Live on ITV - UZALENDO: Dr Slaa vs Mangula

Live on ITV - UZALENDO: Dr Slaa vs Mangula

Status
Not open for further replies.
Mtu hapendwi kwa umri wake, dini yake, kabila yake, rangi yake, au eneo analotoka, ni kwa faida na mchango wake kwa taifa. Tatizo ni mchango mkubwa wa slaa ambao unatishia kila mpenda wizi tanzania, am sorry lkn hata kaka mkubwa hajatoa mchango kwa taifa hili kama ambavyo daktari amefanya, ee kumbe nayeye siku hizi daktari wa kupachikwa!!!
 
Mbona Ddr huwa anatoa midahalo live hapa hapa tu kwa kujibu coments za watu?

Dr ni mwanasiasa mzuri sana tatizo Dj kambadili kabisa, Ddr wa leo sio yule tuliezoea kumuona akiwa kinara bungeni, amekuwa kama Llema tu

Hivi wewe Mbowe na Lema walikufanya nini? Mbona umejaa mahaba nao sana?
 
kwa muumini yoyote wa dini sio vizuri kumwita mwenzio msukule wote tumeubwa kwa mfano wa MUNGU.zaidi nimeona sura yako kwenye ID yako sidhani kama dini yako inahitaji kuita wafuasi wa kiongozi msukule.ila kama ungekuwa na hoja ungejenga hoja kuliko kutusi
Dah! inasikitisha sana. Ndio maana tunaona kila mikutano na maandamano yao vita haziishi. Huyu Mzee na wafuasi (misukule) wake ni hatari sana kwa amani ya Taifa.
 
kwa muumini yoyote wa dini sio vizuri kumwita mwenzio msukule wote tumeubwa kwa mfano wa MUNGU.zaidi nimeona sura yako kwenye ID yako sidhani kama dini yako inahitaji kuita wafuasi wa kiongozi msukule.ila kama ungekuwa na hoja ungejenga hoja kuliko kutusi

Sasa wewe kuongozwa na mtu namna hiyo na ukakubali kila ovu lake na kuliona jema kama si msukule ni nini?
 
Vipindi kama hivi vinasababisha umeme uwe unakatwa dakika chake baada ya kuanza kipindi na kuwashwa kipindi kinapokwisha. Chonde chonde mnatuletea tena balaa la kutangaziwa "....yalikuwa ni matengezezo ya kawaida..."

Magamba hawataki kabisa vipindi vya kuhojiwa live maana vinawaumbua, mara nyingi wanaingia mitini wakiona motion iliyotengwa hawana majibu. Ni chama pekee duniani kinacho ongoza nchi lakini hakina majibu ya mipango yake!
 
Katika kipindi cha UZALENDO ambacho huwa kinarushwa kila alhamis-ITV, jana wapipata ugeni kutoka chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema ambapo katibu mkuu wa chama hicho DR SLAA alikuwepo na pia upande wa pili alikuwepo makamo mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Mh Mangula.

Mhe Dr Wilbrod Slaa ambaye aliwahi pia kuwa mbunge wa CCM na kujing'atua baada ya kutokuridhishwa na mambo yaliyokuwa yakiendelea ndani ya chama hicho ameeleza kwenye kipindi hicho kuwa alipokuwa mbunge alikuwa aliishi na mtu wa usalama wa taifa katika ofisi yake akiwa kama katibu wake ambaye ndiye alikuwa akiratibu shughuli zote za ofisi yake kwa muda wa miaka 14 ambapo aligundua wadhifa wa katibu wake huyo baada ya kutofautiana na waajiri wake kwa kutokulipwa posho hivyo kuhitaji msaada wa dr slaa.

Dr wilbrod slaa alizungumza hayo alipokuwa akijibu swali la mtangazaji wa kipindi hicho lililouliza kwanini wabunge wa CHADEMA wamekuwa wakizungumza mambo nyeti sana bungeni badala ya kufuata taratibu. Dr Slaa alisisitiza pia kuwa si jambo la kiungwana kuwaacha viongozi walihujumu taifa kwa kisingizio cha kulindwa na usalama wa taifa, lakini pia watu wa usalama wa taifa ndio wahujumu uchumi no 1 huku akichukulia mfano wa wizi wa EPA ambapo kiongozi mkubwa wa usalama wa taifa alihusika kulihujumu taifa.

