muulize CC imekabidhiwa kazi gani na NEC, kama CCM walijua hakuna magamba kwa nini walianzisha dhana ya kuvuana walikuwa wanamvua nani ikiwa wote walikuwa wasafi, utakumbuka Wassira baada ya kutoka Arusha alitamba amemaliza mgororo wa vijana lakini jana akaanza kuwashambulia tena, kwa hiyo wengine hatutashangaa wakitoka kule na kufanya pati kuwa wamemaliza ugomvi wakati sote tumeona kabisa M/kiti kaufunika.
Migogoro CCM ndimo nyumbani mwake, huwezi amini maneno aliyotamka leo Lowassa kwamba (Kikwete kafika pale kwa neema tu) alikuwa nayo moyni zaidi ya miaka kumi ila ukiwauliza wanakuambia ni tofauti tu ya mitazamo, mitazamo gani inafikia kuwekeana sumu? (imefikia wakati hatuaminiani hata kuachiana glass ya maji, JK).
Nape ataadhibiwa si kwa kosa lake bali kwa ujinga wake, alijua wazi anatumiwa na watu walimweleza mapema kuwa wewe ni chambo tu utatupwa, leo lengo lililokusudiwa limeshindikana anageuziwa kibao afadhali basi lingefanikiwa angebaki na heshima yake lakini sasa labda atakachoambulia ni ubalozi wa nje lakini heshima na utu wake kwa watanzania na vijana umepungua kama si kwisha.
Neville Meena na Habel Chidawali, Dodoma
Thursday, 24 November 2011
Lowassa alisema kama alivyozungumza na Makamu Mwenyekiti wa CCM, Pius Msekwa walipokutana jijini Dar es Salaam, tatizo kubwa analolifahamu la vita ya sasa ni urais wa 2015.
Lowassa mwizi tu anawaleeza nyie mlokuwepo chama na kumwona kwenda kanisani basi mnafikiri mtu mzuri sana..Kama yeye alikuwa mkweli kwa nini asiwahutubie Umma mzima wa Watanzania badala yake anaenda katika mikutano ya chama! anajua huko mmejaa masaburi watupu. Kikao cha chama CC wanatokea watu wanafokea wengine as if wao ni Miungu!..damn.
Yeye alikuwa waziri mkuu na sii katibu wa chama, hakuwahi kupendwa na Nyerere hadi leo hii wananchi hawampendi pengine huko kwenu CCM. Halafu naweza sema ni jambazi lililokubuhu yaani anatuondolea watu tu kila mwaka. Kesho sintoshangaa Nape mgonjwa anatakiwa kupelekwa India..
Washawasha ni mpuuzi mmoja tu humu JF, na nashukuru umejipambanuwa kama huna ushirika nae.Maselef shukrani sana kwa kuipenda Title yangu. Hata picha yangu bomba sema mvivu mmoja ajiitaye washawasha ameikopi kiasi cha kunidhalilisha. Naye ni gamba tena la kiakili. Tuendelee kujadili CCM inavyoendelea kubaka taifa letu huku fisadi mkuu Jakaya Kikwete akijifanya atapambana na magamba wakati yeye ndiye gamba kuu.