Lissu: Wanaohama CHADEMA wasiwatishe

Lissu: Wanaohama CHADEMA wasiwatishe

Hivi chadema nyie ndio mmekuwa mboga kiasi hiki? [emoji28][emoji28][emoji28] yani kwamba sasa na ninyi mnafika bei? Alafu sasa mnakuja kulilia hapa kwamba mnafika bei bila aibu?

Najiuliza tu, mngepewa nchi ingekuwaje? Maana hao mnaosema wamenunuliwa ndio wamgekuwa mawaziri wenu hao! Ndio ambao wangekuwa wawakilishi wa rasilimali zetu dhidi ya mabepari, sasa ingekuwaje?

Wanaume wazima mnalia kununuliwa kweli bila aibu?
Nilishasema humu na ninaendelea kusema, Hakuna chama pinzani kilicho serious wala hakuna chama pinzani kinachofanya kazi kikidhamiria kushika dola.

CCM sio chama imara, wala CCM haipendwi, wananchi hawashindwi kuiacha CCM ila sasa wakiacha CCM watamchagua nani?
Ni bora CCM mara 10 kuliko kuchagua chama pinzani, huko vyama pinzani kuna wanafiki sana, mtu yuko upinzani anahamia chama tawala kirahisi tu alafu tukiamini chama?

Mtu wa chama pinzani anateuliwa kua RC alafu tuamini kwamba kuna chama pinzani?

CCM ni hovyo sana lakini vyama pinzani ndio hovyo zaidi, sio Chadema wala CUF wala ACT wote hovyo tu hakuna mwenye unafuu.

Muendelee kununuliwa na mngepewa nchi mngeiuza kwa wazungu mchana kweupe.
 
Kwa wenye akili wangekaa kimya.
Sasa hivi wako bize mitandaoni wakiwaambiwa wananchi;
TUPENI NCHI ILA MJUE TUNANUNULIKA. Sasa sijui ni mwananchi gani wa kuwachagua.
 
Hivi CHADEMA nyie ndio mmekuwa mboga kiasi hiki? Yani kwamba sasa na ninyi mnafika bei? Alafu sasa mnakuja kulilia hapa kwamba mnafika bei bila aibu?

Najiuliza tu, mngepewa nchi ingekuwaje? Maana hao mnaosema wamenunuliwa ndio wamgekuwa mawaziri wenu hao. Ndio ambao wangekuwa wawakilishi wa rasilimali zetu dhidi ya mabepari, sasa ingekuwaje?

Wanaume wazima mnalia kununuliwa kweli bila aibu?

Aisee ni aibu kuwa na taifa linalonunua wapinzani kila kitu kina mwisho wake sasa ombea mwisho uwe mwema usije ukakutafuna

Unarusha mawe wakati nyumba yako ina vioo ngoja tusubiri Siku zote muda huongea
 
Ili Mti Unawiri vizuri Sharti Majani yadondoke yaliyochoka yadondoke. (Kwa wanaojua miti). Kwa wasomaji wa Biblia Yesu akawauliza wanafunzi wake, "Je Nanyi mwataka kuondoka?" Ni vema miti ipukutike majani yaliyochoka
Haka kamastar nakapata wapi mkuu
 
Hivi kama watu wanaofaidika na kuwa wanachama wa HADEMA, wanalipwa mafao posho na mishahara minono wananunulika kirahisi hivi, vipi kuhusu hawa wanachama njaa ambao ndiyo wengi, ikitangazwa bei si watahama wote?
 
Mapinduzi ya chama nitayafanya mimi pindi nitakapo anzisha chama changu hicho atakayejinga hakuna kutoka. Sahiz mauza uza tuu naona hapa
 
Zikiwa zimebaki siku chache Mkutano Mkuu wa hawa mabwana uanze,ni lazima maandalizo ya kuwapokea wasaliti yaanze sasa na mojawapo ni wasaliti kutangaza kujiuzulu hivyo hili zoezi linaweza kuendelea mpaka siku moja kabla ya Mkutano Mkuu kuanza.

Wote hawa watapokelewa siku ya Mkutano Mkuu mbele ya Baba Mflame huku Camera zikimulika.

Wanakoelekea watatamani hata kununua kivuli cha CHADEMA kwa jinsi wanavyoiogopa maana CHADEMA haiwezi kufa na uwepo wake ni tishio kwa hawa waoga.
it's very sad kuona wakati sasa watumishi wa Mungu (Askofu Bagonza, Munga, etc) wakiinuka kuanza kui challenge status quo kuhusu masuala ya governance, wanasiasa uchwara (ambao wananchi walikuwa wanawategemea kuwaongoza dhidi ya status quo) ndiyo kwanza wanasaliti mapambano!
 
Mwanao anafuata malezi yako, ukimlea kifisadi atakuwa fisadi, ukimlea bila maadili basi naye Ataishi hivyo. Lakini pia mwanao mwanao akiona maadili yako hayamjengei maisha basi atwafuata waungwana wenye maadili.

