Loliondo pananuka mauti

my goodness! yani sasa umefikia kiwango cha kusema Yesu alifanya makosa? Tafadhali sana...kubali kuwa huelewi hii ishu. Hapa utaishia kukufuru bure! Sema tu mimi sio mjuzi, na haya ni mawazo yangu. Kwisha. Usijaribu kabisa kueleza vitu usivyojua. Utakosa uzima wa milele bure. Kama huamini Loliondo na unaona kuna vitu basic kwenye biblia vimevunjwa...sawa weka wazi. lakini kama unaanza kwa kuweka story nusu nusu za biblia, utaishia kukufuru kabisa.
Yesu alijua toka mwanzo kuwa atamfufua Lazaro. Huu ulikuwa ni mmoja wa miujiza yake mikubwa. Na 'kuchelewa' kwake (siku tatu) kulikuwa ni njia ya kutimiza huo muujiza.
But my point remains, kuwa watu wanaweza kufa wakiwa wanasubiri msaada Mungu. Huwezi sema kuwa kufa ukiwa njiani ina maana kuwa Mungu hayupo involved. It may suggest that but its not a strong suggestion. Wewe fanya sala muombe Mungu akufunulie ukweli juu ya hii ishu.

Yesu alitenda miujiza mbalimbali kuhihirisha Yeye ni Mungu. Aliacha mambo yatokee ili apate utukufu. Hata tukio la Lazaro kufa liliwaliza wengine Yeye akasema amelala tu, amini, atafufuka. Hivyo kufa kwa Lazaro haikuwa kwa bahati mbaya bali ni kusudi baba atukuzwe katika Mwana. Hata yule kiwete ambaye, Yesu walimuuliza, kazaliwa vile kwa dhambi za wazazi wake? Yesu aliwajibu kuwa, kazaliwa vile ili mapenzi ya Mungu yatimizwe. Hivyo si sahihi sana kuifananisha miujiza ya Yesu na hii ya sasa kwani sisi tumesha mjua Mungu tayari.
 
Babu ameleta balaa kubwa kwa unabii wake wa kutia mashaka, kusema amepewa dawa na MUNGU inayotibu maradhi yote sugu bila kuangalia dini gani kumesababisha maafa makubwa kulinganisha na ilivyotarajiwa.
Vifo vya mateso vya wagonjwa ktk mazingira magumu, mateso wanayopata wagonjwa njiani, vitendo vya ulanguzi wa kukithiri wa nauli, vyakula nk. haya yote ni matokeo ya unabii wake babu.
Tunajua haya yote yapo lakini kwa hili la loliondo ni matokeo ya babu.
Kwa mtazamo wangu huyu "MUNGU" aliye mtuma babu ni waajabu na hayuko fair at all kwa watu wake, mungu anayezidiwa na wagonjwa, mungu mwenye masharti kama sangoma, mungu katili asiyejali watu na kuwaongezea tabu,.
Hakika huyu si MUNGU wangu nimjuae ninaye msoma ktk Bibilia takatifu. Mungu wa rehema anaye taka watu wampokee na kuishi ktk yeye kisha watapata kwakadri ya neema yake. Mungu wangu asiyetuma watu kutoa tiba bali kutuma watu wamtumikie.
Mwisho Bwana asema hivi KWANZA UTAFUTENI UTUKUFU WA MUNGU NA MAMBO MENGINE MTABARIKIWA
 
Babu ameleta balaa kubwa kwa unabii wake wa kutia mashaka, kusema amepewa dawa na MUNGU inayotibu maradhi yote sugu bila kuangalia dini gani kumesababisha maafa makubwa kulinganisha na ilivyotarajiwa.
Vifo vya mateso vya wagonjwa ktk mazingira magumu, mateso wanayopata wagonjwa njiani, vitendo vya ulanguzi wa kukithiri wa nauli, vyakula nk. haya yote ni matokeo ya unabii wake babu.
Tunajua haya yote yapo lakini kwa hili la loliondo ni matokeo ya babu.
Kwa mtazamo wangu huyu "MUNGU" aliye mtuma babu ni waajabu na hayuko fair at all kwa watu wake, mungu anayezidiwa na wagonjwa, mungu mwenye masharti kama sangoma, mungu katili asiyejali watu na kuwaongezea tabu,.
Hakika huyu si MUNGU wangu nimjuae ninaye msoma ktk Bibilia takatifu. Mungu wa rehema anaye taka watu wampokee na kuishi ktk yeye kisha watapata kwakadri ya neema yake. Mungu wangu asiyetuma watu kutoa tiba bali kutuma watu wamtumikie.
Mwisho Bwana asema hivi KWANZA UTAFUTENI UTUKUFU WA MUNGU NA MAMBO MENGINE MTABARIKIWA

.
Sema maandiko yasema hivi.... Japokuwa hata hivyo umeshindwa kuyanukuu vema.
WEE!! UNAJUA MAANA YA BWANA ASEMA HIVI, AU UNAAMUA KUROPOKA TU?
.
 
