Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,568
Mashabiki wa Simba wameleta video hii ya Tundu Lissu akifafanua kuhusu mwaka 1993 kwenda uwanjani kushuhudia mchezo wa Fainali kati ya Simba dhidi ya Stella Abijan ya Ivory Coast.
Mashabiki wa Simba kwa sasa wameibua video hiyo hapo juu ikimuonesha Lissu akielezea ushiriki wake katika mchezo wa fainali wa Simba dhidi ya Stella Abijan mwaka 1993.
Lissu akihojiwa na Wanahabari kama anaendaga kwenye viwanja vya mpira amejibu kuwa, hakuwahi kwenda tena uwanjani kuangalia soka tangu mwaka 1993 alipoenda kushuhudia mchezo wa Simba vs Stella Abijan ambapo Mashabiki wa Simba walikaribia kumvua suruali.
Zaidi ya hayo Mashabiki wa simba wanaendelea kuleta vithibitisho vingine kuonesha waliwahi kucheza fainali ya michuano ya Afrika.
Tazama tiketi hii hapa chini: