Live Updates: Mdahalo wa katiba ITV leo

Live Updates: Mdahalo wa katiba ITV leo

Wakina Wassira walibadilisha kanuni na moja ya vitu waliingiza kwenye kanuni kuwa bunge maalumu linauwezo kuingiza sura mpya baada ya Ukawa kutoka nje-Lissu
 
wassira amekubali atakuwa subiri tuone jinsi ccm watavyoumbuka leo kwenye mdahalo saa tisa itv

Yaani mabinti wa mbowe mnababaika sana ona sasa TUndu anadai walivyotoka eti kanuni ziliwekwa sura mpya! nani aliwaambia watoke bungeni.?
 
Hivi huyu Lissu ana akili timamu kweli? Anasema kuwa wakiwa UKAWA wametoka, waliobaki wamebadilisha kanuni ili kuongeza sura mpya. Ngoja tusubiri majibu ya Prof Wassira
 
Kumbe lissu uelewa wake Wa kisheria in mdogo sana zaidi amebobea kwenye nadharia tu

Njaa kitu kibaya sana. Mi nahisi we mchumia tumbo. Usiyetaka kuishughulisha akili yako kufikiri ,alafu bado unajiita gt. Haya we bobea vitendo
 
Lipumba - Kazi ya BMK ni kuangalia namna ya kutekeleza maoni ya wananchi.
Wananchi wanataka serikali tatu, kazi BMK ni kuangalia hizi serikali tatu ziweje.
 
Hivi huyu Lissu ana akili timamu kweli? Anasema kuwa wakiwa UKAWA wametoka, waliobaki wamebadilisha kanuni ili kuongeza sura mpya. Ngoja tusubiri majibu ya Prof Wassira

Waraka wa siri naona unatolewa hapo. Ha ha ha ha
 
TL: wakati ukawa wametoka nje ccm na kundi la 201 walithubuthu kuingiza kipengele kwenye sheria kuwa "Bunge maalum la katiba lina mamlaka ya kubadili au kurekebisha na kuingiza kipengele chochote kwenye rasimu ya katiba mpya"
 
Ni kwenye mdahalo wa kuhusu rasimu ya katiba.Hana hoja mpya anabaki kutoa historia zilizofeli! source: nimo ndani ya mjadala.

Huwezi tupa historia ukafika popote when it comes to politics. Angalia context ya mawazo ya Lisu, usiangalie sentensi, context!
 
Moyo wa katiba ni serikali 3 na huu msemo umetoka kwenye waraka wa siri wa CCM-Lissu
 
OMG! Kwa mara ya kwanza leo ndio nimekubali madai ya muda mrefu kwamba Tundu Lissu ni mwongo! Haingii akilini kwamba kanuni za Rasimu ya Katiba Mpya zilibadilishwa baada ya UKAWA kuondoka!! Hoja nyepesi mno hii!!! Jamaa yuko "live" ITV.
 
Hizi kanuni baada ya ukawa kutoka nje walibadilisha kanuni na kuweka kifungu kinachoruhusu bunge maalumu kuingiza sura mpya - Tundu Lissu
 
Back
Top Bottom