Babu ameleta balaa kubwa kwa unabii wake wa kutia mashaka, kusema amepewa dawa na MUNGU inayotibu maradhi yote sugu bila kuangalia dini gani kumesababisha maafa makubwa kulinganisha na ilivyotarajiwa.
Vifo vya mateso vya wagonjwa ktk mazingira magumu, mateso wanayopata wagonjwa njiani, vitendo vya ulanguzi wa kukithiri wa nauli, vyakula nk. haya yote ni matokeo ya unabii wake babu.
Tunajua haya yote yapo lakini kwa hili la loliondo ni matokeo ya babu.
Kwa mtazamo wangu huyu "MUNGU" aliye mtuma babu ni waajabu na hayuko fair at all kwa watu wake, mungu anayezidiwa na wagonjwa, mungu mwenye masharti kama sangoma, mungu katili asiyejali watu na kuwaongezea tabu,.
Hakika huyu si MUNGU wangu nimjuae ninaye msoma ktk Bibilia takatifu. Mungu wa rehema anaye taka watu wampokee na kuishi ktk yeye kisha watapata kwakadri ya neema yake. Mungu wangu asiyetuma watu kutoa tiba bali kutuma watu wamtumikie.
Mwisho Bwana asema hivi KWANZA UTAFUTENI UTUKUFU WA MUNGU NA MAMBO MENGINE MTABARIKIWA

si damu na nyama vilivyokufunulia haya bali Baba yetu alie mbinguni.

ubarikiwe sana mpendwa.

Glory to God
 
mkuu kwa mujibu wa maelezo ya babu ni kua kaagizwa kutengeneza tiba ya magonjwa sugu na sio kuhubiri injili.na ndio maana haijalishi imani yako kidini as long as utaamini kua uponyaji upo utapona.wanaokufa inawezekana kabisa hawakua na imani maana sharti moja wapo ni imani juu ya ile huduma na sio Imani juu ya udini wako bali imani kua ukinywa dawa yake utapona.so usilaumu kua huduma ya babu hasaidii kuzalisha matunda ya nguvu ya kiMungu coz hayo sio makusudio yake.makusudio ni kutoa tiba kwa magonjwa sugu kwa binadamu yeyote atakae amini.mtu yeyote atapona mradi tu awe na imani ndio maana huitaji kua mlokole ili dawa ya babu ikuponye, ni imani tu!!

1. Babu kaagizwa na nani, mbona humtaji aliyemuagiza?
2. Aliyemuagiza hajamtuma kuhubiri injili (well, sasa tunaanza kumwelewa aliyemtuma maana hataki injili ihubiriwe)
3. Sharti ni uwe na imani na ile dawa (interesting, usiwe na imani kwa mponyaji ambae ni Mungu bali dawa-this is diverting people from believing in God)
4. Kusudi la dawa ya babu sio kuzalisha nguvu za kiMungu (Oh my God!! I should not come anywhere near Loliondo, its not a safe place)
 
Mwenye uwezo na mamlaka ya kufufua wafu ni Mungu pekee.

Kama mnataka kumlinganisha babu na Mungu hapo ndipo mnaposhindwa hata kuyaelewa maandiko matakatifu, badala yake mnajaribu kujificha kwenye maandiko matakatifu kumshambulia babu kwa sababu ya chuki zenu binafsi.

Ndugu yangu usiwe unasoma Biblia kama unavyosoma gazeti la udaku, unahitaji uwezo wa KiMungu kuisoma na kuielewa Biblia.

Kwani Babu ametumwa na Shetani asiweze kufufua? Katika matendo yote makubwa ya miujiza ulimwona Mungu mwenyewe ameshuka? si anatumia watu wake tuu, sasa iweje babu asiweze kuwafufua ka dawa yake?
 