Chadema chama kilijuharibia maadili NA walezi waliokuwa NA maadili mazuri waliterekezwa NA kutukanwa. Zote hizi zinachangia hii hama hama
 
Wakati mwingine kudondoka kwa jani ni faida kwa mti.
 
Napenda kuchukua fursa hii ya Jukwaa hili kuwapa Taarifa wale wote hasa viongozi wa Chadema wanaotaka kuondoka wafanye Hivyo haraka sana bila kupoteza muda. Sisi kama Chama tuna malengo yetu sasa hii ya kuondoka kwa awamu mnatuvurigia mipango.

Nataka kufunga Mlango jamani malizeni zoezi lenu na CCM mapema.
 
Wapinzani ni wananchi si viongozi. Viongozi wakiondoka wapinzani watabaki.
 
YES , badala ya kupoteza za pesa mara mbili maana kuna na kumshawishi ajiudhuru na kuna za uchaguzi basi elekezeni nguvu kupeleka huduma kwa wananchi wala haita hitajika nguvu wenyewe tu watajileta chamani bila shuruti wala bunduki.

Na ujio wa wapiga kura ni wadhamani na faida kubwa sana kuliko ujio wa mwana siasa mmoja ambaye bado atawaingiza gharama nyingine ya kutumia mafuta ya magari ya polisi na maji ya kuwasha pamoja na mabomu ya mochozi + dkambi ya kuua na kujeruhi ili kumtangaza mshindi aliye shindwa katika jimbo au kata aliyo jiudhuru huyo aliye gharamiwa

Maana haiingii akilini ugharamie mambo yooote ikiwemo manunuzi, gharama za uchaguzi na mafuta ya gari za polisi halafu finally ushindwe !!!!!!!!!! Haiwezekan

Hivyo ni hasara kununua mtu mmoja kwa gharama mara tatu au nne kuliko kujenga imani kwa watu wengi bila gharama kubwa yenye dhambi ndani yake.
 
Hakika umeongea neno zuri mno.
Umetumia hekima na busara za hali ya juu kwa jambo hili.
 
Wameshaona hatuelewi tunakokwenda, hii nayo wanadhani itavutia.
Na 2019 watatoa ajira na miradi kwa wingi. 2020 tutawapigia tena.
Walichosahau ni kwamba huwa hatuwaangushi. 2020 ushindi wa kishindo
 
Kusema chadeda isusie uchaguzi ni sawa na kuipa CCM ulaini wa kuyarudisha majimbo yote yaliyokuwa mikononi mwa UKAWA na ACT. Aliyependekeza na kulisimamia hilo hana tofauti na mtu aliyenunuliwa ila anaogopa tu kusema na mimi nahamia upande uleee kumuunga mkono mkuuu.

Sisi tunafanya siasa wenzetu wanafanya biashara. Wajinga ndiyo ndio waliowao na mimi kesho nitaipangusa vumbi ileeee kadi yangu.

Kushiriki uchaguzi kunakipa fursa chama cha siasa ya kuujua uwanja wa siasa ukoje leo kulinganisha na jana ili upange ya kesho vizuri. Ukisusa kama Raila wenzako walaah!!!

Upinzani ukifa nchini nchi haitakuwa tamu hata kwa wana CCM wenyewe. Hata wewe unaeshangilia leo dalili za upinzani kufa iko siku utajutia hata wewe kama wanavyojuta leo akina nanihii waliookolewa na Maulid Kitenge siku ile.
 
Siku za hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la wanachama wa UKAWA kuvihama vyama vyao na kuhamia CCM, huku baadhi yao waki-sacrifice nafasi zao za uongozi ndani ya vyama hivyo au kupitia vyama hivyo, nafasi ambazo kwa kweli wametumia nguvu kubwa sana kuzipata; na zikiwa zinawapa maslahi mazuri kabisa.

Kama kawaida yao wana-UKAWA wamekuwa wakimnyoshea kidole jirani, kwamba ndiye anayehusika na hama hama hiyo. Wamekuwa wagumu sana kuyaona matatizo yao ya ndani na hasa kutoka kwa viongozi waandamizi wa vyama vyao, na cha ajabu sana kila aliyeongea lolote la kuwakosoa viongozi hao ameonekana ni mtu asiye na akili na hivyo kuambulia matusi ya ajabu ajabu.

Napenda kutoa wito kwa wana-UKAWA wote kujitathmini kwanza ndani kabla ya kumnyoshea kidole jirani. Hao wanaohama ni watu wenye akili zao timamu; wanajua gharama ya maamuzi yao. Wanajua ni nini watakikosa kwa kuchukua maamuzi hayo magumu. Acheni kujidanganya kwamba mnaongozwa na Miungu Watu, wasiokosea, wasiokuwa na tamaa za mali, wazalendo wa kweli; na badala yake wafanyieni tathmini viongozi wenu na hasa kwa kujiuliza ni wapi wanakotaka kuwapeleka. Kinyume na hapo tutarajie UKAWA kumomonyoka zaidi, na uchaguzi wa 2020, umoja huo utakuwa hoi kabisa.
 
Back
Top Bottom