MTK
JF-Expert Member
- Apr 19, 2012
- 8,920
- 6,859
Huku baadhi ya magazeti ya Jumapili yakijitahidi kuweka picha ya Lowassa akisalimiana na Rais Kikwete katika chuo cha Jeshi Monduli, ukweli ni kwamba hali si shwari baina yao.
MBUNGE huyo wa Monduli alikataa kwenda kushiriki chakula cha mchana kwenye ukumbi wa Jenerali Kihwelu kambini hapo mara baada ya rais kuwatunuku Kamisheni maafisa 171 wa jeshi.
Tena kinyume na taratibu, Lowassa aliondoka jeshini hapo kabla ya Kikwete. Kawaida ni hadi Amiri mkuu aondoke ndipo viongozi wengine waruhusiwe.
Hiyo sio habari; ni umbea mtupu!! kwani ni lazima EL ashiriki luncheon? unajuaje kama hakuwa na udhuru muhimu na hivyo kumpa taarifa JK pale walipoongea kwa karibu sana wakiwa wameshikana mikono!? kumbuka wawili hao "hawakukutana barabarani" wana channels zao mahususi kwa ajili ya mawasiliano baina yao!!
Jamani there are more important issues za kujadili sio haya mambo ya hisia na tetesi kila siku; mara leo hajampa mkono! jana hakumtazama usoni! stop all this rubbish.
Najua "binadamu hataishi kwa mkate tu! lakini at this stage katika uhai wa taifa letu habe tuyape kipaumbele mambo ya msingi zaidi kama tunalitakia taifa letu "a new beggining; Mwanzo mpya" na ustawi endelevu; kwa mfano mambo kama haya hapa chini: yanahitaji attention yetu kuliko kumjadili JK na swahiba wake EL!!!!
1. Kuna maprofesa wanapekecha feza za umma na kusimama hadharani na kujiita eti wao ni "Majembe"!!
2. Kuna kina Hawa Ghasia huko TAMISEMI wanavuruga chaguzi za msingi katika utawala wa nchi kwa manufaa ya CCM!!
3. Mgao wa umeme nchi nzima pasi na maelezo! Michango ya kibabe ya maabara za shule lakini serikali inakataa mabilioni ya Tegeta Escrow eti sio feza zake!!;
4. MSD/ hospitali nchini hakuna dawa walala hoi wanakufa kwa kukosa "septrin na Mseto" sio kwenda John Hopkins!
5. Kuna watanzania bado wanakunya na kuoga maji kwatika bwawa lilelile na ng'ombe na mbwa na wanyama pori!
6. Mama zetu wazazi wanalala sakafuni au kubana kwenye kitanda cha futi 3 "mzungu wa 6"!!
7. Kubwa zaidi kuna "katiba ya Vijisenti na Sitta" inayolenga kulinda ufisadi, rushwa na ujangili nchi hii!!; and the litany is very very long.
jamani; give us a break!!