1. Babu kaagizwa na nani, mbona humtaji aliyemuagiza?
2. Aliyemuagiza hajamtuma kuhubiri injili (well, sasa tunaanza kumwelewa aliyemtuma maana hataki injili ihubiriwe)
3. Sharti ni uwe na imani na ile dawa (interesting, usiwe na imani kwa mponyaji ambae ni Mungu bali dawa-this is diverting people from believing in God)
4. Kusudi la dawa ya babu sio kuzalisha nguvu za kiMungu (Oh my God!! I should not come anywhere near Loliondo, its not a safe place)


Aliemtuma haeleweki ndio maana hatuwezi kumtaja! Ukisema katumwa na Mungu oooh! haiji vizuri, ukisema ametumwa na shetani oooh! inafanana vile! hahahahaha kazi kwelikweli
 
1. Babu kaagizwa na nani, mbona humtaji aliyemuagiza?
2. Aliyemuagiza hajamtuma kuhubiri injili (well, sasa tunaanza kumwelewa aliyemtuma maana hataki injili ihubiriwe)
3. Sharti ni uwe na imani na ile dawa (interesting, usiwe na imani kwa mponyaji ambae ni Mungu bali dawa-this is diverting people from believing in God)
4. Kusudi la dawa ya babu sio kuzalisha nguvu za kiMungu (Oh my God!! I should not come anywhere near Loliondo, its not a safe place)

taratibu inaanza kuwa dhahiri,

hatimaye kila mtu atajua kila lililojificha nyuma ya ile ndoto

kwa Bwana Yesu kila goti litapigwa na kila ulimi utakiri

utukufu na nguvu vina yeye hata milele na milele

ubarikiwe sana mpendwa
 
Kwani Babu ametumwa na Shetani asiweze kufufua? Katika matendo yote makubwa ya miujiza ulimwona Mungu mwenyewe ameshuka? si anatumia watu wake tuu, sasa iweje babu asiweze kuwafufua ka dawa yake?

Nadhani uelewa wako wa maandiko matakatifu una walakini,

Hata kama babu wa loliondo ametumwa na Mungu, bado narudia kukukumbusha kwamba mwenye uwezo wa kufufua wafu ni Mungu pekee, na katika hilo la kufufua wafu Mungu mwenyewe ndiye hutenda kazi. Usijaribu kumlinganisha babu wa loliondo na Yesu Mungu mwana.

Hapa hatuzungumzii matendo yote makubwa na ya ajabu kwa ujumla wake, tunazungumzia specifically hoja ya kufufua wafu, kitu ambacho hakuna mwanandamu yeyote amewahi kupewa uwezo, kipawa ama karama ya kufufua wafu.

Babu wa loliondo ametumwa na Mungu kwa kazi ya kuwapatia watu kikombe, na Mungu mwenyewe anatenda kazi kupitia hapo, suala la kufa ama kutokufa ni Mungu mwenyewe ndo anajua.
 
Ni upi ushahidi wa wazi kwamba babu katumwa na MUNGU?.
Je yeye kusema tu kwamba kaonyeshwa dawa ndotoni na MUNGU yatosha kutufanya sisi tuamini kwamba katumwa na MUNGU?.
Kama ukimwamini babu bila kuhoji, akitokea mtu mwingine akasema ameoteshwa na MUNGU kwamba kila mwisho wa mwezi lile fungu la kumi la mshahara wako umpe yeye( muotaji), utampa?.

Wandugu, yatupasa kuzipima kila roho zinazotumia jina la MWENYEZI MUNGU kufanya mambo yake.
 
Tulishasema jaman hapo mwanzoni kuwa Loliondo patakuwa makaburini, ooh! watu wakaanza kututukana mara nyie mmetumwa ooh mara hili! Sasa mapema kabisa ukweli umekuwa wazi! Ukweli la suala la Loliondo ni la kiimani, na ni gumu kulitafsiri lakini inakuwaje yawe makaburi ya watu?? roho ya mauti hatari sana! Mungu hawezi kuwaponya hao watu kwa neno mara moja mpaka wafe wanasubiri kikombe?? Naogopa kusema sio kazi ya Mungu ila jiulize. Yeremia 5:29-31!!
Tafakuru yangu:-
1. Hivi shetani hawezi kuja akijifananisha kama Mwana wa Nuru?
2. Hivi kweli kumbe watu wanaweza kufa wakisubiria tiba ya Mungu?
3. Hivi kumbe Mungu anaweza kuzidiwa kuhudumia watu aliowaumba?
4. Hivi kumbe Mungu anaweza kuzuia watu wasiongezeke hadi amalize kuwahudumia waliotangulia?
5. Ahaaaa kumbe Loliondo unaweza kuwa mtego wa shetani kumaliza watu wetu?

Nimetosha, lakini sihukumu sijui kama Babu katumwa na mungu au la? ninachoweza kusema tafakari mambo hayo matano!
Nawasilisha

View attachment 25816

Naona ulikuwa unamaanisha hizi.

