Lissu: Wanaohama CHADEMA wasiwatishe

Lissu: Wanaohama CHADEMA wasiwatishe

Wenye akili za kununulika!? Mwambieni aruhusu mikutano ndo uje tena na unafiki wako.
 
Wahenga walisema dalili ya mvua ni mawingu.
Hisia zinanituma kuamini kuna mpango madhubuti kwa ku disolve upinzani kiasi cha kubaki una mpinzani dhaifu goigoi atakayeambia cha kufanya

Na hatimaye kuongeza muda wa kutawala iwe miaka 7 au 10 au hadi achoke

Hizi ni hisia tu sio lazima ziwe kweli au ukubaliane nazo.
 
Jaman upinzani unaimarika.
Mark my word dudes!!!
 
Sugu (Josef Mbilinyi) na Godbless Lema kwangu mimi hawa jamaa ndiyo wapinzani wa kweli na siyo hao wengine.
Hawa jamaa mmoja wao akiondoka CHADEMA kwenda CCM hapo ndiyo nitakapotambua kuwa kweli kuna hoja za msingi za kumuunga mkono rais ukiwa CCM na wala siyo ukiwa Upinzani.
Nawasilisha.
 
Mimi in MTU Wa Kigoma ila ndugu zangu akina David kafulila Machali na wengineo waliotangulia wametushusha sana yaani Wa Kigoma hawana msimamo au njaa sana
 
Ninaendelea kushangazwa na sababu zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani pale wanaporudi ama kuhamia ccm.

Porojo ni nyingi, lakini kwa kifupi, ni kama wamemfuata mtu na si chama. Chama ni kile kile, sera ni zile zile. Lakini wanapotoa sababu zao, unaona kabisa ni kwasababu ya mtu, ni kwasababu ya Maghufuli, na si kwasababu ya chama.

Wengine ambao wako ccm, wanasema Maghufuli anafanya yale ambayo upinzani waliahidi kuyafanya, kwahiyo ndiyo maana wengi walioko upinzani wanarudi ccm.

Hii situation yote inatufanya tuonekane kama hamnazo! Ngoja nikusanye sababu zilizotajwa na baadhi ya viongozi wa upinzani kuhusu kuhamia ama kurudi ccm, halafu tuone kama akili zao hao watu si mbovu.

Kuna mmoja wa huko Siha mkoani Kilimanjaro, ambaye ni diwani, katoa sababu kuwa eti “ccm ni chama kinachofanya siasa za maendeleo na siyo za kulumbana na kupoteza muda”. Kuna ukweli gani hapo? Anafahamu alichoongea? Sababu iliyomfanya akajiunga na upinzani hapo mwanzoni, kwa maoni yake, hazipo tena kwasababu ccm inafanya siasa za maendeleo!

Nitaweka hizo sababu za wengine, halafu tujadili.
 
wanafuata ugali tuu,wew mtu ulikuwa mbunge moja ya nyadhfa kubwa nchi hiialafu leo unaniambia kuwa unabwaga ubunge unaamua kwenda chama kingine kuwamwanachama wa kawaida tuu,hivi inaingia aikilini kweli,sisemi kuwa haiwezekani ila kwa kiwango cha njaa walizo nazo wanasiasa wetu walio wengi sidhani kama hili linawezekana
 
Hii dhana ya kusema Chama ni kile kile na itikadi ni ile ile haina mashiko katika uwanja wa siasa ambazo zinachagizwa na mazingira.

Kiongozi mkuu wa chama ndiye chachu katika mageuzi, mabadiliko na maendeleo ndani na nje ya chama.

Chama kile kile na itikadi ile ile lakini CCM ya wakati wa Mwl. Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete inatofautiana kulingana na uongozi wa kila mmojawapo.

Yes, Kiongozi Mkuu wa chama ni muhimu kama driver bila regardless una abiria wana uwezo gani. Driver akiwa mzuri hata kama gari linamatatizo anaweza kumudu kuliongoza kwa weledi

Kwa nini unadhani Mbowe anaweza kuongoza CHADEMA badala ya Prof. Safari kama chama ni kile kile na Itikadi ni ile ile!

Hata nchini Uingereza pamoja na kwamba chama chenye wabunge wengi ndichp huunda serikali lakini kama kiongozi wa chama hana uwezo hata chama hakiwezi kushinda uchaguzi hata kama wagombea wake wa ubunge watakuwa wana uwezo mkubwa kiuongozi.
 
Mkuu usijisumbue CCM hawana hoja....walichofanikiwa ni kubana mihimili ya dola......

