mbuguni
JF-Expert Member
- May 15, 2013
- 568
- 134
Ukweli ni kwamba Lissu hana chochote zaidi ya kucheza na lugha, nimeshawahi sema tena humu. Lisu ni mjanja katika maneno na siyo katika hoja. na siku zote wajenga hoja hawapendwi. Watu tunashadaia sana mbunge anaposimama na kunena mabaya juu ya chama fulani iwe kwa ukweli ama uongo. Lisu kama mwanaharakati na siyo mwanasiasa lazima aongee kwa style hiyo ni kama ilivyo kwa wengine wengi tu tunaowajua. Kwa mfano Lipumba pale Msikitini (ingawa inasemekana Nchemba ndiyo aliitengeneza Video hiyo) alikuwa anaongea yasiyo mema lakini waliokuwepo pale walikua wanashangilia na kumuona shujaa.
Msimamo wangu utabaki palepale kuwa Lisu no mchezea maneno, populist, mpenda kuonewa huruma na asiweza kusimama mwenyewe kwenye siasa bila kivuli cha mtu mwingine (nacho kwa sasa ni CCM).
We gamba ni lini lissu kashindwa hoja?
Siku zote ccm ndio hawana hoja dhaidi yaku yakucheza na maneno na kutulaghai kwa maneno ambayo sasa tushayazoea kuwa ni uzushi na uongo mtupu.