Lissu ametengwa? Tazama kinachoendelea

Jamaa anakusanya ushahidi wa kupewa hela kwenye NGO maana mabeberu wanahitaji ushahidi.
 
Mkuu Countrywide , japo Chadema wenyewe hawajasema, hizi ziara za Lissu, na mikutano yake, ni ziara binafsi ambazo haziratibiwi na chama, bali ni yeye Lissu ninafsi kama Lissu na atatumia fedha zake binafsi!.

Kwa vile buyu la asali limeishatua Chadema, zingekuwa ni ziara za kichama, angeisha wezeshwa.
P
 
Tuliwaambia mkimalizana na Magufuli mtaanza kumalizana wenyewe kwa wenyewe.
Na nyie mmemalizana na nani maana mnaparurana wenyewe kwa wenyewe. Mpona vs mwigulu?
Acha kupayuka kama chizi wewe
 
Elimu inayotolewa kuhusu katiba mpya na muundo mpya wa tume ya uchaguzi hutegemea na miundombinu ya eneo husika. Hili wala siyo suala la kutaka kuonyesha ufahari, bali suala muhimu ni kukimbizana na muda ili kuwafikia wananchi wengi ipasavyo wanaoishi vijijini ambao wametopea katika umaskini wa kutisha. Ni vyema kutafakari nukuu ifuatayo kutoka katika maandiko matakatifu,

ZABURI 20

7. Wengine hujigamba kwa magari ya vita; na wengine hujigamba kwa farasi wao. Lakini sisi twajivunia Mwenyezi - Mungu, Mungu wetu.

8. Hao watajikwaa na kuanguka; lakini sisi tutainuka na kusimama imara.
 
Utafikiri kimetengenezwa na watoto wadogo au unaweza ukadhani ni kichanja cha kuanikia viombo?
Ila ungetuletea na ujumbe wake.
Zaidi, hata Tanzania si ni hivyohivyo, kuna mtu alikua bize kununua mandege huku mahospitalini hajuna dawa, wanafunzi wanasomea kwenye madarasa mabovu.
 
Huu ni uchuro kabisa yaani mgombea Uraisi mnamuandalia banzi la kuanikia migebuka eti ni jukwaa😵😵😵
 
Duh tutaona mengi sana
 
si walisemaga hicho sio chama bali ni genge la wahuni🤣🤣🤣
 
Mbowe kashalewa asali..Lissu alisha poteza credibility yake yoteee ..kwakifupi kinachoendelea cdm kwasasa ni kujitia u busy tuu usio na production yoyote..
 
Lissu alipofikia bado kidogo aonje sumu kwa ulimi.Mwenyekiti hakuwa na mpango na mikutano ya hadhara ila alikuja kushtuliwa na zile shutuma za makamu wake kuhusu nusu mkate morogoro.Tujiulize km makamu mwenyekiti hajui wanalidhiana nn haya ni maridhiano gani???? Km mwenyekiti mikutano yake dakika zote ni kumponda mwendazake na kujisifu alivyokaa gerezani mnategemea nn??? Yani unaruka na chopa unakusanya wanakijiji jua kali kuja kuwaambia ulivyokaa jela??? Mikutano ya Mbowe imekosa hoja wananchi wanasombwa na upepo wa kushangaa chopa
 
Mimi nipo nje ya MADA hivi Watanzania TUNATAKA Rais awe na vigezo gani? Je,TUNATAKA Rais atakaye wafanyia nini Watanzania?

Angalizo TABIA zao tumezielewa je watakidhi vigezo tunavyovihitaji?Kuna BAADHI ni wabishi na WAKALI Sana katika masuala mbalimbali wengine ni wakatili mno hatatunavyoishi nao wanajionyesha.Je,wakikabidhiwa watabadili TABIA walizo nazo za kulitj
 
..mtoa mada anataka tusisikie HOJA za Lissu.

..wananchi wa hapo alipohutubia Lissu hawana uwezo wa kutengeneza majukwaa ya bei mbaya. Je, mlitaka LIssu asitoe darasa la elimu ya katiba na haki za wananchi?

..mimi nampongeza Lissu kwa kuwafikishia elimu wananchi hao bila kujali hali yao ya umasikini.

..CCM wangefika hapo wangetumia majukwaa ya bei mbaya, wangengurumisha ma-V8, na kutumia wasanii wa bongo-flavour kulaghai wananchi.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…