Pia wanafaidika na ufinyu wa elimu yetu watanzania
 
Hii dhana ya kusema Chama ni kile kile na itikadi ni ile ile haina mashiko katika uwanja wa siasa ambazo zinachagizwa na mazingira.

Kiongozi mkuu wa chama ndiye chachu katika mageuzi, mabadiliko na maendeleo ndani na nje ya chama.

Chama kile kile na itikadi ile ile lakini CCM ya wakati wa Mwl. Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete inatofautiana kulingana na uongozi wa kila mmojawapo.

Yes, Kiongozi Mkuu wa chama ni muhimu kama driver bila regardless una abiria wana uwezo gani. Driver akiwa mzuri hata kama gari linamatatizo anaweza kumudu kuliongoza kwa weledi

Kwa nini unadhani Mbowe anaweza kuongoza CHADEMA badala ya Prof. Safari kama chama ni kile kile na Itikadi ni ile ile!

Hata nchini Uingereza pamoja na kwamba chama chenye wabunge wengi ndichp huunda serikali lakini kama kiongozi wa chama hana uwezo hata chama hakiwezi kushinda uchaguzi hata kama wagombea wake wa ubunge watakuwa wana uwezo mkubwa kiuongozi.
Si mseme wanamfuata Maghufuli na siyo chama? Au pengine wananchi huwa hawafuati sera, bali personalities nk. Ndo maana hata midahalo hakuna wakati wa uchaguzi wa rais, na wananchi wanaona sawa kabisa!
 
Wanahama kwa sababu wanamuunga mkono Rais Magufuli, yale yanayofanywa na serikali yake ndio yale waliyokuwa wakiyapigania walipokuwa upinzani na wote huandika barua moja yenye maneno sawa wanapohama😀😀😀
 
Ninaendelea kushangazwa na sababu zinazotolewa na baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani pale wanaporudi ama kuhamia ccm.

Porojo ni nyingi, lakini kwa kifupi, ni kama wamemfuata mtu na si chama. Chama ni kile kile, sera ni zile zile. Lakini wanapotoa sababu zao, unaona kabisa ni kwasababu ya mtu, ni kwasababu ya Maghufuli, na si kwasababu ya chama.

Wengine ambao wako ccm, wanasema Maghufuli anafanya yale ambayo upinzani waliahidi kuyafanya, kwahiyo ndiyo maana wengi walioko upinzani wanarudi ccm.

Hii situation yote inatufanya tuonekane kama hamnazo! Ngoja nikusanye sababu zilizotajwa na baadhi ya viongozi wa upinzani kuhusu kuhamia ama kurudi ccm, halafu tuone kama akili zao hao watu si mbovu.

Kuna mmoja wa huko Siha mkoani Kilimanjaro, ambaye ni diwani, katoa sababu kuwa eti “ccm ni chama kinachofanya siasa za maendeleo na siyo za kulumbana na kupoteza muda”. Kuna ukweli gani hapo? Anafahamu alichoongea? Sababu iliyomfanya akajiunga na upinzani hapo mwanzoni, kwa maoni yake, hazipo tena kwasababu ccm inafanya siasa za maendeleo!

Nitaweka hizo sababu za wengine, halafu tujadili.
Wao wanachoshindwa kuelewa kuanzia mwenyekiti hadi hawa kina jinga lao & co malumbano ni chachu ya maendeleo . Hata huko ulaya walilumbana wee mpaka wakapata maendeleo. Ni hatari sana kiongozi kufikiria ana akili nyingi na ni suluhisho la matatizo yoote kwenye taasisi? ukiona hivyo ujue huyo anataka kuabudiwa na kutukuzwa... lakini utukufu wa pekee huletwa na mungu wala hauji kwa hutuba za mazabahuni
 
Moderator , Invisible . Thread niliyoanzisha ikitaka tujadili sababu za viongozi wa upinzani kuhamia au kurudi ccm, imeunganishwa na thread hii ambayo Lissu alisema “wanaohama chadema wasiwatishe”. Uhusiano kato ya thread hizo mbili Uko wapi hadi ziunganishwe? Hapo kuna mijadala miwili ya tofauti kabisa. Kama ikitokea thread imeungwa na iko sahihi, basi huwa naignore ama kuwashukuru. Lakini mara nyingi siyo sahihi hata kidogo. I’m wondering g if kuna mtu ambaye huwa tunapishana humu halafu yeye ni moderator. Please looks at this issue wakuu.
 
Mh.Tundu Lissu atabaki kuwa Mwanasiasa wa karne.
Ccm wameamua wammimimie marisasi,ili wasikosolewe kwenye wizi wao
 
Back
Top Bottom