DSC04415.JPG


DSC04417.JPG


DSC04416.JPG


Kama wenye ndugu wamewaacha hii haipendezi hata kidogo.
 
Ni upi ushahidi wa wazi kwamba babu katumwa na MUNGU?.
Je yeye kusema tu kwamba kaonyeshwa dawa ndotoni na MUNGU yatosha kutufanya sisi tuamini kwamba katumwa na MUNGU?.
Kama ukimwamini babu bila kuhoji, akitokea mtu mwingine akasema ameoteshwa na MUNGU kwamba kila mwisho wa mwezi lile fungu la kumi la mshahara wako umpe yeye( muotaji), utampa?.

Wandugu, yatupasa kuzipima kila roho zinazotumia jina la MWENYEZI MUNGU kufanya mambo yake.

Je wewe una ushahidi gani kwamba hajatumwa na Mungu? una ushahidi gani kwamba katumwa na shetani??

Tatizo sio kuhoji, tatizo ni pale watu mnapomhukumu babu bila kuwa na ushahidi wa maandiko matakatifu, mnamhukumu kwa sababu zenu binafsi.

Nakubaliana na wewe kwamba tunapaswa kuzipima roho zinazotumia jina la mwenyezi Mungu, sasa nakuuliza swali hapa, je wewe umeipima hiyo roho inayotenda kazi kwa babu wa loliondo??
 
Nadhani uelewa wako wa maandiko matakatifu una walakini,

Hata kama babu wa loliondo ametumwa na Mungu, bado narudia kukukumbusha kwamba mwenye uwezo wa kufufua wafu ni Mungu pekee, na katika hilo la kufufua wafu Mungu mwenyewe ndiye hutenda kazi. Usijaribu kumlinganisha babu wa loliondo na Yesu Mungu mwana.

Hapa hatuzungumzii matendo yote makubwa na ya ajabu kwa ujumla wake, tunazungumzia specifically hoja ya kufufua wafu, kitu ambacho hakuna mwanandamu yeyote amewahi kupewa uwezo, kipawa ama karama ya kufufua wafu.

Babu wa loliondo ametumwa na Mungu kwa kazi ya kuwapatia watu kikombe, na Mungu mwenyewe anatenda kazi kupitia hapo, suala la kufa ama kutokufa ni Mungu mwenyewe ndo anajua.
Kalale Loliondo wewe unaambiwa A unasema yei tukusaidiaje?
 
Huna hoja kumbe unabwabwaja tu. Mtakufa njaa mwaka huu, babu kachukua wafuasi wenu wote!!:lol:

yOTE KWA YOTE NI SIKU YA MWISHO! si babu si wewe si mimi hukumu iko swafi tu! hebu soma thread moja imo humu kwenye jukwaa la lugha imeandikwa WANASUBIRI HUKUMU YA MZEE GAZETI!
 
Kuna baazi ya wachangiaji wanaomhukumu babu kwa sababu tu eti Mungu anaemtumia hajajijulisha ni wa dini gani. Hii inanipa wasi wasi kama kweli tunazifahamu tabia za Mungu kwa watu wake. Kwa upande wa watu wa biblia Mungu hakuwahi kujinasibisha na dini yoyote. Au labda tusaidiane kwa upande wa manabii wa Mungu maana ndio huji
funua kwao, dini zao ama dini yao iliitwa je?
Labda tuanze na kina Henoko,Nuhu,Abraham,Isaka,Yakobo,Nehemia,Isaya,Yeremia,Ezekieli mpaka kwa Yahana mbatizaji na wa agano jipya, dini yao iliitwa je?
Au kwa kifupi tujiulize ni nabii yupi katika wote wa OT/NT aliyewahi kuwa na dhehebu?
.
 
Je wewe una ushahidi gani kwamba hajatumwa na Mungu? una ushahidi gani kwamba katumwa na shetani??

Tatizo sio kuhoji, tatizo ni pale watu mnapomhukumu babu bila kuwa na ushahidi wa maandiko matakatifu, mnamhukumu kwa sababu zenu binafsi.

Nakubaliana na wewe kwamba tunapaswa kuzipima roho zinazotumia jina la mwenyezi Mungu, sasa nakuuliza swali hapa, je wewe umeipima hiyo roho inayotenda kazi kwa babu wa loliondo??

Upo ushahidi mwingi ambao unaonyesha kuwa babu na Mungu wanatofautiana sana
1. Masharti- Wakati Mungu amewatuma watumishi wake kwenda ulimwenguni kote kuhubiri injili na kuponya wagonjwa, babu anasema hapana mimi siendi popote watu watanifuata Loliondo.

