Hamuogopi, bali anaogopesha!. EL amejaaliwa kitu kinachoitwa karama ya kukubalika ambayo JK hana!.
Wakati wa enzi ya Boys II Men, mikoani wakisikia ni ziara ya JK, ni shangwe tuu miguu juu kwani akiisha tayarishiwa ile taarifa, na kupitishwa kule alikopangiwa, jioni ni kula kunywa siku imepita!.
EL akifanya ziara, haishii kwenye taarifa ya makaratasi, kama amepangiwa kufungua mradi kambi ya Makotupora, kwenye taarifa walisema Msalato vyomba vya madarasa vimekamilika, Ihumwa kisima cha maji kimekamilika na maji yanatoka!, katika ziara yake ya kuelekea Makotupora, kwa vile ndio nji hiyo hiyo, anatangaza kuanzia Msaloto kuona vyumba vya madarasa kisha kupitia Ihumwa kuona kisima ndipo auende Makotu!. Sasa ikatokea kumbe hakuna chumba cha darasa wala mradi wa maji!, kilikuwa kinawaka hapo kwa hapo mbele ya kadamnasi ya watu kwa kutaka maelezo, na kesho yake watu hawana kazi!. Hivyo watu walikuwa wakisikia EL anakuja, ni hakuna kulala!, JK akija ni sherehe tuu!.
Na ndio maana wana CCM wote wenye akili timamu wanaitakia mema nchi hii, mwaka 2015 wanamtaka EL, wasiomtaka ni wale CCM waendekeza matumbo!.
Merry X-Mass
Pasco