Sasa mbona huwasemi Lowassa na JK walivyotishia nao kuondoka CCM au wao ni elites hawaguswi. Kutishia kila mtu anaweza kutishia hata ndoa watu hutishia kuvunja ikiwa matakwa yao hayatafikiwa.. sasa jiulize walirudi vipi na iweje JK aliwapa madaraka makubwa zaidi..Hoja tunayokataa sisi hapa ni kule kunyoshewa kidole watu watatu na wakati ndani ya CCM nzima ni uvundo tupu. Vijana wenyewe akina Nape na wenzake kama wana ubavu si wangetoka nje ya CCM na kuanza kuwanyooshea vidole badala ya kuanzisha chama cha CCJ wakati wako ndani ya CCM kitu ambacho ni usaliti wa hali ya juu na tabia ya ukinyoknga. Vijsent tulisimamia kwenye account ya kisiwa cha UK, lowasa Richmond.
Lakini siri ni kwamba account hizo ni za CCM wanaoiba pesa za serikali na kuzificha nje ya nchi kwa kufungua account za watu binafsi. Ndio maana unamwona vijisent katulia tuliiii, Mnadhimu wa jeshi nchini Abdalah Shimbo anapeta tu na account yake ya mabilioni nchini Afrika kusini, yote hayo ni mapesa ya CCM, vinginevyo wasingethubutu kuachwa na kufunikwa kana kwamba hakuna kinachoendelea.
Mkuu wangu usafi unauanza ndani na hasa ukikabidhiwa ufagio sasa mlitaka afanye nini? siasa za majitaka kutukana vyama vya Upinzani wakati uchafu uko ndani mwako!..
Yes, CCM imejaa mafisadi lakini unaanza na wale waliokwisha kamatwa na ushahidi upo na wao ndio sababu ya chama kudhoofika. Popularity ya CCM imeiondolewa na watu hawa na sii JK amini maneno yangu kwa sababu Chadema wametumia tu Ufisadi na sasa hivi CCM mahtuti kisha mnafikiri kwenda Loliondo ndio dawa?.. Lowassa ana nini huyu mtu alotuaminisha mvua za kisayansi na Uganga wa Loliondo...Leo ati ni mtu wa kanisa sana kuvaa ngozi ya kondoo basi mnafikiri kesha kuwa Paulo mtakatifu..Hamjiulizi tu kwa nini kila mtu ni against yeye lakini sii wao kuwa na maadui zaidi, maana nijuavyo maadui wa Nape wanatokana na Lowassa na sii wao wenyewe - WHY?
Nakwambieni atawachafua vibaya sana na hakika kufikia mwaka 2015 sijui CCM watabakia kina nani..