2. Wakati uponyaji wa Mungu ni for free, mmepewa bure, toeni bure, babu anatoza watu pesa.

3. Wakati palipo na uponyaji wa Mungu watu wanakuwa wazima, kwa babu watu wanakunywa kikombe halafu wanasikilizia kama watapona, wengine wanakufa.

4. Wakati Mungu ana namna tofauti za kuponya (very rich kwenye uponyaji), babu anategemea aina moja ya uponyaji.

Hiyo ya babu huwa tunaiita CULTIC AND DECEPTION MOVEMENT, wenye macho tunamjua AUTHOR wake. The author of this movement has come to KILL and DESTROY!! BE ON THE WATCH TANZANIA!!
 
Upo ushahidi mwingi ambao unaonyesha kuwa babu na Mungu wanatofautiana sana
1. Masharti- Wakati Mungu amewatuma watumishi wake kwenda ulimwenguni kote kuhubiri injili na kuponya wagonjwa, babu anasema hapana mimi siendi popote watu watanifuata Loliondo.

2. Wakati uponyaji wa Mungu ni for free, mmepewa bure, toeni bure, babu anatoza watu pesa.

3. Wakati palipo na uponyaji wa Mungu watu wanakuwa wazima, kwa babu watu wanakunywa kikombe halafu wanasikilizia kama watapona, wengine wanakufa.

4. Wakati Mungu ana namna tofauti za kuponya (very rich kwenye uponyaji), babu anategemea aina moja ya uponyaji.

Hiyo ya babu huwa tunaiita CULTIC AND DECEPTION MOVEMENT, wenye macho tunamjua AUTHOR wake. The author of this movement has come to KILL and DESTROY!! BE ON THE WATCH TANZANIA!!

Pia tumeambiwa tuwe na imani kwamba kikombe kinaponya. He! Hii ni ibada ya sanamu kabisa. Yaani Mungu anafananishwa na kikombe cha babu? Kwamba mzizi hauponyi ila nano lililomo ndani ya kikombe! Wee, wacheni kabisa habari yenu hiyo. Kristo ni NENO. Na huyo neno nimuabuduye mimi hakai kwenye kikombe cha Loliondo kwani yuko moyoni mwangu.
 
Pia tumeambiwa tuwe na imani kwamba kikombe kinaponya. He! Hii ni ibada ya sanamu kabisa. Yaani Mungu anafananishwa na kikombe cha babu? Kwamba mzizi hauponyi ila nano lililomo ndani ya kikombe! Wee, wacheni kabisa habari yenu hiyo. Kristo ni NENO. Na huyo neno nimuabuduye mimi hakai kwenye kikombe cha Loliondo kwani yuko moyoni mwangu.

umehit penyewe kabisa mpendwa,

asomaye na afahamu, kweli sasa ni dhahiri, Neno wa Mungu hawezi kukaa kwenye kikombe wala sehemu nyingine yoyote zaidi ya moyoni mwa mwanadamu. tangu wakati wa Yesu hata sasa na hata milele na milele ijayo, ibada zetu ni za
1. roho
2. Kweli (Neno la Mungu)

hakuna ibada ya kikombe!

NENO wa Mungu alifanyika mwili akakaa kwetu nasi tukauona utukufu wake,
utukufu kama wa Mwana pekee wa Baba
amejaa neema na Kweli
 
Upo ushahidi mwingi ambao unaonyesha kuwa babu na Mungu wanatofautiana sana
1. Masharti- Wakati Mungu amewatuma watumishi wake kwenda ulimwenguni kote kuhubiri injili na kuponya wagonjwa, babu anasema hapana mimi siendi popote watu watanifuata Loliondo.

2. Wakati uponyaji wa Mungu ni for free, mmepewa bure, toeni bure, babu anatoza watu pesa.

3. Wakati palipo na uponyaji wa Mungu watu wanakuwa wazima, kwa babu watu wanakunywa kikombe halafu wanasikilizia kama watapona, wengine wanakufa.

4. Wakati Mungu ana namna tofauti za kuponya (very rich kwenye uponyaji), babu anategemea aina moja ya uponyaji.

Hiyo ya babu huwa tunaiita CULTIC AND DECEPTION MOVEMENT, wenye macho tunamjua AUTHOR wake. The author of this movement has come to KILL and DESTROY!! BE ON THE WATCH TANZANIA!!

Mkuu umejibu vema kabisa, mtu hato ishi wala kupona kwa kikombe cha babu bali kwa neno la uzima likikaa ndani yake
 
Back
Top Bottom