Ama kwa hakika ninaweza nikasema DR SLAA CCM walimshindwa tangu kitambo kwani pamoja na kutuma watu wa usalama kumchunguza lakini bado wahakuibuka na hoja yoyote ya kummaliza alipokuwa akigombea URAIS mwaka 2010
 
Samahani, hakuwahi kuwa mbunge wa CCM, Huyo usalama alikuwa naye akiwa CHADEMA. Hebu rekebisha kabla Ritz hajakulima. Dk Slaa ni jembe linalohamasisha kulima. Sio jembe butu.
 
Naona una like ya DR Slaa ,nataka kujua je DR Slaa aliwahi kuwa mbunge kupitia CCM manake tunaambiwa alipotaka kugombea alipendekezwa na jina likakatwa Dodoma ndipo alipogombea kupitia chadema
 
unaishi nchi gani wewe?
Mimi sigombani na wewe Kamanda. Dr Slaa alipotaka kugombea ubunge kupitia CCM Jina lake lilikatwa kwa mizengwe. Ndipo watu wa jimbo lake walipomfuata na kumuomba agombee kupitia Chama kingine. Na Dk akaamua kupitia CHADEMA. Soma kitabu cha historia yake. Sio kwamba nataka kukunyongonyesha. Sisi sote huwa tunaendelea kujifunza na kusoma kila siku. Ila nimeipenda sana mada yako. hii ni kasoro ndogo sana, lakini inaweza kuharibu utamu.

Kuhusu kuzaliwa, nilizaliwa Tanganyika, unaijua?
 
Dr Slaa Ni akili kubwa na maccm Ni akili ndogo. IQ ya Dr Slaa Ni kubwa kuliko IQ za wajumbe wote wa sekretarieti ya CCM zikichanganywa. Kwa minajiri hii hakuna mwanaccm yeyote wa kusimama na Dr Slaa jukwaani au katika mdahalo. Only umburula wetu watanzania umetufanya tushindwe kugundua hazina iliyopo kwa Dr Slaa. Hebu fikiria kama tungemchagua kuwa rais 2010 na akashusha bei ya cement hadi shs 5000, akina Lumumba buku Saba na watanzania wengine wangekaa kwenye nyumba za tembe?
 
Duh,ila namsifu Mangula angalau amethubutu kukubali mdahalo na DK SLAA, Wenzake akina Kikwete mara kadhaa wanamkwepa...
 
Dr Slaa Ni akili kubwa na maccm Ni akili ndogo. IQ ya Dr Slaa Ni kubwa kuliko IQ za wajumbe wote wa sekretarieti ya CCM zikichanganywa. Kwa minajiri hii hakuna mwanaccm yeyote wa kusimama na Dr Slaa jukwaani au katika mdahalo. Only umburula wetu watanzania umetufanya tushindwe kugundua hazina iliyopo kwa Dr Slaa. Hebu fikiria kama tungemchagua kuwa rais 2010 na akashusha bei ya cement hadi shs 5000, akina Lumumba buku Saba na watanzania wengine wangekaa kwenye nyumba za tembe?

Mkuu naomba nikure kebishe kauli kidogo,"hapo hebu fikiria kama tunge mchagua kuwa rais 2010" ni hivi mkuu, dr slaa wananchi walimchagua 2010 na akashinda.ila Kikwete na magamba wenzake plus lipumba ndio waliiba kura.lakini kiukweli na kiuhalali dr slaa alishinda.wewe unadhani kikwete mwananchi gani ambaye ni maskini atamchagua kikwete? Yaani kikwete ni mzigo na janga bora muda wake uishe akafie mbele.
 
View attachment 105205

1:00 USIKU leo alhamisi Usikose kuangalia kipindi kipya kabisa cha UZALENDO kikuhusu mambo yanayojiri katika medani ya siasa nchini na waalikwa wakiwa wanasiasa kutoka vyama tofauti wakichambua hoja mbalimbali kuhusiana na hali inavyoendelea nchini.

Katika kipindi cha leo tutakuwa na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Bwana Philp Mangula na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk.Wilbroad Slaa

Marudiooooo lini?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom